Tuesday, October 22, 2019

MAVUNDE AWATAKA VIONGOZI KUWATUMIA WATOA MSAADA WA KISHERIA KUTATUA MATATIZO YA WANANCHI

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Anthony Mavunde amezindua rasmi Maadhimisho ya wiki ya msaada wa kisheria ambayo yanafanyika Kitaifa
Mkoani Simiyu na kutoa wito kwa viongozi wa Serikali kuwatumia wasajili wasaidizi na watoa huduma za kisheria kutatua matatizo ya kisheria yanayowakabili wananchi.

Akizungumza na wananchi Oktoba 21, 2019  katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi  Mkoani Simyu Mavunde amesema matatizo ya kisheria yanashughulikiwa kisheria na siyo kisiasa hivyo ni vema wakawashirikisha na wakaambatana nao hata katika ziara zao ili waweze kutoa msaada wa kisheria kila unapohitajika.

“Yapo mambo mengi sana ambayo ni ya kisheria wananchi mmekuwa mkikimbilia kwa viongozi wa kisiasa, siasa ina sehemu yake inakoma inabaki sheria, wiki ya msaada wa kisheria ni fursa ya kipekee kuelewa namna ya kushughulikia matatizo yenu na mnaendelea kujifunza kuwa sheria inabaki kuwa sheria na utatuzi wake unakuwa katika mfumo uliowekwa kisheria,” alisema Mavunde.

Awali akitoa taarifa ya wiki ya msaada wa kisheria  Msajii wa Taasisi za watoa huduma za kisheria, B. Felistas Mushi amesema lengo la kuwepo wa huduma ya msaada wa kisheria ni kuhakikisha haki inapatikana kwa wananchi wasioweza kumudu gharama za wawakili”tunaamini kuwa baada ya maadhimisho haya kutakuwa na mtazamo chanya katika kutatua matatizo ya wananchi kisheria.”

Naye Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe Anthony Mtaka ametoa wito kwa viongozi wa Mkoa wa Simiyu wahakikishe katika ziara zao wanaambatana na wasajili wasaidizi na watoa huduma za kisheria walio katika maeneo yao ili waweze kutatua na kutoa ushauri wa namna ya kutatua matatizo yote kisheria.

Aidha, amewataka viongozi na wajumbe wa mabaraza ya ardhi ya vijiji, kata na wilaya kuhakikisha kuwa wanatumia vizuri mafunzo wanayopewa na wakayatafsiri kwa vitendo katika utatuzi wa matatizo ya watu kwa haki na kushirikiana na viongozi wa Serikali, taasisi na vyombo vyote vya maamuzi.

Katika hatua nyingine Mtaka ameshauri kuwa ingekuwa vema pia kama masuala ya kisheria yakajumuishwa katika baadhi ya masomo kama vile somo la Uraia ili kuendelea kujenga uelewa wa pamoja juu ya namna ya kukabiliana na matatizo yote ya kisheria.

Kwa upande wake Mkuugenzi Mtendaji wa TANLAP, Bi. Christina Ruhinda ameiomba Serikali na taasisi zake kushirikiana na watoa huduma za kisheria ili huduma hizo ziwe endelevu na matatizo ya wananchi yaweze kufanyiwa kazi kwa haki.

Mkurugenzi wa Miradi Shirika la Legal Services Facility, Bi. Scholastica Jullu amesema shirika ilo litaendelea kufadhili mashirika yanayotoa msaada wa kisheria kwa ajili ya maendeleo ya wananchi.

