Monday, February 13, 2017

#JUKWAA LA BIASHARA SIMIYU# RC MTAKA AWAKARIBISHA WAWEKEZAJI WAZAWA KUWEKEZA SIMIYU

Na Stella Kalinga
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka ametoa wito kwa Wafanyabiashara wazawa kuwekeza katika mkoa huo na kuwahakikishia kuwa Serikali iko tayari kuwaunga mkono.

Mtaka amesema hayo katika ufunguzi wa Jukwaa la biashara lililofanyika leo mjini Bariadi, ambalo limeandaliwa na Kampuni ya Magazeti ya Serikali(TSN) ikishirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.

Amesema fursa takribani 14 zimetangazwa katika maeneo mbalimbali ya mkoa huo baada ya utafiti uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Kiuchumi na Kijamii(ESRF) uliopelekea kuandaliwa kwa Rasimu ya mwongozo wa uwekezaji wa mkoa.

"Tunataka kutransform mkoa wa Simiyu na kuufanya kuwa wa tofauti katika kuelekea  kwenye uchumi wa kati, Tungehitaji kujenga mkoa tofauti na watu wengine waje wajifunze; yapo tuliyoanza kutekeleza na yapo yaliyo kwenye pipeline" alisema.

Mtaka amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri zote mkoani humo, kutoweka urasimu usio wa lazima kwa wawekezaji wanaotaka kuwekeza katika maeneo yao.

Ameongeza kuwa mkoa wa Simiyu umeanzisha mfumo tofauti wa kushirikisha Sekta binafsi katika utekelezaji wa Sera ya Tanzania ya Viwanda ambapo wameanza kwa Halmashauri kuendesha viwanda vidogo kwa ubia na Vikundi vya Vijana; Wilaya ya Meatu(kiwanda cha kusindika maziwa) na Wilaya ya Maswa (Kiwanda cha kutengeneza Chaki).

Aidha, pamoja na kuwepo kwa viwanda vidogo  Mtaka amesema Serikali mkoani Simiyu imedhamiria kuwa na viwanda vya kati na vikubwa kwa lengo la kuyaongezea thamani mazao ya kilimo na mifugo.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, ambaye pia ni Mtaalam wa masuala ya biashara, Profesa Elisante Ole Gabriel amewataka wafanyabiashara kuwa na utamaduni wa kulipa kodi kwa hiari ili biashara zao ziwe endelevu.

Pia Profesa Ole Gabriel ametoa rai kwa wafanyabiashara wa Mkoa wa Simiyu kuzijua vema biashara zao na kufanya biashara hizo kimkakati hususani katika kubuni biashara zinazojibu changamoto za jamii na suala la huduma bora kwa wateja.

Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA), Ndg.Richard Kayombo ametoa wito kwa wafanyabiashara kutunza kumbukumbu za biashara zao ili walipe kodi kulingana mapato yao ili kuiwezesha serikali kupata kodi/mapato stahiki.

Naye Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali(TSN) ambao ndiyo waandaaji wa Jukwaa la biashara, Dkt. Jim Yonazi amesema wao wanaamini maendeleo ni Habari, hivyo wako tayari kufanya kazi na mkoa wa Simiyu kwa kuwa viongozi wake wanachukia kasi ndogo katika maendeleo.

"Wakati wengine wanaona Simiyu kama mkoa mpya sisi tunaona fursa, tumeamua kupeleka habari za uwekezaji na maendeleo ya mkoa huu sehemu mbalimbali duniani kupitia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) na sasa hivi watu zaidi ya 80,000 wanajua nini kinaendelea hapa" alisema.

Jukwaa la biashara mkoani Simiyu limeandaliwa na Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) yaani Habari Leo, Daily News na Spoti Leo kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu. Wadau wengine ni Benki ya Maendeleo(TIB), Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA), Benki ya NMB na Baraza la Uwezeshaji wananchi Kiuchumi (NEEC)

Jukwaa hilo limewahusisha viongozi wa Mkoa huo ngazi ya Mkoa na Wilaya, wafanyabiashara na wadau mbalimbali wa Maendeleo wa Mkoa huo.

