Tuesday, February 7, 2017

SIMIYU YAWEZA KUINGIA 10 BORA PAMBA DUNIANI

       Na Stella Kalinga

*Mtaka asema wako tayari*

*Dk Bamwenda afichua kuwa Simiyu inaweza*

*Dk Diallo asisitiza ushirikishwaji sekta binafsi*

Serikali mkoani Simiyu imeshauriwa kuwekeza katika kilimo cha pamba kitakacholeta tija kwa haraka.

Mtafiti Mwandamizi wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na kijamii(ESRF), Dkt.Gratian Bamwenda ametoa ushauri huo mjini Bariadi leo katika kikao maalum cha kujadili Rasimu ya Mwongozo wa Uwekezaji katika mkoa wa Simiyu kwa mwaka 2017,  kilichowahusisha viongozi wa mkoa huo na wadau wa maendeleo kutoka sekta binafsi

Dkt. Bamwenda amesema endapo wananchi watatumia mbegu bora, mbolea, viuatilifu na kutumia huduma za maafisa ughani ipasavyo, uzalishaji wa pamba mkoani humo utaongezeka kwa kiwango kikubwa.

Amesema Simiyu inashika nafasi ya 64 duniani kwa uzalishaji wa pamba na ili ifike katika kumi bora ni lazima gharama za uzalishaji zikiwemo za nyenzo za uzalishaji zipungue na wakulima waelimishwe na kuhimizwa kutumia mbegu bora na mbolea pale inapobidi. 

"Kwa mujibu wa utafitituliofanya tuliona eneo lingine linaloweza kuwatoa zaidi ni kilimo cha pamba ya oganiki (pamba hai) ambayo inahitajika sana duniani na bei yake ni nzuri," alisema.

Dk Bamwenda kusisitiza kuwa kama watazalisha pamba hai inaweza kuwaletea pato kubwa," alisema.

Ameongeza kuwa pamoja na kilimo cha pamba mkoa wa Simiyu unayo fursa kubwa katika kilimo cha umwagiliaji kwa mazao ya mpunga, mboga mboga, matunda pamoja na kilimo cha mazao ya mikunde ambayo soko lake ni kubwa ndani na nje ya nchi.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, amesema pamba ya oganiki katika mkoa huo inalimwa katika wilaya ya Meatu na inauzwa kwa bei nzuri hivyo viongozi wajipange kupata masoko ya uhakika ya mazao mengine ya oganiki, hasa mboga mboga na matunda.

“Nisingehitaji kuwa kiongozi wa kuhamasisha wananchi kulima mazao ya oganiki wakati sijui watayauaza wapi, kama kiongozi wa mkoa na stakeholders wetu tunajipanga kuona tunapata masoko ili kujua wananchi wetu wanalima mazao yapi ya oganiki hasa katika maeneo yenye uhakika wa maji” alisema.

Mtaka amewataka viongozi wa mkoa wa Simiyu kubadili mtazamo wao katika kufikia azma ya kuubadilisha mkoa huo katika kufanyia kazi ushauri wa wataalam wakiwemo watafiti wa ESRF juu ya fursa mbalimbali za uwekezaji katika wilaya zote ili kutekeleza Sera ya Tanzania ya Viwanda katika kufikia Uchumi wa Kati.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Mkoa Mwanza ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Sahara Media Group Limited, Dk Anthony Diallo,  ameshauri Serikali ya Mkoa wa Simiyu kuwavutia kuwekeza katika maeneo mbalimbali ya mkoa huo kwa kutoweka urasimu usio wa lazima na kuishirikisha sekta binafsi katika utekezaji wa Sera ya Tanzania ya Viwanda.

Wakati huo huo Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu Ndg. Jumanne Sagini amewataka Wakurugenzi wote wa Halmashauri mkoani humo kupitia rasimu ya mwongozo wa uwekezaji wa ESRF ili kubaini maeneo ya kipaumbele yaliyopo katika fursa za uwekezaji zilizoanishwa kwenye mwongozo.

