Wednesday, August 8, 2018

SIMIYU KINARA UTEKELEZAJI ILANI YA CCM, MSHIKAMANO VIONGOZI WA SERIKALI NA CHAMA

Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Bashiru Ally amesema Mkoa wa Simiyu ni mkoa wa kwanza ukifuatiwa na Mkoa wa Singida, Dodoma na Pwani  katika utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa mshikamano kati ya Serikali na Chama Tawala

Dkt. Bashiru amesema hayo wakati akitoa salamu za Chama Cha Mapinduzi  katika  Kilele  cha Maonesho ya Nane nane Kitaifa mwaka 2018 Mkoani Simiyu,  Uwanja wa Nyakabindi, Halmashauri ya Mji  wa Bariadi.


“ Simiyu ni Mkoa wa Kwanza kwa Tanzania Bara katika Utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi, matokeo tunayoyaona, haya yanayotufurahisha chanzo chake ni mshikamano baina ya Viongozi wa Chama na Serikali katika Mkoa” alisema Dkt. Bashiru.


Wakati huo Dkt. Bashiru ameitaja mikoa mitatu ikiongozwa na Simiyu ambayo inafanya vizuri katika Utekelezaji wa Ilani ya CCM kuwa ni pamoja na Singida, Dodoma na Pwani, huku akieleza kuwa katika mikoa hii viongozi na watendaji wa Chama wanafanya kazi kwa kushirikiana na Chama.


Aidha, ameitaja mikoa minne ambayo haifanyi vizuri kuwa ni Mara, Arusha, Mbeya na Dar es Salaam na akawataka viongozi wa Chama na Serikali katika mikoa hiyo  kujirebisha ili waweze kufanya kazi kwa kushirikiana.

Amesema Chama kimeumizwa sana na makundi na kinapata tabu pale ambapo viongozi wa Chama na Serikali hawana mtazamo mmoja hivyo amewataka viongozi wa mikoa ya Mara, Mbeya, Arusha na Dar es Salaam kushikamana na kuwa kitu kimoja ili waweze kuwatumikia wananchi ipasavyo.


Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema uhusiano kati ya Chama na Serikali  kwa mkoa huo kuanzia ngazi ya Kijiji na Tawi hadi mkoa uko vizuri na akimhakikishia Katibu Mkuu wa CCM kuwa mshikamano baina yao utaendelea kuimarishwa.

Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Bashiru Ally akizungumza na wananchi Bariadi katika Kilele cha Maonesho ya Nananane Kitaifa mwaka 2018 yaliyofanyika Uwanja wa Nyakabindi Bariadi 

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!