Thursday, December 29, 2016

MKUU WA MKOA WA SIMIYU ATOA TAMKO LA MKOA KUHUSU ELIMU MWAKA 2017



Na Stella Kalinga
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe.Anthony Mtaka ametoa tamko la Mapinduzi ya Elimu na mwelekeo wa Elimu mwaka 2017 kama kipaumbele cha kwanza kwa mkoa huo.

 Mkuu huyo wa Mkoa ametoa tamko hilo katika kikao maalum cha viongozi na wadau mbalimbali wa maendeleo wa Mkoa wa Simiyu kilichofanyika mjini Bariadi kwa lengo la kujadili dira ya maendeleo ya Mkoa huo.

Tamko hilo linamtaka kila Mwalimu Mkuu, Mtendaji wa Kijiji, Mtendaji wa Kata kuhakikisha ifikapo tarehe 05 Januari, 2017 awe amebandika majina yote ya watoto wanaoanza awali, darasa la kwanza na kidato cha kwanza tarehe 09 Januari, 2017.

Mtaka amesema tangu Serikali ya awamu ya tano ilipotangaza elimu bila malipo Mkoa wa Simiyu umepokea takribani kiasi cha shilingi 2,841,356,000/= kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari, hali iliyowapunguzia mzigo wazazi.

Mtaka amesema wajibu wa wazazi ni kuhakikisha kila mtoto anapelekwa shule tarehe 09 Januari, 2017 shule zitakapofunguliwa, ambapo amesema wazazi wote ambao hawatawapeleka watoto wao shule watachukuliwa hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kuwa vibarua wa kudumu watakaofanya usafi katika Taasisi za Umma.

“Wazazi wote ambao hawatawapeleka watoto shule wajiandae kuwa vibarua wa kudumu wa Serikali, hao ndiyo watakaosafisha masoko, vituo vya polisi, hospitali, vituo vya afya wengine watadeki hata madarasa na maeneo mengine ya Serikali. Nimeamua kuongea mbele yenu viongozi ili ujumbe huu muwafikishie wananchi, lakini pia nimekuwa nikizungumza na wananchi kila ninapofanya mikutano ya hadhara”, amesema Mtaka.

Pamoja na tamko hilo ameelekeza mambo muhimu yaliyoamuriwa kupitia vikao ya kisheria na kimaamuzi kama Vikao vya Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC),Kamati za Ushauri za Wilaya(DCC), Mabaraza ya Madiwani, Vikao vya Maendeleo ya kata (WDC) na mikutano ya vijiji yatekelezwe ambayo ni kukamilisha madawati Desemba 2016,kukamilisha ujenzi wa madarasa ifikapo Januari 30, 2017.

Maelekezo mengine ni pamoja viongozi wote kugawana na kusimamia madarasa yote ya mtihani (darasa la nne, darasa la saba, kidato cha pili, kidato cha nne na kidato cha sita), Shule zote kutumia chaki za Maswa, Madarasa ya Mitihani kufanya mazoezi ya kila siku asubuhi  saa 1:30 2:00 asubuhi, na kuwepo kwa makambi ya kielimu kwa shule, kata, Wilaya na Mkoa katika siku za mwisho za juma, mapumziko ya kati na mwisho wa mihula.

Naye Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu,Ndg.Jumanne Sagini amewataka Watendaji wote Serikali kuhakiksha kuwa wanafanyia kazi maelekezo yanayotolewa na viongozi wa mkoa huo ili kutekeleza dira ya maendeleo ya Mkoa kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu.

Wakati huo huo Mkuu wa Mkoa amesema katika utekelezaji wa Kauli mbiu ya Mkoa huo ya “Wilaya Moja Bidhaa Moja”baada ya wilaya ya Maswa kuzalisha chaki, Wilaya ya Meatu kusindika maziwa Mkoa umejipanga kuanzisha kilimo cha Umwagiliaji wilayani Busega mwaka 2017.

Mtaka amesema Katibu Tawala Mkoa ameunda kikosi kazi cha Wahandisi wa kilimo watakaosaidiana na watalaam wa Busega kuandaa mpango kazi wa utekelezaji wa kilimo cha Umwagiliaji hususani kilimo cha mpunga  kwa misimu miwili au zaidi ili wananchi wa Busega wanufaike kwa kuwa na maji ya Ziwa Victoria.

Pamoja na kilimo cha umwagiliaji Mtaka amewataka wananchi wa Mkoa wa Simiyu kulima mazao yanayokomaa muda mfupi na yanayostahimili ukame kama mtama, muhogo na viazi kutokana na taarifa kuwa mwaka 2017 hautakuwa na mvua za kutosha.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Lamadi wilayani Busega, Mhe.Laurent Bija amesema ili wilaya hiyo iweze kuzalisha chakula cha kutosha mkoa mzima na ziada kwa ajili ya kuuza kupitia mradi wa  kilimo cha umwagiliaji,  mkoa unapaswa kuwa  na mpango mkakati wa kudumu kwa lengo la kuufanya mradi huo kuwa endelevu.

Naye Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Simiyu,Mhe.Gimbi Masaba ametoa wito kwa viongozi wa mkoa huo kuwajibika ipasavyo katika shughuli za maendeleo ya wananchi bila kujali tofauti zao za kisiasa.