"Sasa hivi tuko katika maandalizi ya bajeti kaeni katika vikao vyenu vya mabaraza mpitie, angalieni namna ya kuyaingiza yale yatakayowezekana katika mipango ya bajeti za Halmashauri," alisema. 

Rasimu ya mwongozo wa uwekezaji Simiyu inalenga kuongeza pato la mwananchi wa Simiyu kutoka dola za Kimarekani 3600 hadi 12,000 kwa mwaka ifikapo mwaka 2050.

Mtafiti Mwandamizi wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na kijamii(ESRF), Dkt.Gratian Bamwenda akiwasilisha rasimu ya mwongozo wa uwekezaji katika mkoa wa Simiyu katika kikao maalumm kilichowahusisha viongozi wa mkoa huo na wadau wa maendeleo wa mkoa huo kutoka sekta binafsi.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka (kulia) akitoa hotuba ya ufunguzi katika kikao maalum cha kujadili rasimu ya mwongozo wa uwekezaji ya mkoa huo  kilichowahusisha viongozi wa mkoa huo na wadau wa maendeleo wa mkoa huo kutoka sekta binafsi.
Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu,Ndg.Jumanne Sagini akichangia hoja katika kikao maalum cha kujadili rasimu ya mwongozo wa uwekezaji ya mkoa huo  kilichowahusisha viongozi wa mkoa huo na wadau wa maendeleo wa mkoa huo kutoka sekta binafsi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka(wa tatu kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Mtafiti Mwandamizi wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na kijamii(ESRF), Dkt.Gratian Bamwenda(wa pili kulia), Mkurugenzi wa Sahara Media Group Limited, Dkt.Anthony Diallo(wa tatu kulia) na wadau wengine wa maendeleo wa mkoa huo
Baaadhi ya viongozi wa Mkoa wa Simiyu wakimsikiliza Mtafiti Mwandamizi wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na kijamii(ESRF), Dkt.Gratian Bamwenda (hayupo pichani) akiwasilisha rasimu ya mwongozo wa uwekezaji katika mkoa wa Simiyu katika kikao maalumm kilichowahusisha viongozi wa mkoa huo na wadau wa maendeleo wa mkoa huo kutoka sekta binafsi.
Bw.Gungu Silanga ambaye ni mfanyabiashara na mdau wa maendeleo mkoa wa Simiyu kutoka katika Sekta binafsi akichangia hoja katika kikao maalum cha kujadili rasimu ya mwongozo wa uwekezaji ya mkoa huo  kilichowahusisha viongozi wa mkoa huo na wadau wa maendeleo wa mkoa huo kutoka sekta binafsi.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa Mwanza ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Sahara Media Group Limited, Dkt.Anthony Diallo akiwasilisha hoja yake katika kikao maalum kilichowahusisha viongozi wa mkoa huo na wadau wa maendeleo wa mkoa huo kutoka sekta binafsi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa, Dkt.Fredrick Sagamiko akichangia hoja katika kikao maalum cha kujadili rasimu ya mwongozo wa uwekezaji ya mkoa huo  kilichowahusisha viongozi wa mkoa huo na wadau wa maendeleo wa mkoa huo kutoka sekta binafsi.

1 comment:

  1. Hello.
    Mimi ni Mr Rahel binafsi wakopeshaji mkopo ambao hutoa maisha wakati nafasi ya mkopo kwa watu binafsi, makampuni ya biashara, bima, nk Je, katika shida yoyote ya kifedha au katika haja ya mkopo wa kuwekeza au unahitaji mkopo kulipa bili yako kutafuta hakuna zaidi kama sisi ni hapa kufanya matatizo yako yote ya kifedha kitu cha zamani. Sisi kutoa kila aina ya mkopo katika dhehebu lolote fedha kwa kiwango cha 2% bila fee.I upfront wanataka kutumia kati hii kubwa ya kukufahamisha kwamba tuko tayari kukusaidia kwa aina yoyote ya mkopo kutatua kwamba tatizo.Kama yako ya kifedha ndiyo basi kupata nyuma sasa kupitia barua pepe (rahelcohranloan@gmail.com) kwa maelezo zaidi, wewe ni sana makala.

    ReplyDelete

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!