Monday, March 9, 2020

BASHEAZINDUA MKAKATI WA MAPINDUZI YA KILIMO SIMIYU


Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe amezindua Mkakati wa Mapinduzi ya Kilimo cha Pamba wa miaka mitano (2019-2024) Mkoa wa Simiyu na kuwahimiza wakulima wote kufungua akaunti za benki kwa kuwa katika msimu ujao Wakulima watalipwa fedha zao kupitia mfumo wa benki ili kudhibiti matumizi mabaya ya fedha za wakulima yanayofanywa na baadhi ya viongozi wa Vyama vya Msingi vya Ushirika(AMCOS).

Aidha, Mhe. Bashe amesema Serikali imedhamiria kuwekeza katika kilimo na kujenga ushirika imara ikiwa ni pamoja na kufufua baadhi ya Viwanda vya kuchambua pamba(ginneries) vya wakulima kikiwepo kiwanda cha Luguru wilayani Itilima na viwanda vingine wiwili kutoka wilayani ya Maswa. 

Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe amezindua Mkakati wa Mapinduzi ya Kilimo cha Pamba wa miaka mitano (2019-2024) wa Mkoa wa Simiyu, uzinduzi huo ulifanyika katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari Kusekwa Mjini Bariadi, Machi 05, 2020.
Baadhi ya viongozi na watendaji wakifuatilia uzinduzi wa Mkakati wa Mapinduzi ya Kilimo cha Pamba wa miaka mitano (2019-2024) wa Mkoa wa Simiyu, uzinduzi huo ulifanyika katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari Kusekwa Mjini Bariadi, Machi 05, 2020.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!