Saturday, January 20, 2018

WAKUU WA IDARA ELIMU WAKATAKIWA KUSAIDIA JAMII KUONDOKANA NA MILA ZILIZOPITWA NA WAKATI

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka ametoa wito kwa Wakuu wa Idara za Elimu Msingi na Sekondari Halmashauri za Wilaya kuisadia jamii kuondokana na mila zilizopitwa na wakati.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu ametoa wito huo katika tathimini ya elimu iliyofanyika katika Shule ya Msingi Lukungu Wilayani Busega.
  
Ni kikao cha tathimini ya elimu Mkoa wa SIMIYU kilichowakutanisha  maafisa elimu na wakuu wa idara wa Halmashauri SITA chenye lengo la kufanya  taathimini ya kitaaluma na mikakati ya ufaulu wa mitihani ijayo ya kitaifa.

Akizungumza kwenye kikao hicho Mkoa wa Mkoa wa Simiyu, Antony Mtaka anasema tathimini ya matokeo ya elimu ilenge kuangalia changamoto zinazowakabili walimu sambamba na kuleta mabadiliko katika jamii.

Amesema jukumu lililombele yao ni kuhakikisha wanaibadilisha jamii ya Simiyu ili iondokane na mila potofu zilizopitwa na wakati ikiwemo ya kuwaadhibu walimu hadharani  kwa kuwatandika viboko almaarufu dagashida.

Kuhusu  Wilaya ya MEATU kufanya vibaya katika mitihani ya kitaifa ya darasa la saba na darasa la nne 2017 amewataka kuhakikisha wanabadilika ili kuuwezesha mkoa wa simiyu kuingia kumi bora kitaifa.

‘Meatu punguzeni kuwa mkia mnatuaibisha jitihidini muondoke huko alisema Mtaka.

Kwa upande wake Afisa Elimu wa Mkoa wa Simiyu, Julius Nestory  amesema pamoja na changamoto zilizopo katika sekta elimu lakini ufaulu umekuwa  ukiongezeka .

Aidha amesema wametekeleza agizo la mkuu wa mkoa la kulima zao la pamba katika shule za msingi na sekondari za serikali  ambapo jumla ya hekari  1,500  na hekari 230 za mahindi  ili kuwawezesha wanafunzi kupata chakula cha mchana .
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka akizungumza na Maafisa Elimu wa Halmashauri  za Mkoa huo (hawapo pichani) katika  tathimini ya elimu iliyofanyika katika Shule ya Msingi Lukungu Wilayani Busega.

Afisa Elimu Mkoa wa Simiyu,Mwl. Julius Nestory Maafisa Elimu wa Halmashauri  za Mkoa huo (hawapo pichani) katika  tathimini ya elimu iliyofanyika katika Shule ya Msingi Lukungu Wilayani Busega. 
Baadhi ya Maafisa Elimu wa Halmashauri za Mkoa wa Simiyu wakimsikilizaMkuu wa Mkoa huo, Mhe.Anthony Mtaka(hayupo pichani) katika tathmini ya Elimu iliyofanyika Wilayani Busega.
Baadhi ya Maafisa Elimu wa Halmashauri za Mkoa wa Simiyu wakimsikilizaMkuu wa Mkoa huo, Mhe.Anthony Mtaka(hayupo pichani) katika  tathmini ya Elimu iliyofanyika Wilayani Busega.


0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!