Kikao cha Viongozi na Wadau wa Maendeleo Mkoani Simiyu kimewahusisha Viongozi wa Serikali Ngazi ya Mkoa, Wilaya,Wabunge, Madiwani, Watendaji wa Sekretarieti ya Mkoa na Halmashauri, Viongozi wa CCM ngazi ya Mkoa na wilaya,viongozi wa Vyama vingine vya siasa na wadau wengine.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka (kushoto) akizungumza na viongozi na wadau wa maendeleo wa Mkoa huo (hawapo pichani) katika kikao cha kujadili dira ya maendeleo ya Mkoa mwaka 2017.
Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Ndg. Jumanne Sagini (wa pili kushoto) akizungumza na viongozi na wadau wa maendeleo wa Mkoa huo (hawapo pichani) katika kikao cha kujadili dira ya maendeleo ya Mkoa mwaka 2017.
Mkuu  wa Wilaya ya Bariadi, Mhe.Festo Kiswaga akizungumza na viongozi na wadau wa maendeleo wa Mkoa huo (hawapo pichani) katika kikao cha kujadili dira ya maendeleo ya Mkoa mwaka 2017.
Baadhi ya Viongozi na wadau wa Maendeleo wa Mkoa wa Simiyu wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa huo Mhe.Anthony Mtaka (hayupo pichani) katika kikao kilichowahusisha wadau hao ambacho kilifanyika jana katika ukumbi wa Bariadi Alliance mjini Bariadi.
Baadhi ya Viongozi na wadau wa Maendeleo wa Mkoa wa Simiyu wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa huo Mhe.Anthony Mtaka (hayupo pichani) katika kikao kilichowahusisha wadau hao ambacho kilifanyika jana katika ukumbi wa Bariadi Alliance mjini Bariadi. 
Katibu Mkuu wa CCM Mkoa wa Simiyu, Joyce Masunga (wa pili kulia) akizungumza katika kikao cha Viongozi na Wadau wa Maendeleo wa Mkoa huo kilichofanyika jana ukumbi wa Bariadi Alliance mjini Bariadi.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Mzumbe Bw. Paulo Faty akiwasilisha dhana ya Wilaya Moja,Bidhaa Moja (ODOP)  ambayo imeshaanza kutekelezwa Mkoani Simiyu mbele ya Viongozi na Wadau wa Maendeleo wa Mkoa huo katika kikao kilichofanyika jana ukumbi wa Bariadi Alliance mjini Bariadi.
Diwani wa Kata ya Lamadi, Mhe.Laurent Bija akichangia katika  kikao cha viongozi na wadau wa Maendeleo ya Mkoa wa Simiyu katika kikao kilichofanyika jana ukumbi wa Bariadi Alliance mjini Bariadi
Diwani wa Kata ya Zanzui na Katibu Mwenezi wa CCM Mkoa,Mhe.Jermia Shigala akichangia hoja katika  kikao cha viongozi na wadau wa Maendeleo ya Mkoa wa Simiyu katika kikao kilichofanyika jana ukumbi wa Bariadi Alliance mjini Bariadi.
Kutoka kushoto Mkuu wa Wilaya ya Itilima,Mhe. Benson Kilangi, Mkuu wa Wilaya ya Maswa,Mhe.Dkt.Seif Shekalaghe, Mkuu wa Wilaya ya Busega,Mhe.Tano Mwera na Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Mhe.Dkt.Joseph Chilongani wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka (hayupo pichani) wakati wa kikao cha Wadau wa Maendeleo ya Mkoa huo, kilichofanyika jana ukumbi wa Bariadi Alliance mjini Bariadi.
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Simiyu, Mhe.Gimbi Masaba akichangia hoja katika  kikao cha viongozi na wadau wa Maendeleo ya Mkoa wa Simiyu katika kikao kilichofanyika jana ukumbi wa Bariadi Alliance mjini Bariadi.
Diwani wa Kata ya Lingeka wilayani Meatu akichangia hoja katika  kikao cha viongozi na wadau wa Maendeleo ya Mkoa wa Simiyu katika kikao kilichofanyika jana ukumbi wa Bariadi Alliance mjini Bariadi.
Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe.Seif Shekalaghe akichangia hoja katika  kikao cha viongozi na wadau wa Maendeleo ya Mkoa wa Simiyu katika kikao kilichofanyika jana ukumbi wa Bariadi Alliance mjini Bariadi.

Baadhi ya Viongozi wa Mkoa wa Simiyu walioshiriki kikao cha viongozi na wadau wa Maendeleo ya Mkoa huo kilichofanyika jana ukumbi wa Bariadi Alliance mjini Bariadi.
Diwani wa Viti Maalum kutoka wilaya ya Maswa, Mhe.Mercy Emmanuel akichangia hoja katika  kikao cha viongozi na wadau wa Maendeleo ya Mkoa wa Simiyu katika kikao kilichofanyika jana ukumbi wa Bariadi Alliance mjini Bariadi.


Katibu Mkuu wa CCM Mkoa wa Simiyu, Joyce Masunga (wa pili kulia) akizungumza katika kikao cha Viongozi na Wadau wa Maendeleo wa Mkoa huo kilichofanyika jana ukumbi wa Bariadi Alliance mjini Bariadi.


0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!