Mwenge wa Uhuru umemaliza mbio zake leo Mkoani
Simiyu na kukabidhiwa katika Mkoa wa Mara, ambapo miradi 33 kati 34 sawa na
asilimia 97 ya miradi iliyopitiwa na Mwenge wa Uhuru katika Halmashauri zote
sita imekubaliwa na kuzinduliwa, kukaguliwa, kuonwa na kuwekewa mawe ya msingi.
Akitoa taarifa kabla ya kukabidhi Mwenge wa
Uhuru mkoani Mara, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka amesema ni mradi
mmoja tu wa maji ambao umeonekana kuwa na kasoro ambapo amebainisha kuwa kasoro
hizo zitafanyiwa kazi na kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru mwaka 2019 atapata
taarifa mapema iwezekanavyo ya namna zilivyofanyiwa kazi.
Naye Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Mwaka
2019, Ndg. Mzee Mkongea Ali amewapongeza viongozi na wananchi Mkoani Simiyu,
huku akibainisha kuwa tangu mbio za
Mwenge wa Uhuru mwaka 2019 zizinduliwe rasmi Mkoani Songwe, Simiyu ni mkoa wa
Tisa lakini umeonekana kuwa mkoa nambari moja kwa namna ulivyolitekeleza jukumu
hili.
Aidha, amesema yeye pamoja na wakimbiza Mwenge
wa Uhuru Kitaifa wengine katika kipindi cha siku sita walizokaa Simiyu wamebaini
kuwepo kwa umoja, ushirikiano na kuheshimiana miongoni mwa wananchi, watumishi
na viongozi mambo ambayo ni ya msingi katika maendeleo.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,
Mhe. Anthony Mtaka (kushoto) akimkabidhi Mwenge wa Uhuru, Mkuu wa Mkoa wa Mara,
Mhe. Adam Malima, Mei 28, 2019.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Mwaka 2019, Ndg. Mzee
Mkongea Ali akiongea na baadhi ya viongozi wa mkoa wa Simiyu kabla ya
kukabidhiwa rasmi mkoani Mara, Mei 28, 2019
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(mwenye
karatasi mkononi) akiwasilisha taarifa yam bio za Mwenge wa Uhuru Mkoani
Simiyu, kabla ya kukabidhi Mwenge wa Uhuru Mkoani Mara, Mei 27, 2019.
0 comments:
Post a Comment