Saturday, November 30, 2019

RAS SIMIYU AZINDUA UTAFITI WA MATUMIZI YA SIMU KATIKA KUONGEZA ULIPAJI KODI ZA MAJENGO


Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini amezindua rasmi utafiti unaohusu matumizi ya simu za mikononi katika kuongeza ulipaji kodi za majengo nchini Tanzania, PIERI 20355 ambao utafanyika kuanzia Novemba 28, 2019 hadi 30 Juni 2020 katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi na Halmashauri ya Wilaya ya Busega.

Akizindua utafiti huo Novemba 28, 2019 mjini Bariadi Sagini amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri hizo kutoa ushirikiano unaotakiwa kwa watafiti ili kuwawezesha kufanya kazi yao kwa ufanisi na kupata matokeo sahihi.

 “ Wakurugenzi katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi na Busega, hakikisheni mnatoa ushirikiano katika utafiti kwani majengo yanayolipiwa kodi ya majengo yapo kwenye maeneo yenu na wamiliki wa majengo hayo pia wapo katika maeneo yenu,” alisema Sagini.
Sagini amewaahidi watafiti ushirikiano mkubwa ili utafiti ufanyike kama ilivyokusudiwa kwa lengo la kuongeza mapato yatokanayo na kodi ya majengo huku akiwaomba watafiti hao  kuendeleza kushirikiano na mkoa wa Simiyu katika tafiti mbalimbali kwa maendeleo ya Mkoa, wananchi na Taifa kwa ujumla.

Akiwasilisha taarifa ya utambulisho wa utafiti huo Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu Mzumbe na Mtafiti Mwandamizi wa Utafiti huu, Dkt.Francis Mwaijande, amesema Matokeo ya utafiti huu yatawezesha mamlaka za maamuzi ziweze kutoa maamuzi kwa kuzingatia taarifa zilizifanyiwa utafiti na hivyo kuwa na maamuzi ya kuongeza ufanisi kwenye ukusanyaji kodi.

Ameongeza kuwa matokeo ya utafiti huu yanatarajiwa kuongeza mapato yatokanayo na kodi za majengo kwa Serikali kwa kuhamasisha ulipaji kodi kwa kutumia simu zao za mkononi kwa njia ya meseji.
Utafiti unaohusu matumizi ya simu za mikononi katika kuongeza ulipaji kodi za majengo nchini Tanzania, PIERI 20355 unafanyika kwa lengo la kutafuta Ushahidi wa kitaaluma ili kuainisha kipi kinaweza kuongeza ulipaji kodi kwa kufuata sheria.
MWISHO
 Katibu Tawala wa Mkoa, Bw. Jumanne Sagini akizungumza na watafiti wanaofanya utafiti kuhusu unaohusu matumizi ya simu za mikononi katika kuongeza ulipaji kodi za majengo nchini Tanzania, PIERI 20355 katika mikoa ya Simiyu na Shinyanga wakati wa utambulisho wa utafiti mjini Bariadi  Novemba 28, 2019
 Watafiti wanaofanya utafiti kuhusu unaohusu matumizi ya simu za mikononi katika kuongeza ulipaji kodi za majengo nchini Tanzania, PIERI 20355 katika Mikoa ya Simiyu na Shinyanga, wakimsikiliza Katibu Tawala wa Mkoa, Bw. Jumanne Sagini wakati akizungumza nao katika  utambulisho wa utafiti mjini Bariadi  Novemba 28,  2019. 




Katibu Tawala wa Mkoa, Bw. Jumanne Sagini akizungumza na watafiti wanaofanya utafiti kuhusu unaohusu matumizi ya simu za mikononi katika kuongeza ulipaji kodi za majengo nchini Tanzania, PIERI 20355 wakati wa utambulisho wa utafiti mjini Bariadi  Novemba 28, 2019.

 
 Katibu Tawala wa Mkoa, Bw. Jumanne Sagini(katikati mbele)  akiwa katika picha ya pamoja na watafiti wanaofanya utafiti kuhusu matumizi ya simu za mikononi katika kuongeza ulipaji kodi za majengo nchini Tanzania, PIERI 20355 wakati wa utambulisho wa utafiti mjini Bariadi  Novemba 28, 2019.



 Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu Mzumbe na Mtafiti Mwandamizi wa Utafiti huu, Dkt.Francis Mwaijande akiwasilisha taarifa kwa Katibu Tawala wa Mkoa, Bw. Jumanne Sagini wakati wa utambulisho wa utafiti huo mjini Bariadi  Novemba 28, 2019. 


 


Katibu Tawala wa Mkoa, Bw. Jumanne Sagini akizungumza na watafiti wanaofanya utafiti kuhusu unaohusu matumizi ya simu za mikononi katika kuongeza ulipaji kodi za majengo nchini Tanzania, PIERI 20355 katika mikoa ya Simiyu na Shinyanga wakati wa utambulisho wa utafiti mjini Bariadi  Novemba 28, 2019.

 Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu Mzumbe na Mtafiti Mwandamizi wa Utafiti huu, Dkt.Francis Mwaijande akiwa katika picha ya pamoja na  Katibu Tawala wa Mkoa, Bw. Jumanne Sagini mara baada ya utambulisho wa utafiti kuhusu matumizi ya simu za mikononi katika kuongeza ulipaji kodi za majengo nchini Tanzania, PIERI 20355 mjini Bariadi  Novemba 28, 2019. 
 Katibu Tawala wa Mkoa, Bw. Jumanne Sagini akifurahia jambo na mmoja wa watafiti wanaofanya  utafiti kuhusu matumizi ya simu za mikononi katika kuongeza ulipaji kodi za majengo nchini Tanzania, PIERI 20355 katika mikoa ya Simiyu na Shinyanga, mara baada ya utambulisho wa utafiti huo mjini Bariadi  Novemba 28, 2019. 
Katibu Tawala wa Mkoa, Bw. Jumanne Sagini akiagana na mmoja wa watafiti wanaofanya  utafiti kuhusu matumizi ya simu za mikononi katika kuongeza ulipaji kodi za majengo nchini Tanzania, PIERI 20355 katika mikoa ya Simiyu na Shinyanga, mara baada ya utambulisho wa utafiti huo mjini Bariadi  Novemba 28, 2019.


0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!