Thursday, May 4, 2017

RAS SIMIYU ASAINI MIKATABA YA UJENZI WA MIRADI NANE YENYE THAMANI YA SHILINGI 3,219,429,243.

Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu,Ndg.Jumanne Sagini leo amesaini mikataba ya ujenzi wa miradi nane itakayojengwa na Wakala wa Majengo (TBA) kupitia Kikosi chake cha Ujenzi  (Building Brigade) katika makao Makuu ya Mkoa Mjini Bariadi, Wilaya ya Busega na Itilima.

Mikataba iliyosainiwa ni pamoja na Mradi wa Ujenzi wa Jengo la Wagonjwa wa Nje la Hospitali ya Mkoa(OPD) litakalojengwa  kwa gharama ya shilingi 1,191,721,678.00, Nyumba ya Mkuu wa Mkoa (shilingi 273,390,082.99), Nyumba ya Katibu Tawala Mkoa(shilingi 266,269,130.29), Nyumba ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima (shilingi 141,196,144.51) na Nyumba ya Mkuu wa Wilaya ya Busega (shilingi 238,061,242.06).

Mikataba mingine ni ya mradi wa ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega litakalojengwa kwa shilingi  1, 390,030,338.57, ukamilishaji wa Ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa kwa shilingi 128,247,283.79 pamoja na Ujenzi wa Nyumba 10 za Makatibu Tawala Wasaidizi wa Sekretarieti ya Mkoa kwa gharama ya shilingi 841,540,642.50, ambapo kwa sasa mradi huu utaanza na ujenzi wa nyumba tatu.

Akizungumza na wataalam kutoka Wakala wa Majengo(TBA) na Makao Makuu na Mkoa wa Simiyu kabla ya kusaini mikataba hiyo, Sagini amewataka wataalam hao kuhakikisha majengo yote yanajengwa kwa ubora na kwa muda uliowekwa katika mikataba hiyo.

Meneja wa Kikosi cha Ujenzi cha TBA, Humphrey Killo amesema kikosi hicho kitajenga majengo yote kwa ubora unaotakiwa na ndani ya muda ulipoangwa kwa kuwa kushindwa kuzingatia muda kutawaongezea gharama ambazo hazipo kwenye mikataba.

Aidha, Killo amesema katika gharama za ujenzi wa majengo hayo watazingatia bajeti waliyokubaliana na mteja wao ambaye ni Katibu Tawala Mkoa na kutakuwa na timu itakayofuatilia matumizi ya fedha katika kila kazi itakayofanyika kwa kuwa wana viwango vya chini ikilinganishwa na wakandarasi wengine.


Ukamilishaji wa ujenzi wa miradi hii unatofautiana kulingana na mikataba iliyowekwa kuanzia leo tarehe 04/05/2017 ambapo Ujenzi wa Jengo la Wagonjwa wa Nje la Hospitali ya Mkoa(OPD) litajengwa katika kipindi cha miezi sita(06), Nyumba ya Mkuu wa Mkoa miezi sita(06), Nyumba ya Katibu Tawala Mkoa miezi sita(06), Nyumba ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima miezi minne(04), Nyumba ya Mkuu wa Wilaya ya Busega miezi mitano (05), Jengo la Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega miezi sita(06) ,ukamilishaji wa Ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa miezi miwili (02) na Nyumba 10 za Makatibu Tawala Wasaidizi wa Sekretarieti ya Mkoa miezi sita (06).
Katibu Tawala Mkoa Simiyu, Ndg.Jumanne Sagini akisaini moja ya mikataba ya ujenzi wa miradi nane (08) ya Ujenzi inayotarajiwa kutekelezwa na Wakala wa Majengo (TBA) Mkoani Simiyu.

Kaimu Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Miundombinu, Mhandisi.Deusdedit Mshuga akichangia jambo wakati wa zoezi la kusaini mikataba ya ujenzi wa miradi nane (08) ya Ujenzi inayotarajiwa kutekelezwa na Wakala wa Majengo (TBA) Mkoani Simiyu.
Baadhi ya Watalaam wa TBA na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wakimsikiliza Katibu Tawala Mkoa Simiyu, Ndg.Jumanne Sagini kabla ya kusaini mikataba ya ujenzi wa miradi nane inayotarajiwa kutekelezwa na TBA Mkoani Simiyu.
Meneja wa Kikosi cha Ujenzi cha TBA, Humphrey Killo akisisitiza jambo wakati wa zoezi la kusaini mikataba ya ujenzi wa miradi nane (08) inayotarajiwa kutekelezwa na Wakala wa Majengo (TBA) Mkoani Simiyu.
Katibu Tawala Mkoa Simiyu, Ndg.Jumanne Sagini akizungumza na Watalaam wa TBA wakati wa zoezi la kusaini mikataba ya  miradi nane ya ujenzi inayotarajiwa kutekelezwa na Wakala wa Majengo (TBA) Mkoani Simiyu.
Baadhi ya Watalaam wa TBA wakimsikiliza Katibu Tawala Mkoa Simiyu, Ndg.Jumanne Sagini kabla ya kusaini mikataba ya ujenzi wa miradi nane inayotarajiwa kutekelezwa na TBA Mkoani Simiyu.
Kaimu Meneja wa TBA Mkoa wa Simiyu,  Mhandisi Yohana Mashausi akisisitiza jambo wakati wa zoezi la kusaini mikataba ya ujenzi wa miradi nane (08) inayotarajiwa kutekelezwa na Wakala wa Majengo (TBA) Mkoani Simiyu.
Katibu Tawala Mkoa Simiyu, Ndg.Jumanne Sagini akiwaonesha kitu Watalaam wa TBA na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu katika ramani ya eneo la ujenzi wa Ofisi ya Taasisi za Umma na Makzi ya Viongozi lililopo Nyaumata (BARIADI) baada ya zoezi la kusaini mikataba ya  miradi nane ya ujenzi inayotarajiwa kutekelezwa na Wakala wa Majengo (TBA) Mkoani Simiyu.
Mwanasheria Mwanahamisi Kawega(kulia)akisaini moja ya mikataba ya ujenzi wa miradi nane (08) ya Ujenzi inayotarajiwa kutekelezwa na Wakala wa Majengo (TBA) Mkoani Simiyu.


0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!