Tuesday, February 28, 2017

SIMIYU YAZINDUA RASMI MRADI WA KUPIMA NA KUTIBU WAATHIRIKA WA VVU

Na Stella Kalinga
Mkoa wa Simiyu leo umezindua mradi wa Kupima na Kutibu (Test and Treat) Wale watakaobainika kuwa na Virusi vya Ukimwi bila kujali wingi wa CD4.

Mradi huo ambao unaendeshwa na Shirika lisilo la Kiserikali la CUAMM umezinduliwa leo na Mkuu wa Wilaya ya Bariadi ambaye amemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka katika Ukumbi wa Kanisa Katoliki Mjini Bariadi na kushuhudiwa na viongozi wa serikali, viongozi wa dini, wataalam wa Afya ngazi ya Mkoa na wilaya na wadau wa Afya kutoka mashirika mbalimbali yasiyo ya Kiserikali.

Akisoma Hotuba ya Uzinduzi wa Mradi huo kwa Niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka, Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe.Festo Kiswaga ametoa wito kwa wananchi Mkoani humo  kujitokeza kwa wingi kupima na kujua hali zao, na kwa wale watakaobainika kuwa na maambukizi kuanza dawa mara moja kama wataalamu watakavyoelekeza.

Akitoa shukrani kwa Shirika la CUAMM amesema Serikali ya Mkoa iko tayari kuhamasisha na kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji katika idara ya Afya kwa kutoa ushirikiano kwa wawekezaji watakaofuata sheria, uwekezaji wenye tija  na kusisitiza kuwa wadau watakaotaka kushirikiana na Mkoa huo katika maeneo tofauti ilikiwemo eneo la mapambano dhidi ya UKIMWI kujadiliana kwanza ili kuzingatia vipaumbele vya Mkoa.

 Aidha, ameuagiza  uongozi wa idara ya afya Mkoa kuhakikisha mipango ya wadau wote wanaofanya kazi na Mkoa wa Simiyu  inaingizwa katika mipango ya Idara hiyo (Comprehensive Regional Health plan/CCHP) ili kujua mchango wa wadau hao na kutokubali mipango isiyo na tija kwa wananchi.

“Mtakumbuka kuwa jukumu la kudhibiti UKIMWI si la Serikali peke yake bali ni la jamii kwa ujumla wakiwepo wadau mbalimbali, tukishirikiana kwa pamoja tunaweza kufikia malengo ya sifuri tatu, yaani maambukizi mapya sifuri, unyanyapaa kwa waathirika wa VVU sifuri na Vifo vitokanavyo na UKIMWI sifuri” amesema.

Akitoa taarifa ya mradi wa Pima na Kutibu(Test and Treat) ambao unatekelezwa katika Mikoa ya Simiyu na Shinyanga, Mwakilishi wa Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Shinyanga, Liberatus Sangu, Paroko wa Parokia ya Bariadi Padre Kizito Nyanga Victor, amesema Mradi huu unatarajiwa kutoa ushauri nasaha na kupima  ,jumla ya wakazi 300,000 Simiyu  sambamba na utoaji wa matibabu ya watoto wadogo  20,000  ikiwa ni moja ya  mkakati wa kupunguza kasi ya   maambukizi ya  asilimia 3.1 kimkoa.

Kizito amesema kuwa  makusudio ya mradi huo ni kuweka vituo vya upimaji ,kuimarisha  maabara na vitendanishi ,kupima usugu wa VVU ,wingi wa VVU  katika mwili ambapo wao kama Kanisa kwa kushirikiana na mashirika mbalimbali wanaungana na Serikali katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa UKIMWI.

