Wednesday, March 11, 2020

UNUNUZI MAZAO MCHANGANYIKO KUPITIA AMCOS UTAWAKOMBOA WAKULIMA: DC BARIADI



Mkuu wa wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga amesema  mfumo wa ununuzi wa mazao mchanganyiko kupitia vyama vya msingi vya Ushirika ( AMCOS) utakaoanza kutekelezwa mwaka huu 2020 umelenga kuwakomboa wakulima na  kuwawezesha kupata soko la uhakika  lenye ushindani pamoja na kuwaondoa wanunuzi wanyonyaji.

Kiswaga ameyasema  hayo jana katika kikao cha wadau wa mazao mchanganyiko kilichofanyika shule ya sekondari Kusekwa Memorial mjini Bariadi mkoani Simiyu, lengo lilikuwa kujadiliana namna ya kutekeleza maelekezo yaliyotolewa na  Naibu Waziri wa Kilimo Mhe.  Hussein Bashe kupitia tangazo alilolitoa Februari 14, 2020 kuhusu mfumo wa ununuzi wa choroko,dengu ,mbaazi , na soya kupitia Vyama vya ushirika vya msingi (AMCOS)  kwa mikoa yote inayolima mazao hayo kuanzia mwaka huu 2020.

Amesema wakulima wa mazao ya jamii ya mikunde pamoja na mbegu wamekuwa wakiuza kiholela pasipokuwa na mfumo rasmi hali iliyokuwa ikipelekea kuuza kwenye mizani ambayo haijahakikiwa huku wanunuzi wakijiamlia bei wanazozitaka.

"Serikali  imeamua kuja na mpango huo mzuri na lengo lake kubwa  ni kuwakomboa wakulima pamoja na kuwaondoa wanunuzi wanyonyaji kwani wamekuwa wakinunua mazao kwa wakulima kwa bei zao wenyewe jambo ambalo linapelekea kuwa na kilimo kisichokuwa na tija;kila mmoja anayehusika na mazao hayo atashirikishwa tutazifikia kata zetu zote kutoa elimu,"alisema Kiswaga.

Ameongeza kuwa mfumo huo wa kuuza kupitia AMCOS  utawezesha kila zao kuwa na bei halisi hatua ambayo itapunguza manung'uniko  ya wakulima juu ya unyonywaji huku akiwasisitiza pembejeo bora za kilimo ikiwemo  mbolea na mbegu bora ili  waweze kuwa na kilimo chenye tija.

Sambamba na hayo aliongeza kuwa changamoto kubwa ya wakulima ni uzalishaji ,masoko na namna ya upataji wa fedha baada ya kuuza huku akibainisha kuwa mkutano huo ni mwanzo mzuri wa kuhakikisha wanawasaidia wakulima kuwa wabunifu kwa kujua wanazalisha nini kwa kiasi gani na uchaguzi sahihi wa mbegu ,matumizi sahihi ya mbolea na viuadudu.

Kwa upande wake Naibu Mrajisi wa Vyama vya Ushirika upande wa uhamasishaji, Bw. Charles Malunde  amesema  kuwa mfumo unaoweza kuwanufaisha wakulima na wenye tija ni wa stakabidhi ghalani na kuwa nguvu ya ushirika inapatikana kwa jinsi wanaushirika wanavyoshirikiana.

Naye mkurugenzi wa uendeshaji soko la bidhaa (TMX), Bw. Augustino Mbulumi amesema kupitia mfumo huu wakulima watapata taarifa za soko kwa mazao yao na watapaswa kupata malipo ya mazao yao ndani ya saa 48 hivyo ni vema wakafungua akaunti benki ili kurahisisha mapokezi ya fedha zao.

Akizungumza kwa niaba ya wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa wa Simiyu, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Melkizedeck Humbe amesema ni vema kila mmoja akatimiza wajibu wake ili mfumo huu uweze kufanikiwa huku akibainisha kuwa mfumo huo utazisaidia Halmashauri kupata takwimu sahihi na namna ya ukusanyaji mapato.

Awali  akisoma tangazo la maelekezo ya serikali kuhusu  mfumo wa ununuzi wa choroko ,dengu, mbaazi, soya, na ufuta  mrajis msaidizi wa vyama vya ushirika mkoa wa Simiyu Ibrahim   Kadudu amesema tangazo hilo litaanza kutumika mwaka huu 2020 ambapo mazao hayo yatauzwa kupitia mfumo wa ushirika kwa mfumo wa minada ya vyama vikuu vya ushirika katika maeneo yao .

Aidha imedaiwa kuwa tume ya maendeleo ya ushirika kwa kushirikiana na soko la bidhaa (TMX) itaendesha minada kwa maeneo maalum kwa mazao hayo kupitia mfumo wa soko la bidhaa na taratibu zake zitabainishwa na TMX.

Wakizungumza kwa niaba ya wakulima baadhi viongozi wa vyama vya msingi vya ushirika Amcos walisema kuwa ni vema watendaji wa idara ya kilimo na ushirika wakatembelea kata zote kutoa elimu kwa wakulima ili mfumo huo ufahamike kwa wote.
MWISHO.

 Mkuu wa Wilaya ya Bariadi. Mhe. Festo Kiswaga akifungua kikao cha wadau wa mazao mchanganyiko kilichofanyika jana Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili namna ya kutekeleza maelekezo ya Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe kuhusu mfumo wa ununuzi wa choroko, dengu, mbaazi na soya  kupitia vyama vya ushirika vya msingi (AMCOS) kwa mikoa inayolima mazao hayo kuanzia mwaka huu 2020.



