Thursday, December 22, 2016

RC SIMIYU AKUTANA NA VIONGOZI WA MKOA WA SHINYANGA KUJADILI MATUMIZI YA CHAKI ZA MASWA

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka (kushoto) akionesha pakti ya Chaki za Maswa kwa  Wakurugenzi wa Halmashauri na Maafisa Elimu wa Wilaya za Mkoa wa Shinyanga (hawapo pichani) walioshiriki kikao maalum cha kujadili matumizi ya Chaki hizo katika Mkoa wa Shinyanga
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka (katikati) akizungumza na Wakurugenzi wa Halmashauri na Maafisa Elimu wa Wilaya za Mkoa wa Shinyanga (hawapo pichani) wakati wa kikao maalum cha kujadili matumizi ya Chaki zinazotengenezwa Maswa (Simiyu) katika Mkoa wa Shinyanga,(kushoto) Mkuu wa Mkoa huo, Mhe.Zainab Telack na Katibu Tawala Mkoa, Ndg.Albert Msovela.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu, Mkoani Shinyanga Ndg.Augostine Matomora akichangia katika kikao maalum cha kujadili matumizi ya Chaki zinazotengenezwa wilayani Maswa (Simiyu) katika Mkoa wa Shinyanga.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Kahama , Mkoani Shinyanga Ndg. Anderson Msumba akichangia katika kikao maalum cha kujadili matumizi ya Chaki zinazotengenezwa wilayani Maswa (Simiyu) katika Mkoa wa Shinyanga.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka (kulia) akimkabidhi katoni ya Chaki za Maswa-Simiyu Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe.Zainab Telack(kushoto) baada ya kikao maalum cha kujadili matumizi ya Chaki hizo Mkoani humo.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka akimkabidhi katoni ya Chaki za Maswa-Simiyu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala, Mkoani Shinyanga Ndg.Simon Berege baada ya kikao maalum cha kujadili matumizi ya Chaki hizo Mkoani humo.
Viongozi wa Mkoa wa Simiyu na Shinyanga wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kikao maalum cha kujadili matumizi ya Chaki zinazotengenezwa wilayani Maswa (Simiyu) katika Mkoa wa Shinyanga.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe.Dkt. Titus Kamani akizungumza na Wakurugenzi wa Halmashauri na Maafisa Elimu wa Wilaya za Mkoa wa Shinyanga (hawapo pichani) wakati wa kikao maalum cha kujadili matumizi ya Chaki zinazotengenezwa Maswa mkoani Simiyu, katika Mkoa wa Shinyanga.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka akimkabidhi katoni ya Chaki za Maswa-Simiyu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga,baada ya kikao maalum cha kujadili matumizi ya Chaki hizo katika Mkoa wa Shinyanga.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala, Mkoani Shinyanga Ndg. Simon Berege akichangia katika kikao maalum cha kujadili matumizi ya Chaki zinazotengenezwa wilayani Maswa (Simiyu) katika Mkoa wa Shinyanga.
: Baadhi ya Wakurugenzi wa Halmashauri na Maafisa Elimu wa Wilaya za Mkoa wa Shinyanga wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu (hayupo pichani) katika kikao maalum cha kujadili matumizi ya Chaki zinazotengenezwa Maswa Mkoani Simiyu katika Mkoa wa Shinyanga.

   Na Stella Kalinga
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka amekutana na Uongozi wa Mkoa wa Shinyanga wakiogozwa na Mkuu wa Mkoa huo,Mhe.Zainab Telack, Katibu Tawala Mkoa na Wakurugenzi wa Halmashauri zote kujadili juu ya matumizi ya Chaki za Maswa mkoani Shinyanga.

Mtaka amesema Mkoa wake umefungua mlango wa biashara na ushirikiano katika bidhaa zinazozalishwa Mkoani Simiyu chini ya Kauli Mbiu ya “Wilaya Moja, Bidhaa Moja” kila wilaya itazalisha bidhaa moja itakayoitambulisha(branding); ambapo Wilaya ya Maswa imeanza kwa kutengeneza Chaki (MASWA CHALKS) na Wilaya ya Meatu inasindika maziwa ya ng’ombe (MEATU MILK).

Mtaka ameongeza kuwa Watanzania wanapaswa kuthamini na kupenda bidhaa zinazozalishwa hapa nchini na kubadili mtazamo wa kifikra kuwa bidhaa bora ni zile zinazozalishwa nje ya nchi, chini ya Kauli Mbiu “Buy Tanzania, Watanzania Tupende vya Kwetu”

Aidha, Mtaka amesema endapo viongozi hao wataridhia kutumia Chaki zinazotengenezwa na Vijana wa Maswa, wataokoa fedha nyingi zinazotolewa na Serikali kupitia Elimu bila malipo kwa kuwa zinauzwa kwa gharama nafuu ikilinganishwa na zile zinazotoka nje.

“Shule zetu zimekuwa zikinunua chaki kwa gharama kubwa kati ya shilingi 35,000 hadi 60,000 kwa katoni , lakini Vijana hawa wa Maswa watawauzia shilingi 25,000 kwa katoni.Chaki hizi zimethibitishwa na Shirika la Viwango nchini (TBS) na taratibu za TRA zimezingatiwa, vijana wanatoa risiti za EFD” alisema Mtaka.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe.Zainab Telack amesema ikiwa Wakurugenzi Halmashauri na Maafisa Elimu wa Wilaya za Mkoa huo wataridhia kutumia chaki za Maswa  katika shule zao uongozi wa Mkoa huo hautakuwa na kipingamizi.

Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa wa Simiyu walikubaliana kwa pamoja na kuunga mkono jitihada za Serikali na Vijana wa Wilaya ya Maswa kukubali kununua chaki za Maswa ili zitumike katika shule zao.

Kiwanda cha chaki kinachoendeshwa na Vijana wa Wilaya ya Maswa kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Maswa kinaweza kuzalisha takribani katoni 200 kwa siku na wakati matumizi halisi ya Mkoa wa Simiyu pekee ni katoni 700 kwa mwezi hivyo kuna ziada ya kuuza nje ya mkoa huo.


0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!