Kwa upande wake Professa Samuel Kaluvya kutoka Chuo Kikuu cha Tiba  Bugando, ambaye ndiye Mshauri Mkuu wa Mradi  huu amesema kuwa Malengo ya   Shirika la Ukimwi Dunia katika nchi zote asilimia 90 ya watu  wanaoishi naVVU waweze kutambulika kwa kupimwa na kuweza kuunganishwa na mfumo wa kutoa dawa na asilimia 90 ya watu  wanaotumia dawa za kufubaza VVU wahakikishe wanatumia dawa hizo  ipasavyo kwa maisha yao yote .

Mradi wa Pima na Kutibu (Test and Treat) Mkoani Simiyu utaanza kutekelezwa katika vituo viwili vya kutolea huduma za Afya  Mwamapalala (wilayani Itilima) na Songambele (wilayani Bariadi) na baadaye vituo nane na hatimaye utatekelezwa katika wilaya zote.
Mwakilishi wa mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka, Mhe.Festo Kiswaga akizindua alama inayotambulisha Mradi wa Pima na Kutibu VVU (Test and Treat) uliozinduliwa leo Mjini Bariadi.
Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka, Mhe.Festo Kiswaga akizungumza na viongozi, wataalam wa Afya na wadau mbalimbali wa afya kabla ya Uzinduzi wa Pima na Kutibu VVU (Test and Treat) Mjini Bariadi, ambao unatekelezwa na Shirika la CUAMM kwa kushirikiana na Serikali.

Mwakilishi wa Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Shinyanga, Liberatus Sangu, Paroko wa Parokia ya Bariadi Padre Kizito Nyanga Victor akizungumza na viongozi, wataalam wa Afya na wadau mbalimbali wa afya kabla ya Uzinduzi wa Mradi wa Pima na Kutibu VVU (Test and Treat) Mjini Bariadi, ambao unatekelezwa na Shirika la CUAMM kwa kushirikiana na Serikali.
Mwakilishi wa Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Shinyanga, Liberatus Sangu, Paroko wa Parokia ya Bariadi Padre Kizito Nyanga Victor akizungumza na viongozi, wataalam wa Afya na wadau mbalimbali wa afya kabla ya Uzinduzi wa Mradi wa Pima na Kutibu VVU (Test and Treat) Mjini Bariadi, ambao unatekelezwa na Shirika la CUAMM kwa kushirikiana na Serikali.
Meneja wa Mradi wa Pima na Kutibu VVU(Test and Treat)   Dkt.Arianna Bortolani kutoka Shirika la CUAMM  akitoa maelezo kwa Mkuu wa Wilaya ya Bariadi juu ya alama inayotumika kutambulisha mradi huo mara baada ya kufanya uzinduzi.
Baadhi ya Wajumbe wa Timu ya Usimamizi wa Idara ya Afya Mkoa (Regional Health Management Team RHMT) wakimsikiliza Mwakilishi wa mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka, Mhe.Festo Kiswaga kabla ya Uzinduzi wa Pima na Kutibu VVU (Test and Treat) Mjini Bariadi
Baadhi ya Wajumbe wa Timu ya Usimamizi wa Idara ya Afya Mkoa (Regional Health Management Team RHMT) wakimsikiliza Mwakilishi wa mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka, Mhe.Festo Kiswaga kabla ya Uzinduzi wa Pima na Kutibu VVU (Test and Treat) Mjini Bariadi.
Mratibu wa Mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI Mkoa wa Simiyu Dkt.Khamis Kulemba akiwasilisha mada ya hali ya maambukizi ya VVU kimkoa  kwa wadau malimbali wa afya katika kikao cha Pima na Kutibu VVU(Test and Treat).
Mganga Mkuu wa Mkoa, Dkt.Mageda Kihulya (wa pili kushoto) akizungumza katika kikao cha uzinduzi wa Mradi wa Pima na Kutibu VVU (Test and Treat) Mjini Bariadi,  (kushoto) Professa Samuel Kaluvya kutoka Chuo Kikuu cha Tiba  Bugando, ambaye ndiye Mshauri Mkuu wa Mradi  huo

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!