Na Stella Kalinga
Watumishi wa idara ya mahakama wameaswa
kufanya kazi zao kwa weledi pasipo kutia unajisi wadau wengine wa mahakama
hususani jeshi la polisi.
Wito huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa
Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka katika maadhimisho ya siku ya sheria nchini
yaliyofanyika kimkoa katika viwanja vya Mahakama ya Wilaya Mjini Bariadi, chini
ya kauli mbiu"UMUHIMU WA UTOAJI WA HAKI KWA WAKATI KUWEZESHA UKUAJI WA
UCHUMI".
"Ukikaa Mtaani utasikia huyo hapo
alikuwa mwizi akakamatwa akapelekwa polisi akaachiwa, kumbe hawajui kuwa
kaachiwa mahakamani aliposhinda kesi lakini mdau wenu mmoja analaumiwa sana, ni
vizuri mkafanya kazi kwa weledi ili tafsiri ya wadau wenu kuwa kwenye mtazamo
hasi kwa jamii uondoke", alisema.
Mtaka amesema kumekuwa na malalamiko
mengi ya wananchi dhidi ya jeshi la polisi hata pale inapotokea mapungufu
katika utendaji wa watumishi wa mahakama, kwa kuwa baadhi yao hawajui
kuwa baada ya mtu kupelekwa polisi hupelekwa mahakamani.
Amesema watoa haki wa mahakama
wanatambulika kama wasomi (learned brothers and sisters) hivyo, wanapaswa
kujiridhisha katika utoaji wa maamuzi yao ili wasiifedheheshe taaluma yao na
mhimili wa mahakama kwa ujumla.
Aidha,ameipongeza idara ya mahakama na
wadau wengine wakiwemo viongozi wa dini,jeshi la polisi kwa mchango wao wa
kubadili taswira ya mkoa huo katika kushughulikia kesi za uhalifu
zikiwemo za kukatana mapanga kwa visasi,mauaji ya vikongwe na mauaji ya albino
na kufanya mkoa huu kusikika kwa mema.
Ameongeza kuwa mkoa wa Simiyu
umejitambulisha kama mkoa wa tofauti ktk masuala mbalimbali ya kiuchumi na
Mhe.Rais amewataka wengine kujifunza Simiyu, hivyo akawataka watumishi wa
mahakama kujituma na kutoa haki kwa wakati ili wengine waje kujifunza pia katika
utendaji wa Mahakama.
Kwa upande wake Mwakilishi wa Chama cha
Wanasheria Tanganyika(TLS) ambaye ni wakili, Polycarp Mtega amesema mambo
yanayochelewesha utoaji wa haki kwa wakati ni pamoja na ukosefu wa maadili kwa
baadhi ya watoa haki, upungufu wa watoa haki katika mahakama,watuhumiwa
kutofikishwa mahakamani toka gerezani kwa misingi ya kisiasa, ukosefu wa
mashahidi na kesi kuahirishwa pasipo sababu za msingi.
Naye Hakimu Mkazi Mfawidhi(M) Mhe. John
Nkwabi amesema Mahakama ya Tanzania imejipanga kuhakikisha wadau wote wanapata
haki zao kwa wakati ili wajikite katika shughuli za kiuchumi badala ya kupoteza
muda mwingi mahakamani, ambapo ameeleza kuwa jumla ya kesi 692 zimesikilizwa
kwa mwaka 2016, pamoja na upungufu wa mahakimu uliopo mkoani Simiyu.
Nkwabi ametoa wito kwa wananchi wenye
kesi kufika mahakamani kila wanapohitajika badala ya kusubiri kutumiwa hati za
kuitwa mahakamani.
Siku ya sheria nchini huadhimishwa kila
wiki ya kwanza ya mwezi Februari kila mwaka.
Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi (M)Mhe. John Nkwabi
akiwasilisha hotuba yake kwa Mkuu wa Mkoa huo , Mhe.Anthony Mtaka(hayupo
pichani) katika maadhimisho ya siku ya
sheria hapa nchini, yaliyofanyika kimkoa katika viwanja vya Mahakama ya Wilaya,
Mjini Bariadi
Wakili wa Serikali Mfawidhi wa Mkoa wa
Simiyu, Mhe.Yeriko Mlekano akiwasilisha hotuba yake kwa Mkuu wa Mkoa huo ,
Mhe.Anthony Mtaka(hayupo pichani) katika
maadhimisho ya siku ya sheria hapa
nchini, yaliyofanyika kimkoa katika viwanja vya Mahakama ya Wilaya, Mjini Bariadi.
Mwakilishi wa Chama cha Mawakili
Tanganyika (TLS) ,Mhe.Polycarp Mtega hotuba kwa niaba ya chama hicho mbele ya
Mkuu wa Mkoa huo , Mhe.Anthony Mtaka(hayupo pichani) katika maadhimisho ya siku
ya sheria hapa nchini, yaliyofanyika kimkoa katika viwanja vya Mahakama ya
Wilaya, Mjini Bariadi.