Pichani ni Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhariri Mhe.Anthony Mtaka, Mhariri Mtendaji wa TSN, Dkt.Jim Yonazi, Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Sanaa, Utamaduni na Michezo, Profesa Elisante Ole Gabriel,Mkurugenzi wa Elimu ya Mlipa Kodi wa TRA Ndg Richard Kayombo, Katibu Tawala Mkoa Simiyu,Ndg.Jumanne Sagini, viongozi wengine wa mkoa huo pamoja na wadau mbalimbali wakiwa katika jukwaa hilo.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe.Anthony Mtaka akizungumza na wadau mbalimbali wa maendeleo wa Mkoa huo katika Jukwaa la biashara lililofanyika leo mjini Bariadi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe.Anthony Mtaka  wa pili kulia na Profesa Elisante Ole Gabriel wa pili kushoto wakiteta jambo katika Jukwaa la Biashara lililofanyika leo Mjini Bariadi, (kushoto) Katibu Tawala mkoa , Ndg.Jumanne Sagini.
Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali(TSN) Dkt. Jim Yonazi  akizungumza na wadau wa maendeleo ya Mkoa wa Simiyu wakati wa jukwaa la Biashara lililofanyika leo Mjini Bariadi.
Mbunge wa Jimbo la Busega Mhe.Raphael Chegeni akichangia jambo katika Jukwaa la Biashara lililofanyika Mjini Bariadi.
Baadhi ya Makatibu Tawala Wasaidizi wakifuatilia uwasilishwaji wa mada mbalimbali katika Jukwaa la Biashara lililofanyika Mjini Bariadi.
Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Ndg.Jumanne Abdalla Sagini akizungumza na wadau wa Maendeleo ya huo katika Jukwaa la Biashara Mjini Bariadi.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Sanaa ,Utamaduni na Michezo, Profesa Elisante Ole Gabriel akiwasilisha mada katika Jukwaa la Biashara Mjini Bariadi . 
Baadhi ya Viongozi wakifuatilia uwasilishwaji wa mada mbalimbali katika Jukwaa la Biashara lililofanyika Mjini Bariadi katika Ukumbi wa Kanisa Katoliki.
Kwaya ya Kanisa la AICT Bariadi wakiimba wimbo maalum wakati wa Jukwaa la Biashara katika Ukumbi wa kanisa Katoliki Mjini Bariadi.
Kutoka kulia,(walioketi) Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Festo Kiswaga, Mkuu wa Wilaya ya Busega, Tano Mwera, Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Prof.Elisante Ole Gabriel,  Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka , Mhariri Mtendaji wa TSN, Dkt. Jim Yonazi , Katibu Tawala Mkoa, Jumanne Sagini, Mwakilishi wa Benki ya Maendeleo (TIB) katika picha ya pamoja na washiriki wa  Jukwaa la Biashara  Mjini Bariadi.
Kutoka kulia,(walioketi)  Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Festo Kiswaga, Mkuu wa Wilaya ya Busega, Tano Mwera, Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Prof.Elisante Ole Gabriel,  Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka , Mhariri Mtendaji wa TSN, Dkt. Jim Yonazi , Katibu Tawala Mkoa, Jumanne Sagini, Mwakilishi wa Benki ya Maendeleo (TIB)katika picha ya pamoja na viongozi wa Mkoa wa Simiyu wakati wa Jukwaa la Biashara .
Kutoka kulia,(walioketi)  Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Festo Kiswaga, Mkuu wa Wilaya ya Busega, Tano Mwera, Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Prof.Elisante Ole Gabriel,  Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka , Mhariri Mtendaji wa TSN, Dkt. Jim Yonazi , Katibu Tawala Mkoa, Jumanne Sagini, Mwakilishi wa Benki ya Maendeleo (TIB)katika picha ya pamoja na Wabunge na Wakurugenzi wa Halmashauri wakati wa Jukwaa la Biashara Mjini Braiadi.
Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali(TSN) Dkt. Jim Yonazi akiwatambaulisha baadhi ya watumishi wa Kampuni ya Uchapishaji wa Magazi ya Serikali (TSN) kwa wadau wa Maendeleo y Mkoa wa Simiu wakati wa Jukwaa la Biashara Mkoani humo Mjini Bariadi.

1 comment:


  1. Hello.
    Mimi ni Mr Rahel binafsi wakopeshaji mkopo ambao hutoa maisha wakati nafasi ya mkopo kwa watu binafsi, makampuni ya biashara, bima, nk Je, katika shida yoyote ya kifedha au katika haja ya mkopo wa kuwekeza au unahitaji mkopo kulipa bili yako kutafuta hakuna zaidi kama sisi ni hapa kufanya matatizo yako yote ya kifedha kitu cha zamani. Sisi kutoa kila aina ya mkopo katika dhehebu lolote fedha kwa kiwango cha 2% bila fee.I upfront wanataka kutumia kati hii kubwa ya kukufahamisha kwamba tuko tayari kukusaidia kwa aina yoyote ya mkopo kutatua kwamba tatizo.Kama yako ya kifedha ndiyo basi kupata nyuma sasa kupitia barua pepe (rahelcohranloan@gmail.com) kwa maelezo zaidi, wewe ni sana makala.

    ReplyDelete

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!