Saturday, August 5, 2017

WANANCHI WAHIMIZWA KWENDA KUSHUHUDIA MASHINDANO YA BAISKELI NA NGOMA ZA ASILI AGOSTI 06

Wananchi Mkoani Simiyu wamehimizwa kwenda kushuhudia mashindano ya Baiskeli na Ngoma za Asili yatakayofanyika kesho Jumapili katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi.

Akizungumza na Waandishi wa Habari Mratibu wa Mashindano hayo yanayotambulika kama Simiyu Jambo Festival ambayo yanadhaminiwa na Kampuni ya Jambo Food Products, Ndg.Kulwa Mtebe amesema washiriki wa mbio za baiskeli kutoka mikoa mbalimbali wameshawasili Mjini Bariadi na wamejiandaa vizuri kwa ajili mashindano.

Aidha, amesema Mgeni Rasmi katika tukio hilo(Simiyu Jambo Festival) la Kihistoria Mkoani Simiyu ambaye ni Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt.Tulia Ackson ameshawasili Mkoani kwa ajili ya mashindano hayo.

Mkuu wa Usalama Barabarani Mkoa wa Simiyu, Edson Mwakihaba amesema Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani limejipanga kikamilifu kuhakikisha kwamba watumiaji wa barabara wanazingatia sheria za usalama barabarani na askari watakuwepo katika vituo vyote ambavyo washiriki wa mbio za baiskeli watapita.

Rais wa Chama cha Baiskeli Taifa Godfrey Mhagama amesema Chama hicho kupitia kamati yake ya Ufundi kitakahikisha kanuni na taratibu za mchezo wa mbio za baiskeli zinasimamiwa na kufuatwa katika mashindano hayo.

Mhagama ameongeza kuwa Wachezaji wahakikishe wanacheza katika viwango vinavyotakiwa kwa kuwa vigezo vyote vitavyozingatiwa ikiwa ni pamoja na kasi ya mchezaji na muda anaoutumia katika kukamilisha mbio kwa umbali uliopangwa, ambayo pia itakuwa ni njia ya kupata wachezaji wanaoweza kuwakilisha Taifa katika Mashindano ya Olimpiki.

Kwa upande wake Meneja Masoko wa Kampuni ya Jambo Food Products Anthony Paul amewahakikishia washiriki kuwa zawadi zote zilizopangwa kwa washindi katika makundi yote matatu (wanaume, wanawake, walemavu) ziko tayari ambayo ni pikipiki itakayotolewa kwa mshindi wa kwanza(wanaume) na fedha taslimu zaidi ya shilingi Milioni nane zitakazotolewa kwa washindi wengine.

Naye Emmanuel Mollel mshiriki wa mashindano ya mbio za Baiskeli kutoka mkoa wa Arusha amesema washiri kutoka katika mkoa huo wamejipanga kikamilifu na kiushindani kuhakikisha wanapata ushindi.

Tatu Malulu mshiriki wa mbio za Kilometa 80 kutoka katika Mkoa wa Mwanza amesema amekuwa akifanya mazoezi siku zote ambayo yamemuimarisha hivyo akathibitisha kuwa kutokana na maandalizi hayo anatarajia ushindi na ametoa wito kwa Wachezaji kujenga utamaduni wa kufanya mazoezi siku zote maana ndio siri ya kufanikiwa kwao.

Zaidi ya washiriki 160 kutoka katika mikoa ya Simiyu, Shinyanga, Mwanza, Geita na Arusha wanatarajia kushiriki mashindano hayo ambayo yatagawanyika katika makundi matatu; wanaume Kilometa 200, wanawake Kilometa 80 na Watu wenye Uemavu Kilometa 05.
Baadhi ya Washiriki wa mashindano ya baiskeli wanawake kutoka wakisikiliza maswali kutoka kwa waandishi wa habari hawapo pichani wakati wa mahojiano maalum juu ya maandalizi ya mashindano hayo yanayotarajiwa kufanyika Jumapili ya tarehe 06/08/2017 Mjini Bariadi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka(mwenye pikipiki) akiwa na pikipiki itakayotolewa kwa mshindi wa kwanza kwa Kilometa 200 pamoja na baadhi ya washiriki wa mashindano ya mbio za baiskeli yatakayofanyika Jumapili ya tarehe 06/08/2017 Mjini Bariadi.
Meneja Masoko wa Kampuni ya Jambo, Anthony Paul akiwaonesha waandishi wa habari (hawapo pichani) pikipiki aina ya SHINERAY itakayotolewa na Kampuni hiyo ambayo ni Wadhamni wa Mashindano ya Baiskeli kwa mshindi wa kwanza wanaume yatakayofanyika  Jumapili ya tarehe 06/08/2017, Mjini Bariadi.
Rais wa Chama cha Baiskeli Taifa Godfrey Mhagama ( wa tatu kulia) akizungumza na viongozi wa Chama hicho Mkoa wa Simiyu kuhusu masuala mbalimbali ya maandalizi ya mashindano ya baiskeli yatakayofanyika Jumapili ya tarehe 06/08/2017 Mjini Bariadi.
Rais wa Chama cha Baiskeli Taifa Godfrey Mhagama akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa mahojiano maalum juu ya maandalizi ya mashindano ya Mbio za Baiskeli yatakayofanyika Jumapili ya tarehe 06/08/2017 Mjini Bariadi.
Mratibu wa Mashindano ya Baiskeli na ngoma za Asili yanayotambulika kama Simiyu Jambo Festival, Kulwa Mtebe akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa mahojiano maalum juu ya maandalizi ya mashindano ya Mbio za Baiskeli yatakayofanyika Jumapili ya tarehe 06/08/2017 Mjini Bariadi.
Mkuu wa  Usalama Barabarani Mkoa wa Simiyu, Edson Mwakihaba akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa mahojiano maalum juu ya hali ya usalama wa barabarani wakati wa mashindano ya Mbio za Baiskeli yatakayofanyika Jumapili ya tarehe 06/08/2017 Mjini Bariadi.
Mshiriki wa Mashindano ya Baiskeli kutoka Mkoa wa Arusha, Emmanuel Mollel akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa mahojiano maalum juu ya maandalizi ya mashindano ya Mbio za Baiskeli yatakayofanyika Jumapili ya tarehe 06/08/2017 Mjini Bariadi.




0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!