Wednesday, August 30, 2017

WITO UMETOLEWA KWA WANANCHI KUCHANGIA UJENZI VYUMBA VYA MADARASA

Wananchi  wa Kata ya Nkololo katika Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi wametakiwa kutambua wajibu wao katika kuchangia ujenzi wa Vyumba vya madarasa ili kupunguza tatizo la upungufu wa vyumba vya madarasa katika shule za msingi na sekondari.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe.Anthony Mtaka wakati alipokuwa akijibu kero mbalimbali za wananchi katika Mkutano wa Hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Nkololo Kata ya Nkololo Wilayani Bariadi.

Mtaka amesema ni vema wananchi wakahamasika kuchangia katika ujenzi wa vyumba vya madarasa kama wanavyochangia katika masuala mengine ili watoto wao wawe na mazingira mazuri ya kusomea.

“Kujenga vyumba vya madarasa siyo wajibu wa walimu wetu ni wajibu wenu wenu wazazi, ni lazima wananchi wa Nkololo mjenge vyumba vya madarasa kama mnavyojitoa katika mambo mengine, najua hamuwezi kushindwa kutoa angalau mfuko mmoja wa saruji kila kaya; Nkololo itajengwa na wana Nkololo wenyewe” amesema Mtaka.

Aidha, Mtaka ametoa wito kwa wananchi hao kuzingatia suala la uzazi wa mpango kwa kuwa ongezeko kubwa la watoto ndio linalopelekea idadi kubwa ya wanafunzi ikilinganishwa na vyumba vya madarasa.

“Mhe.Diwani nikuombe tengeneza utaratibu hapa na watu wako, Nkololo ni moja ya centre(kituo) kubwa wachangie, wala wasiseme tumechangia sana ni lazima wachangie; na kama hatutajirekebisha kwenye kuzaana, tutachanga, tutachanga, tutachanga” amesema Mtaka.

Naye Afisa Elimu wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, Doreen Rutahanamilwa amesema, Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali inaendelea na ujenzi wa miundombinu ya elimu vikiwemo vyumba vya madarasa na matundu ya vyoo, hivyo wananchi wanao wajibu kuunga mkono jitihada hizo ili kuleta maendeleo katika sekta ya elimu.

Kuhusu kero ya uharibifu wa mazao unaofanywa na wanyamapori hususani Tembo, ambayo ilitolewa na Luja Masala Mkazi wa Kijiji cha Bubale, Mkuu huyo wa Mkoa amesema, Serikali kupitia watalaam wake wa Wanyamapori watakabiliana na tatizo hilo, hivyo akawataka wananchi wasiache kulima na wazingatie ushauri wanaopewa na watalaam hao.

Akitoa ufafanuzi wa kitaalam juu ya kero hiyo, Mkuu wa Idara ya Ardhi na Maliasili, Ndg.Mazengo Sabaya amesema, Halmashauri imekuwa ikipeleka askari wa Wanyamapori katika maeneo yanayovamiwa na tembo na akawataka wananchi kuendelea kufuata ushauri wa kutumia uzio wa pilipili katika mashamba yao ili kuwazuia tembo hao.

Katika suala la upatikanaji wa mbegu bora, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe.Anthony Mtaka Serikali kupitia kwa wakala wa mbegu ina mpango wa kuhakikisha wakulima wanapata mbegu bora katika bei wanayoweza kuimudu.

Katika hatua nyingine Mtaka ametoa maelekezo kwa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi kuhakikisha inaweka mipango ya ujenzi wa stendi, soko na barabara katika kituo cha Nkololo ambacho ni moja vituo vikubwa vya kibiashara wilayani humo.

Mkuu wa Mkoa ameanza ziara katika Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi katika Kata ya Nkololo na baadaye atafanya ziara katika kata za Dutwa na Ngulyati ambapo atafanya mikutano ya hadhara na kusikiliza kero mbalimbali za wananchi. 
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka akizungumza na wananchi wa Kata ya Nkololo wilayani Bariadi (hawapo pichani) katika Mkutano wa Hadhara, wakati wa ziara yake aliyofanya kwa lengo la kusikiliza kero mbalimbali za wananchi.
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe.Festo Kiswaga akizungumza na wananchi wa Kata ya Nkololo (hawapo pichani) wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka wilayani humo aliyofanya kwa lengo la kusikiliza kero mbalimbali za wananchi
Luja Masala Mkazi wa Kijiji cha Bubale Kata ya Nkololo akiwasilisha kero yake kwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka (hayupo pichani) wakati wa ziara  aliyofanya kwa lengo la kusikiliza kero mbalimbali za wananchi.
Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Simiyu na viongozi wengine wa Mkoa na Wilaya ya Bariadi wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka (hayupo pichani) wakati wa ziara  aliyofanya katika Kata ya Nkololo wilayani Bariadi, kwa lengo la kusikiliza kero mbalimbali za wananchi.
Mkuu wa Idara ya Ardhi na Maliasili, Ndg.Mazengo Sabaya akitoa maelezo ya Kitalaam kujibu hoja za wananchi wa Kata ya Nkololo wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka wilayani Bariadi aliyofanya kwa lengo la kusikiliza kero mbalimbali za wananchi.
Afisa Elimu wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, Doreen Rutahanamilwa akitoa maelezo ya Kitalaam kujibu hoja za wananchi wa Kata ya Nkololo wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka wilayani Bariadi aliyofanya kwa lengo la kusikiliza kero mbalimbali za wananchi.
Baadhi ya wananchi  wa Kata ya Nkololo wilaya ya Bariadi wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka katika Mkutano wa Hadhara aliofanya katika Kata hiyo wakati wa ziara yake yenye lengo la kusikiliza kero mbalimbali za wananchi.
Katibu wa CCM Mkoa wa Simiyu, Ndg. Donald Magesa akizungumza na wananchi wa Kata ya Nkololo (hawapo pichani) wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa huo, Mhe.Anthony Mtaka wilayani Bariadi, aliyofanya kwa lengo la kusikiliza kero mbalimbali za wananchi.
Yusufu Masunga Mkazi wa Nkololo akiwasilisha kero yake kwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka (hayupo pichani) wakati wa ziara  aliyofanya Kata ya Nkololo wilayani Bariadi kwa lengo la kusikiliza kero mbalimbali za wananchi.
Baadhi viongozi na Wataalam wa Wilaya ya Bariadi na Mkoa wa Simiyu wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa huo, Mhe.Anthony Mtaka (hayupo pichani) wakati wa ziara  aliyofanya katika Kata ya Nkololo wilayani Bariadi, kwa lengo la kusikiliza kero mbalimbali za wananchi.
Maduhu Kalimilo Mkazi wa Kijiji cha Ikungulyandili wilayani Bariadi akiwasilisha kero yake kwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka (hayupo pichani) wakati wa ziara  aliyofanya kwa lengo la kusikiliza kero mbalimbali za wananchi.
Baadhi ya wananchi  wa Kata ya Nkololo wilayani Bariadi wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka katika Mkutano wa Hadhara aliofanya katika Kata hiyo wakati wa ziara yake yenye lengo la kusikiliza kero mbalimbali za wananchi.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!