Monday, May 29, 2017

RAS SAGINI AWATAKA WAKURUGENZI KUANDAA MIPANGO MIKAKATI YA HALMASHAURI

Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Ndg.Jumanne Sagini amewataka Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri Mkoani Humo kuandaa mipango mikakati katika Halmashauri zao.

Sagini ameyasema hayo wakati akifungua mafunzo ya siku tatu ya uandaaji wa Mipango mikakati ya Mamlaka za Serikali za Mitaa Mkoani humo yanayofanyika Lamadi wilayani Busega, chini ya Mpango wa Maboresho ya Usimamizi wa Fedha za Umma katika Mamlaka za Serikali za Mitaa(PFMRP).

Amesema wakurugenzi wote wahakikishe wanatumia rasilimali zilizopo katika maeneo yao kuhakikisha kuwa wanakamilisha uandaaji wa mipango mikakati hiyo.

“ Niwaombe Wakurugenzi Watendaji kuepuka visingizio vya kutokuwa na fedha kutekeleza jambo hili na badala yake mjipange kwa kutumia rasilimali tulizonazo” amesema.
Aidha, amesema Mpango Mkakati ni muhimu kwa kila Halmashari kwa kuwa unasaidia Halmashauri kufikia malengo ya kuanzishwa kwake na kuboresha utoaji huduma za kiuchumi na kijamii kwa wananchi.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, Ndg.Abdallah Malela  amesema mafunzo hayo yatawasaidia wao kama viongozi na watendaji wengine katika Halmashauri zao kutekeleza shughuli mbalimbali za maendeleo zikiwemo za uanzishwaji  na uendeshaji wa viwanda kimkakati.

Wakati huo huo pia Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kuendelea kutenga maeneo ili kuwezesha utekelezaji wa Sera ya Ujenzi wa Uchumi wa Viwanda Mkoani humo.

Mafunzo ya uandaaji wa Mipango mikakati ya Mamlaka za Serikali za Mitaa (Halmashauri) Mkoani yamewahusisha Wakurugenzi, Wataalam wa Idara ya Kilimo, Fedha, Mipango na Maendeleo ya Jamii kutoka Halmashauri zote sita (06) za mkoa huo (Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, Busega, Itilima, Maswa, Meatu na Halmashauri ya Mji Bariadi).

 
Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Ndg.Jumanne Sagini (wa pili kulia) akizungumza na washiriki wa mafunzo ya uandaaji wa mipango mikakati ya Halmashauri mkoani humo yaliyofanyika Lamadi wilayani Busega
Washiriki wa mafunzo ya uandaaji wa mipango mikakati ya Halmashauri mkoani Simiyu wakimsikiliza Katibu Tawala Mkoa huo, Ndg.Jumanne Sagini katika ufunguzi wa mafunzo hayo wilayani Busega
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, Ndg.Abdallah Malela akichangia jambo wakati wa mafunzo ya uandaaji wa mipango mikakati ya Halmashauri mkoani Simiyu yaliyofanyika Lamadi wilayani Busega
Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Mipango na Uratibu kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Simiyu, Ndg.Donatus Weginah (kushoto)akizungumza na washiriki wa mafunzo ya uandaaji wa mipango mikakati ya Halmashauri mkoani humo yaliyofanyika Lamadi wilayani Busega

Washiriki wa mafunzo ya uandaaji wa mipango mikakati ya Halmashauri mkoani Simiyu wakimsikiliza Katibu Tawala Mkoa huo, Ndg.Jumanne Sagini katika ufunguzi wa mafunzo hayo wilayani Busega

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!