Tuesday, September 27, 2016

HATIMAYE MKOA WA SIMIYU WAPATA HOSPITALI TEULE YA RUFAA YA MKOA

Na Stella Kalinga
Hatimaye Hospitali ya Somanda iliyokuwa inamilikiwa na Halmashauri ya Mji wa Bariadi yakabidhiwa rasmi  kwa Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu  na kuwa Hospitali Teule ya Rufaa ya Mkoa huo.

Makabidhiano hayo yamefanyika  kati ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Melkizedek Humbe na  Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Jumanne Sagini mjini Bariadi,  mbele ya Uongozi wa Mkoa, Halmashauri na baadhi ya watumishi wa Hospitali.

Katika Makabidhiano hayo Katibu Tawala Mkoa amekabidhiwa baadhi ya watumishi na Mali kutoka katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi, ambapo Sagini amesema watumishi hao pamoja na wale waliokuwa wakisimamiwa na Katibu Tawala Mkoa hapo awali, wote watasimamiwa na Sekretarieti ya mkoa wa Simiyu, chini ya uangalizi wa Mganga Mkuu wa Mkoa kwa kushirikiana na Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa

Akizungumza kabla ya makabidhiano hayo Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Jumanne Sagini amewaasa watumishi  wa Hospitali hiyo kufanya kazi kwa weledi na kuhakikisha wanatoa huduma kwa wagonjwa kulingana na taratibu, maadili na miongozo ya taalum ya kitabibu.

Sagini amesema baadhi ya watumishi wa Idara ya afya wamekuwa wakitumia lugha mbaya isiyowaridhisha wateja wao na hivyo kushindwa kuwapa huduma wanayostahili kwa kuwa baadhi ya wananchi wamekuwa wakikatishwa tamaa.

“Nisingependa kusikia kuna watumishi wanatumia lugha mbaya kwa wagonjwa, wengine wanapowahudumia mama wajawazito wanawatolea maneno makali ambayo hayawapi faraja, tabia hiyo isionekane kabisa katika Hospitali yetu,  zingatieni maadili ya kazi zenu na muwape wananchi huduma wanayostahili ili waendelee kuwaamini’ alisema Sagini.

Aidha, Sagini alimtaka Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo Teule ya Mkoa, Dkt. Fredrick Mlekwa  ashirikiane na viongozi wengine kuhakikisha Hospitali hiyo inatoa huduma bora zinazolingana na hadhi iliyonayo kwa sasa ili wananchi wa Mkoa wa Simiyu wanufaike kwa kupata huduma bora za Rufaa.

Wakati huo huo Mkurugenzi wa Halmasahuri ya Mji amewataka Watumishi waliokabidhiwa kwa Katibu Tawala Mkoa watumie fursa hiyo kufanya kazi kwa bidii zaidi  ili huduma itakayotolewa iendane na hadhi ya Hospitali Teule ya Rufaa ya Mkoa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashuari ya Mji wa Bariadi, Mhe. Robert Lweyo ametoa wito kwa Serikali kuu kuhakikisha inajenga majengo bora yatakayokuwa na hadhi ya Hospitali ya Mkoa.
Naye Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo Teule ya Rufaa ya Mkoa, Dkt. Fredrick Mlekwa amesema Wananchi wa Halmashauri zote katika Mkoa wa Simiyu watarajie huduma bora zitakazokidhi kiwango.

Kabla ya Hospitali ya Somanda kuwa Hospitali Teule ya Rufaa ya Mkoa ilikuwa inahudumia wananchi kutoka katika Halmashauri ya Mji Bariadi na Halmashauri Wilaya  jirani za Bariadi, Itilima na baadhi ya vijiji vya  vya Wilaya ya Busega, lakini kuanzia sasa itahudumia Halmashauri zote sita ikiwemo Maswa na Meatu kwa huduma za Rufaa.
Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Jumanne Sagini (kushoto) na Mkurugenzi wa Mji wa Bariadi , Melkezedeki Humbe(kulia) wakikabidhiana nyaraka mara baada ya makabidhiano ya Hospitali ya Somanda iliyokuwa ya Halmashauri ya Mji ambayo imefanywa kuwa HospitaliTeule ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu.

Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Jumanne Sagini (kushoto) na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi , Robert Lweyo wakipeana mikono baada ya makabidhiano ya nyaraka za Hospitali ya Somanda iliyokuwa ya Halmashauri ya Mji Bariadi ambayo imefanywa kuwa Hospitali Teule ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi , Melkezedeki Humbe (kulia) akizungumza na baadhi ya Viongozi wa Mkoa, Halmashauri na Hospitali ya Somanda kabla ya makabidhiano Hospitali ya Somanda iliyokuwa ya Halmashauri ya Mji Bariadi, ambayo imefanywa kuwa Hospitali Teule ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu.


Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Jumanne Sagini(katikati) akizungumza na baadhi ya Viongozi wa Mkoa, Halmashauri na Hospitali ya Somanda kabla ya makabidhiano Hospitali ya Somanda iliyokuwa ya Halmashauri ya Mji Bariadi, ambayo imefanywa kuwa Hospitali Teule ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi , Robert Lweyo akizungumza na baadhi ya Viongozi wa Mkoa, Halmashauri na Hospitali ya Somanda kabla ya makabidhiano Hospitali ya Somanda iliyokuwa ya Halmashauri ya Mji Bariadi, ambayo imefanywa kuwa Hospitali Teule ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu.

Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Jumanne Sagini(katikati) akizungumza na baadhi ya Viongozi wa Mkoa, Halmashauri na Hospitali ya Somanda kabla ya makabidhiano Hospitali ya Somanda iliyokuwa ya Halmashauri ya Mji Bariadi, ambayo imefanywa kuwa Hospitali Teule ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu.

Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Jumanne Sagini akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Viongozi wa Mkoa, Halmashauri na Hospitali ya Somanda baada ya makabidhiano Hospitali ya Somanda iliyokuwa ya Halmashauri ya Mji Bariadi, ambayo imefanywa kuwa Hospitali Teule ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu.
Baadhi ya Viongozi wa Mkoa, Halmashauri na Hospitali ya Somanda wakimsikiliza Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Jumanne Sagini (hayupo pichani) kabla ya makabidhiano Hospitali ya Somanda iliyokuwa ya Halmashauri ya Mji Bariadi, ambayo imefanywa kuwa Hospitali Teule ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu.


Sehemu ya Jengo la Utawala la Hospitali ya Somanda iliyokuwa inamilikiwa na Halamshauri ya Mji wa Bariadi  ambayo sasa ni Hospitali Teule ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu.






0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!