Saturday, February 11, 2017

VIONGOZI WA TAASISI ZA UMMA SIMIYU WAHIMIZWA KUSIMAMIA UTEKELEZAJI WA AGIZO LA MAKAMU WA RAISPI

Na Stella Kalinga

Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu,Ndg.Jumanne Sagini ametoa wito kwa viongozi na Wakuu wa Taasisi za Umma mkoani humo,  kusimamia utekelezaji wa agizo la Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Samia Suluhu Hassan la kufanya mazoezi ya viungo Jumamosi ya pili ya kila mwezi.

Sagini ametoa wito huo leo katika hotuba yake kwa watumishi wa umma,wanafunzi na wananchi walioshiriki mazoezi ya viungo na michezo mbalimbali katika uwanja wa Halmashauri ya Mji Bariadi ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Mhe.Makamu wa Rais.

Amesema Simiyu wamejipanga kutekeleza na akawataka watumishi wa Umma kuheshimu agizo hilo na kutekeleza kama ilivyoelekezwa, badala ya kuamua kushiriki au kutoshiriki. 

"...Niombe wote wanaowasimamia Watumishi wa Umma kuhimiza utaratibu huu wa mazoezi ambao ni agizo la Makamu wa Rais ambalo limeongozana na nyaraka za Ofisi ya Rais TAMISEMI na Wizara yenye dhamana na Elimu na Mafunzo ya Ufundi, lakini mara kadhaa hata Wizara ya Afya imekuwa ikisema,  Sisi kama Watumishi wa Umma hatuwezi kuchagua kutekeleza au tusitekeleze" alisema.

Amesema kila mkuu wa Taasisi,Idara,Sehemu anapaswa kuhakikisha watumishi walio chini yake wanashiriki mazoezi ya viungo mwezi ujao(Machi) kwa kuwa  kushindwa kutekeleza Maelekezo ya viongozi pasipo sababu za msingi ni utovu wa nidhamu, ambalo ni kosa kwa mujibu wa Sheria,kanuni na taratibu za Utumishi wa Umma.

Sagini ameongeza kuwa watumishi ambao hawatashiriki mazoezi ya viungo pasipo sababu za msingi wahojiwe na ikibidi wachukuliwe hatua stahiki kutokana na utoro huo.

Aidha, ametoa rai kuwa watumishi wa umma kujenga utamaduni wa kufanya mazoezi mara kwa mara ili kupambana na ongezeko la magonjwa yasiyoambukiza kama shinikizo la damu, kisukari na magonjwa ya moyo kwa kuwa muda mwingi wanakuwa maofisini.

Wakati huo huo Afisa Michezo wa Mkoa wa Simiyu,Ndg.Addo Komba amesema pamoja na kutekeleza agizo la Mhe.Makamu wa Rais, Mkoa una mpango wa kuwakutanisha watumishi wote wa Umma na Wanafunzi mara mbili kwa mwezi kufanya mazoezi ya viungo na michezo mbalimbali.

Sambamba na hilo Komba amesema katika kutambua na kuinua vipaji kwenye michezo, mkoa umepanga kuandaa ligi mwishoni mwa mwezi Februari, 2017 kwa ajili ya wanafunzi wa shule za Msingi na Sekondari kwa michezo mitatu ambayo ni mpira wa miguu, mpira wa pete na Riadha.


Utekelezaji wa Agizo la Makamu wa Rais Mhe.Samia Suluhu Hassan mkoani Simiyu, unafanyika chini ya kauli mbiu"SIMIYU MPYA, MICHEZO KWA AFYA, AMANI NA MAENDELEO."
Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Ndg.Jumanne Sagini (mwenye kofia nyeupe) akiwa na baadhi ya watumishi  katika mazoezi ya kutembea kwenye Uwanja wa Halamshauri ya Mji Bariadi, wakati wa utekelezaji wa agizo la Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Samia Suluhu Hassan la kufanya mazoezi ya Viungo.

 Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Ndg.Jumanne Sagini (wa pili kushoto) akishiriki mazoezi ya viungo na  baadhi ya watumishi wa Umma,wanafunzi na wananchi katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji Bariadi.
Baadhi ya Watumishi na wanafunzi wakifanya mazoezi ya viungo  katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji Bariadi leo kutekeleza agizo la Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Samia Suluhu Hassan.
Timu ya Sekretarieti ya Mkoa ikivuta kamba dhidi ya timu ya Halmashauri ya Mji Bariadi (haipo pichani) katika  Uwanja wa Halmashauri ya Mji Bariadi.
Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Ndg.Jumanne Sagini akizungumza na Viongozi na watumishi wa Umma, wanafunzi na wananchi walioshiriki mazoezi ya viuongo na michezo mbalimbali mjeni Bariadi ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Samia Suluhu Hassan.
Baadhi ya vijana wa Bariadi walioshiriki mchezo wa mbio za baiskeli leo mara baada ya viongozi, watumishi wa umma na wanafunzi kumaliza mazoezi ya viungo.
Baadhi ya watumishi wakishiriki mbio za mita 100 wakati wa utekelezaji wa agizo la Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Samia Suluhu Hassan la kufanya mazoezi ya Viungo na michezo mbalimbali mjini Bariadi.

1 comment:

  1. Hello.
    Mimi ni Mr Rahel binafsi wakopeshaji mkopo ambao hutoa maisha wakati nafasi ya mkopo kwa watu binafsi, makampuni ya biashara, bima, nk Je, katika shida yoyote ya kifedha au katika haja ya mkopo wa kuwekeza au unahitaji mkopo kulipa bili yako kutafuta hakuna zaidi kama sisi ni hapa kufanya matatizo yako yote ya kifedha kitu cha zamani. Sisi kutoa kila aina ya mkopo katika dhehebu lolote fedha kwa kiwango cha 2% bila fee.I upfront wanataka kutumia kati hii kubwa ya kukufahamisha kwamba tuko tayari kukusaidia kwa aina yoyote ya mkopo kutatua kwamba tatizo.Kama yako ya kifedha ndiyo basi kupata nyuma sasa kupitia barua pepe (rahelcohranloan@gmail.com) kwa maelezo zaidi, wewe ni sana makala.

    ReplyDelete

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!