Monday, March 9, 2020

MAKAMU WA RAIS AAGIZA TTCL KUPELEKA MKONGO WA TAIFA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA SIMIYU


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan ameagiza Shirika la Mawasiliano nchini TTCL kufikisha mkongo wa Taifa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu ili vifaa vinavyotumika kutoa huduma vinavyowezeshwa na Mtandao wa Intanenti viweze kufanya kazi yake sawa.
Mhe. Makamu wa Rais ameyasema hayo wakati akifungua Jengo la Huduma kwa Wateja la TTCL Mkoa wa Simiyu Machi 07, 2020 mjini Bariadi , ambapo amewahimiza watendaji wa TTCL kutoa huduma bora na kwa ufanisi.
Aidha, Mhe. Makamu wa Rais ametoa wito kwa wananchi kutunza na kulinda miundombinu ya mawasiliano na watakaobainika kuhujumu miundombinu hiyo watashtakiwa kama wahujumu uchumi.



0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!