Monday, March 9, 2020

WAZIRI WA AFYA AZITAKA HALMASHAURI KUTENGA ASILIMIA 10 YA VIKUNDI


Kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Kitaifa amabyo yatafanyika Bariadi Mkoani Simiyu, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe.Ummy Mwalimu amezitaka Halmashauri zote ambazo hazijatenga asilimia kumi ya mapato ya ndani ambayo ni fedha kwa ajili Wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kuhakikisha zinatenga fedha hizo ifikapo Machi 30, 2020 ili kuyawezesha makundi hayo kupata mikopo.

Mhe. Ummy Mwalimu ameyasema hayo Machi 05, 2020 wakati wa Uzinduzi wa Maonesho ya shughuli za wanawake wajasiriamali na jitihada za wadau katika kuwezesha wanawake kiuchumi na kuleta usawa wa kijinsia, katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe.Ummy Mwalimu akisaini katika ubao kwa kutumia chaki zinazotengenezwa Maswa mkoani Simiyu(Maswa Chalks) wakati wa alipotembelea banda la Maonesho la Halmashauri ya Wilaya ya Maswa katika maonesho  ya wanawake wajasiriamali, taasisi na vikundi mbalimbali Machi 05, 2020.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!