Maadhimisho ya Wiki ya Msaada wa kisheria mwaka 2019 yanaongozwa na Kauli Mbiu “Msaada wa Kisheria kwa Maendeleo Endelevu”, wakati yakiadhimishwa kitaifa mkoani SIMIYU yanapotarajiwa kuhitimishwa Oktoba 25, 2019 pia yanaadhimishwa katika mikoa ya Arusha, Dar es Salaam, Dodoma, Geita, Iringa, Kagera, Kigoma, Kilimanjaro,Mbeya, Mtwara, Mwanza, Njombe, Ruvuma, Shinyanga, Tabora na Tanga.
MWISHO
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Anthony Mavunde (wa pili kulia) akimsikiliza mmoja wa wananchi wa Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu aliyefika katika banda  la Wizara ya Mambo ya Ndani kupata msaada wa kisheria, katika uzinduzi wa Maadhimisho ya wiki ya Msaada wa kisheria Oktoba 21, 2019 yanayofanyika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu kuanzia Oktoba 21- Oktoba 25, 2019.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Anthony Mavunde (aliyesimama) akishuhudia wanasheria kutoka Kituo cha Haki za Binadamu wakitoa huduma ya msaada wa kisheria  kwa mmoja wa wananchi wa Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu, katika uzinduzi wa Maadhimisho ya wiki ya Msaada wa kisheria Oktoba 21, 2019 maadhimisho haya yanafanyika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu kuanzia Oktoba 21- Oktoba 25, 2019.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (kushoto) akimuongoza Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Anthony Mavunde na viongozi wengine kutembelea mabanda ya watoa huduma ya msaada wa kisheria, katika uzinduzi wa Maadhimisho ya wiki ya Msaada wa kisheria Oktoba 21, 2019 maadhimisho haya yanafanyika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu kuanzia Oktoba 21- Oktoba 25, 2019.



Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Anthony Mavunde (kulia) akimweleza jambo Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, katika uzinduzi wa Maadhimisho ya wiki ya msaada wa kisheria uliofanyika  Oktoba 21, 2019 maadhimisho haya yanafanyika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu kuanzia Oktoba 21- Oktoba 25, 2019.
Mtaalam kutoka Chama cha Wanasheria Tanganyika(TLS), akitoa  maelezo kwa Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Anthony Mavunde ( wa pili kulia) alipotembelea banda la Taasisi hiyo, katika uzinduzi wa Maadhimisho ya wiki ya msaada wa kisheria uliofanyika  Oktoba 21, 2019 maadhimisho haya yanafanyika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu kuanzia Oktoba 21- Oktoba 25, 2019.
Msajili wa Taasisi za Watoa huduma ya msaada wa kisheria nchini, Bi. Felistas Mushi akiwasilisha taarifa ya maadhimisho ya wiki ya msaada wa kisheria, katika uzinduzi wa maadhimisho hayo  Oktoba 21, 2019 maadhimisho haya yanafanyika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Mkoani Simiyu kuanzia Oktoba 21- Oktoba 25, 2019.
 Baadhi ya wananchi , Wenyeviti na Wajumbe wa mabaraza ya ardhi ya Vijiji na kata mkoani Simiyu, wakimsikiliza Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Anthony Mavunde (hayupo pichani ), katika uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya msaada wa kisheria Oktoba 21, 2019 maadhimisho haya yanafanyika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Mkoani Simiyu kuanzia Oktoba 21- Oktoba 25, 2019. 
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Anthony Mavunde , akizungumza na baadhi ya wananchi , Wenyeviti na Wajumbe wa mabaraza ya ardhi ya Vijiji na kata mkoani Simiyu,katika uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya msaada wa kisheria  Oktoba 21, 2019 maadhimisho haya yanafanyika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Mkoani Simiyu kuanzia Oktoba 21- Oktoba 25, 2019.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(wa kwanza mbele), Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Anthony Mavunde(mwenye suti mbele)  na viongozi wengine wakifurahia jambo mara  baada ya kutembelea mabanda ya watoa huduma ya msaada wa kisheria, katika uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya msaada wa kisheria Oktoba 21, 2019 maadhimisho haya yanafanyika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Mkoani Simiyu kuanzia Oktoba 21- Oktoba 25, 2019.
 Baadhi ya viongozi na watoa huduma ya msaada wa kisheria, wakifuatilia jambo katika uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya msaada wa kisheria Oktoba 21, 2019 maadhimisho haya yanafanyika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Mkoani Simiyu kuanzia Oktoba 21- Oktoba 25, 2019. 

 Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Anthony Mavunde (katikati walioketi),  akiwa katika picha ya pamoja baadhi ya viongozi  wa Mkoa na watoa huduma ya msaada wa kisheria mara baada ya uzinduzi wa Maonesho ya Wiki ya Msaada wa kisheria, Oktoba 21, 2019 maadhimisho haya yanafanyika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Mkoani Simiyu kuanzia Oktoba 21- Oktoba 25, 2019.


Wakili wa Serikali kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Bi. Lilian Kilembe akitoa maelezo mbele ya Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Anthony Mavunde, alipotembelea banda la wizara katika uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya msaada wa kisheria   Oktoba 21, 2019 maadhimisho haya yanafanyika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Mkoani Simiyu kuanzia Oktoba 21- Oktoba 25, 2019.



Baadhi ya wananchi wakipata huduma ya msaada wa kisheria katika mabanda mbalimbali ya watoa huduma hiyo, katika Maadhimisho ya wiki ya Msaada wa kisheria, maadhimisho haya yanafanyika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Mkoani Simiyu kuanzia Oktoba 21- Oktoba 25, 2019.

Mtaalam kutoka Chama cha Wanasheria Tanganyika(TLS), akitoa taarifa ya chama hicho katika uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya msaada wa kisheria   Oktoba 21, 2019 maadhimisho haya yanafanyika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Mkoani Simiyu kuanzia Oktoba 21- Oktoba 25, 2019.

 Mkurugenzi Mtendaji wa TANLAP, Bi. Christina Kamili Ruhimba akitoa taarifa ya taasisi hiyo katika uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya msaada wa kisheria   Oktoba 21, 2019 maadhimisho haya yanafanyika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Mkoani Simiyu kuanzia Oktoba 21- Oktoba 25, 2019.
 Mshauri wa Masuala ya Kijinsia Bungeni, Bi Stella Manda kutoka UN WOMEN akiwasilisha taarifa ya Shirika hilo kwa niaba ya Mkurugenzi, katika uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya msaada wa kisheria   Oktoba 21, 2019 maadhimisho haya yanafanyika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Mkoani Simiyu kuanzia Oktoba 21- Oktoba 25, 2019. 


Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Anthony Mavunde (katikati walioketi),  akiwa katika picha ya pamoja baadhi ya viongozi  wa Mkoa na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na usalama Mkoa wa Simiyu, mara baada ya uzinduzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Msaada wa kisheria, Oktoba 21, 2019 maadhimisho haya yanafanyika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Mkoani Simiyu kuanzia Oktoba 21- Oktoba 25, 2019.
Baadhi ya viongozi na watoa huduma ya msaada wa kisheria, wakifuatilia jambo katika uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya msaada wa kisheria Oktoba 21, 2019 maadhimisho haya yanafanyika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Mkoani Simiyu kuanzia Oktoba 21- Oktoba 25, 2019.
Baadhi ya viongozi na watoa huduma ya msaada wa kisheria, wakifuatilia jambo katika uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya msaada wa kisheria Oktoba 21, 2019 maadhimisho haya yanafanyika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Mkoani Simiyu kuanzia Oktoba 21- Oktoba 25, 2019.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (wa pili kushoto) akimuongoza Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Anthony Mavunde na viongozi wengine kutembelea mabanda ya watoa huduma ya msaada wa kisheria, katika uzinduzi wa Maadhimisho ya wiki ya Msaada wa kisheria Oktoba 21, 2019 maadhimisho haya yanafanyika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu kuanzia Oktoba 21- Oktoba 25, 2019.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!