Tuesday, October 8, 2019

NAIBU WAZIRI MWANJELWA AWATAKA WATUMISHI KUFANYA KAZI KWA UADILIFU NA UBUNIFU



Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Dkt Mary Mwanjelwa amewataka watumishi wa umma nchini kufanya kazi kwa weledi na uadilifu na kuwaasa wasikimbie maeneo yao kazi badala yake wawe chachu ya mabadiliko na utatuzi wa changamoto wanazokutana nazo katika maeneo yao

Dkt. Mwanjelwa ametoa rai hiyo wakati akizungumza na Viongozi, watumishi wa umma na viongozi wa vyama vya wafanyakazi Oktoba 04, 2019 Mjini Bariadi  mkoani Simiyu.

Dkt. Mwanjelwa amesema  watumishi wa umma wana maarifa hivyo wanapaswa kutumia maarifa hayo kukabiliana na changamoto zinzzowakabili badala ya kuhama maeneo ya kazi kwa kuwa Watanzania wanawahitaji kwa ajili ya kuwapa huduma wanazostahili.

“Utumishi wa umma ni fursa, utumishi wa umma ni fursa fanyeni kazi kwa weledi, uadilifu na ubunifu maana dunia inabadiilika na ndiyo maana tunasisitiza waajiri watoe mafunzo ya mara kwa mara ili watumishi waendane na mabadiliko ya sayansi na teknolojia,” alisema Dkt. Mwanjelwa.
Katika hatua nyingine Mwanjelwa anawaagiza waajiri kuwalipa kwa wakati fedha za mizigo wastaafu na utoaji wa mafunzo kwa waajiriwa wapya.

Kwa upande wake rais wa shirikisho la vyama vya wafanyakazi nchini TUCTA Tumaini Nyamhokya anaomba watumishi kupandishwa madaraja na wanapopandishwa wapate stahiki zao kwa wakati ikiwemo mishahara.

Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema mbali na upandishwaji madaraja lakini kumekuwepo na tatizo la kupandishwa mishahara ambapo alibainisha kuwa wapo maafisa elimu wanne ambao bado hawajabadilishiwa mishahara yao inayoendana na vyeo vipya hivyo akaomba Mhe. Naibu Waziri alifanyie kazi ili watumishi hao wapate haki yao.

Ziara ya naibu waziri ,ofisi ya Rais menejimenti ya utumishi wa umma na utawala bora Dkt. Mary Mwanjelwa Mkoani Simiyu imelenga   kuzungumza na watendaji na watumishi wa umma na kubadilishana uzoefu, kusikiliza kero na changamoto zinazowakabili .
 MWISHO
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Dkt Mary Mwanjelwa akizungumza na viongozi na watumishi wa Mkoa wa Simiyu katika kikao kilichofanyika Mjini Bariadi Oktoba 04, 2019 wakati akiwa kwenye ziara ya kikazi mkoani hapa.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Dkt Mary Mwanjelwa (kushoto) akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka wakati wa kikao chake na viongozi na watumishi wa mkoa wa Simiyu Oktoba 04, 2019 wakati akiwa kwenye ziara ya kikazi mkoani hapa.
Baadhi  ya viongozi na watumishi wa mkoa wa Simiyu wakiwa kwenye kikao na Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Dkt Mary Mwanjelwa Oktoba 04, 2019 wakati akiwa kwenye ziara ya kikazi mkoani hapa.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Dkt Mary Mwanjelwa (kushoto) akiteta jambo na Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini wakati wa kikao chake na viongozi na watumishi wa mkoa wa Simiyu kilichofanyika Mjini Bariadi Oktoba 04, 2019 wakati akiwa kwenye ziara ya kikazi mkoani hapa.
Rais wa Shirikisho la Wafanyakazi Tanzania(TUCTA), akichangia hoja katika kikao cha Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Dkt Mary Mwanjelwa na viongozi na watumishi wa Mkoa wa Simiyu kilichofanyika Mjini Bariadi Oktoba 04, 2019 wakati akiwa kwenye ziara ya kikazi mkoani hapa.


0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!