Baadhi ya wadau wa mazao mchanganyiko mkoani Simiyu, wakifuatilia kikao cha wadau hao kilichofanyika jana Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili namna ya kutekeleza maelekezo ya Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe kuhusu mfumo wa ununuzi wa choroko, dengu, mbaazi na soya kupitia vyama vya ushirika vya msingi (AMCOS) kwa mikoa inayolima mazao hayo kuanzia mwaka huu 2020.
Naibu Mrajisi wa Vyama vya Ushirika (Uhamasishaji), Bw. Charles Malunde akitoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali katika kikao cha wadau wa mazao mchanganyiko kilichofanyika jana Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili namna ya kutekeleza maelekezo ya Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe kuhusu mfumo wa ununuzi wa choroko, dengu, mbaazi na soya kupitia vyama vya ushirika vya msingi (AMCOS)kwa mikoa inayolima mazao hayo kuanzia mwaka huu .2020.

Mrajisi Msaidizi wa Vyama Ushirika Mkoa wa Simiyu, Bw. Ibrahim Kadudu akitoa ufafanuzi a masuala mbalimbali katika kikao cha wadau wa mazao mchanganyiko kilichofanyika jana Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili namna ya kutekeleza maelekezo ya Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe kuhusu mfumo wa ununuzi wa choroko, dengu, mbaazi na soya kupitia vyama vya ushirika vya msingi (AMCOS)kwa mikoa inayolima mazao hayo kuanzia mwaka huu 2020.
 Mkurugenzi wa Uendeshaji  Soko la Bidhaa(TMX), Bw. Augustino  Mbulumi akitoa mada katika kikao cha wadau wa mazao mchanganyiko kilichofanyika jana Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili namna ya kutekeleza maelekezo ya Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe kuhusu mfumo wa ununuzi wa choroko, dengu, mbaazi na soya kupitia vyama vya ushirika vya msingi (AMCOS) kwa mikoa inayolima mazao hayo kuanzia mwaka huu 2020.


 Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Bw. Melkizedeck Humbe akizungumza kwa niaba ya Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa wa Simiyu, katika kikao cha wadau wa mazao mchanganyiko kilichofanyika  jana Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili namna ya kutekeleza maelekezo ya Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe kuhusu mfumo wa ununuzi wa choroko, dengu, mbaazi na soya kupitia vyama vya ushirika vya msingi (AMCOS) kwa mikoa inayolima mazao hayo kuanzia mwaka huu 2020.


 Bw. James Petro  akichangia hoja katika kikao cha wadau wa mazao mchanganyiko kilichofanyika jana Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili namna ya kutekeleza maelekezo ya Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe kuhusu mfumo wa ununuzi wa choroko, dengu, mbaazi na soya kupitia vyama vya ushirika vya msingi (AMCOS) kwa mikoa inayolima mazao hayo kuanzia mwaka huu 2020.


 Bw. Daniel Masilimbi akichangia hoja katika kikao cha wadau wa mazao mchanganyiko kilichofanyika jana Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili namna ya kutekeleza maelekezo ya Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe kuhusu mfumo wa ununuzi wa choroko, dengu, mbaazi na soya kupitia vyama vya ushirika vya msingi (AMCOS) kwa mikoa inayolima mazao hayo kuanzia mwaka huu 2020.


 Baadhi ya viongozi wakifuatilia kikao cha wadau wa mazao mchanganyiko kilichofanyika jana Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili namna ya kutekeleza maelekezo ya Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe kuhusu mfumo wa ununuzi wa choroko, dengu, mbaazi na soya kupitia vyama vya ushirika vya msingi (AMCOS) kwa mikoa inayolima mazao hayo kuanzia mwaka huu 2020.


 Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini akifafanua baadhi ya masuala kwa wadau wa mazao mchangamyiko katika kikao cha wadau hao kilichofanyika jana Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili namna ya kutekeleza maelekezo ya Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe kuhusu mfumo wa ununuzi wa choroko, dengu, mbaazi na soya kupitia vyama vya ushirika vya msingi (AMCOS) kwa mikoa inayolima mazao hayo kuanzia mwaka huu 2020.


 Mtaalam wa masuala ya stakabadhi ghalani akitoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali katika kikao cha wadau wa mazao mchanganyiko kilichofanyika jana Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili namna ya kutekeleza maelekezo ya Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe kuhusu mfumo wa ununuzi wa choroko, dengu, mbaazi na soya kupitia vyama vya ushirika vya msingi (AMCOS) kwa mikoa inayolima mazao hayo kuanzia mwaka huu 2020.


Baadhi ya wadau wa mazao mchanganyiko mkoani Simiyu, wakifuatilia kikao cha wadau hao kilichofanyika jana Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili namna ya kutekeleza maelekezo ya Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe kuhusu mfumo wa ununuzi wa choroko, dengu, mbaazi na soya kupitia vyama vya ushirika vya msingi (AMCOS) kwa mikoa inayolima mazao hayo kuanzia mwaka huu 2020.



 Baadhi ya wadau wa mazao mchanganyiko mkoani Simiyu, wakifuatilia kikao cha wadau hao kilichofanyika jana Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili namna ya kutekeleza maelekezo ya Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe kuhusu mfumo wa ununuzi wa choroko, dengu, mbaazi na soya kupitia vyama vya ushirika vya msingi (AMCOS) kwa mikoa inayolima mazao hayo kuanzia mwaka huu 2020.

Baadhi ya wadau wa mazao mchanganyiko mkoani Simiyu, wakifuatilia kikao cha wadau hao kilichofanyika jana Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili namna ya kutekeleza maelekezo ya Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe kuhusu mfumo wa ununuzi wa choroko, dengu, mbaazi na soya kupitia vyama vya ushirika vya msingi (AMCOS) kwa mikoa inayolima mazao hayo kuanzia mwaka huu 2020.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!