Baadhi ya Mahakimu wa Mahakama za Mwanzo
katika Mkoa wa Simiyu wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa huo , Mhe.Anthony Mtaka katika
maadhimisho ya siku ya sheria hapa nchini, yaliyofanyika kimkoa katika viwanja
vya Mahakama ya Wilaya, Mjini Bariadi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka
(wa pili kulia) na viongozi wengine wa
mahakama na Serikali wakifuatilia burudani kutoka kwa waimbaji wa kwaya ya AICT
Bariadi (hawapo pichani) katika maadhimisho ya siku ya sheria hapa nchini,
yaliyofanyika kimkoa katika viwanja vya
Mahakama ya Wilaya, Mjini Bariadi.
Baadhi ya viongozi wa dini walioshiriki
na kutoa sala maalum katika maadhimisho ya siku ya sheria hapa nchini,
yaliyofanyika kimkoa viwanja vya Mahakama ya Wilaya, Mjini Bariadi.
Mchungaji wa Kanisa la AICT Bariadi
akitoa sala maalum ya kuliombea Taifa, Viongozi na watendaji wa mihimili yote
katika maadhimisho ya siku ya sheria hapa nchini, yaliyofanyika viwanja vya
Mahakama ya Wilaya, Mjini Bariadi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka
Mtaka (wa pili kulia) na viongozi
wengine wa mahakama na Serikali wakiwa kwenye
picha ya pamoja katika maadhimisho ya siku ya sheria hapa nchini,
yaliyofanyika kimkoa viwanja vya Mahakama ya Wilaya, Mjini Bariadi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka
Mtaka (wa tatu kulia) na viongozi
wengine wa mahakama na Serikali wakiwa kwenye
picha ya pamoja katika maadhimisho ya siku ya sheria hapa nchini, yaliyofanyika
kimkoa viwanja vya Mahakama ya Wilaya, Mjini Bariadi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony
Mtaka Mtaka (wa tatu kulia) na viongozi
wengine wa mahakama na Serikali wakiwa kwenye
picha ya pamoja na watumishi wa Mahakama mbalimbali za mkoa huo katika
maadhimisho ya siku ya sheria hapa nchini, yaliyofanyika kimkoa viwanja vya
Mahakama ya Wilaya, Mjini Bariadi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka
Mtaka (wa tatu kulia) na viongozi
wengine wa mahakama na Serikali wakiwa kwenye
picha ya pamoja na Mahakimu wa Mahakama za Mwanzo za mkoa huo katika
maadhimisho ya siku ya sheria hapa nchini, yaliyofanyika kimkoa viwanja vya
Mahakama ya Wilaya, Mjini Bariadi.
Baadhi ya Watumishi wa Mahakama
mbalimbali katika Mkoa wa Simiyu wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa huo , Mhe.Anthony
Mtaka(hayupo pichani) katika maadhimisho ya siku ya sheria hapa nchini,
yaliyofanyika kimkoa katika viwanja vya Mahakama ya Wilaya, Mjini Bariadi.
Baadhi ya Watumishi wa Mahakama mbalimbali katika Mkoa wa Simiyu na wananchi wa Bariadi wakimsikiliza Mkuu wa
Mkoa huo , Mhe.Anthony Mtaka (hayupo pichani) katika maadhimisho ya siku ya
sheria hapa nchini, yaliyofanyika kimkoa katika viwanja vya Mahakama ya Wilaya,
Mjini Bariadi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe.Anthony Mtaka
akizungumza na viongozi wa Mahakama mkoa wa Simiyu kabla ya kuanza kwa sherehe
za maadhimisho ya siku ya sheria hapa nchini, yaliyofanyika kimkoa katika
viwanja vya Mahakama ya Wilaya, Mjini Bariadi.
Baadhi ya Watumishi wa Mahakama
mbalimbali katika Mkoa wa Simiyu na
viongozi wa Serikali wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa huo , Mhe.Anthony Mtaka (hayupo
pichani) katika maadhimisho ya siku ya sheria hapa nchini, yaliyofanyika kimkoa
katika viwanja vya Mahakama ya Wilaya, Mjini Bariadi.
Waimbaji wa Kwaya ya Kanisa la AICT Bariadi
wakitoa burudani ya wimbo maalum wa Siku ya Sheria nchini katika maadhimisho ya
siku hiyo, yaliyofanyika viwanja vya Mahakama ya Wilaya, Mjini Bariadi.
Sheikh wa Mkoa wa Simiyu,Mahamuod
Kalokola akitoa sala maalum ya kuliombea Taifa, Viongozi na watendaji wa
mihimili yote katika maadhimisho ya siku ya sheria hapa nchini, yaliyofanyika
viwanja vya Mahakama ya Wilaya, Mjini Bariadi.
0 comments:
Post a Comment