Friday, May 3, 2019

NAIBU WAZIRI MADINI ATOA SIKU MOJA KWA MAKANDARASI KUKAMILISHA JENGO LA SOKO LA MADINI SIMIYU


Naibu Waziri wa Madini, Mhe. Stanslaus Nyongo ametoa muda wa siku moja kwa Mkandarasi  SUMA JKT anayejenga Jengo la Kituo cha Umahiri Simiyu kuamilisha sehemu ya Jengo hilo iliyopangwa kutumika kama Soko la Madini la Mkoa.

Nyongo ameyasema hayo Mei  02, 2019 wakati alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa jengo hilo ambalo sehemu litatumika kama kituo cha umahiri na sehemu kama Soko la Madini la Mkoa.

“ Kwa  mkoa wa Simiyu tumeona hapa tunaweza kupatumia kwa kuanzia kwenye soko la madini, nimeshatoa maagizo kuwa jengo hili walimalizie mara moja, ili waweze kutoa sehemu ambayo itatumika kwa ajili ya soko la madini na kufikia kesho jioni tunataka jengo hili lianze kutumika kama soko la Madini “ amesema Nyongo.

Aidha, Nyongo amesema anatumia  fursa hiyo kuwajulisha wachimbaji  wadogo wadogo wa madini kuwa Simiyu kutakuwa na jengo ambalo litatumika kununua na kuuza madini.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema kama mkoa wamejipanga vizuri katika soko la madini, huku akiwakaribisha wafanyabiashara wa madini kutoka mkoa wa Simiyu  na mikoa jirani kufika katika kituo hicho ambacho amesema kitakuwa kituo bora chenye uhakika wa kufanya biashara hapa nchini.

Mtaka ameongeza kuwa kituo hicho ambacho kitafunguliwa rasmi wiki ijayo kitatoa fursa kwa Watanzania kuanza kuangalia ufanyaji wa biashara katika eneo la madini kwa njia ambazo ni halali, akatoa wito kwa wafanyabiashara wa mkoa wa Simiyu pamoja na kuwekeza biashara katika kilimo, mifugo na viwanda wawekeze pia katika biashara ya madini.

Naye Sajenti Emmanuel Igogo kutoka SUMA JKT amesema agizo la Naibu Waziri la kukamilisha sehemu ya Jengo la Kituo ca Umahiri ambayo itatumika kama soko la madini (Kituo cha kuuzia madini) litatekelezwa kama lilivyoagizwa.

“ Tutatekeleza agizo la Mhe. Naibu Waziri tutaanza leo kulifanyika kazi na kwa kuwa kazi hii haikuwepo kwenye mkataba wetu wa awali nitawasiliana na viongozi wangu na tutakamilisha” alisema Sajenti Igogo.
MWISHO



Naibu Waziri wa Madini, Mhe. Stanslaus Nyongo( wa pili kushoto)  akizungumza na baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Simiyu wakati alipotembelea Kituo cha Umahiri kilichopo Nyaumata Bariadi kukagua maendeleo ya ujenzi wa Kituo hicho, ambacho kimeamriwa kuwa sehemu ya jengo hilo ikamilike haraka na ianze kutumika kama Soko la Madini.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ( watatu kushoto) akichangia jambo kwenye mazungumzo wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Madini, Mhe. Stanslaus Nyongo( wa pili kushoto)  alipotembelea Kituo cha Umahiri kilichopo Nyaumata Bariadi kukagua maendeleo ya ujenzi wa Kituo hicho, ambacho kimeamriwa kuwa sehemu ya jengo hilo ikamilike haraka na ianze kutumika kama Soko la Madini.
Naibu Waziri wa Madini, Mhe. Stanslaus Nyongo( wa pili kulia)  akizungumza na baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Simiyu wakati alipotembelea Kituo cha Umahiri kilichopo Nyaumata Bariadi kukagua maendeleo ya ujenzi wa Kituo hicho, ambacho kimeamriwa kuwa sehemu ya jengo hilo ikamilike haraka na ianze kutumika kama Soko la Madini.
Jengo la Kituo cha Umahiri Simiyu kilichopo Nyaumata Bariadi, ambacho kimeamriwa kuwa sehemu ya jengo hilo ikamilike haraka na ianze kutumika kama Soko la Madini.
Meneja wa TANROADS Mkoa wa Simiyu, Mhandisi. Albert Kent (kushoto) akizugumza na baadhi ya viongozi wakati wa Naibu Waziri wa Madini, Mhe. Stanslaus Nyongo( wa pili kushoto)  alipotembelea Kituo cha Umahiri Simiyu kilichopo Nyaumata Bariadi kukagua maendeleo ya ujenzi wa Kituo hicho, ambacho kimeamriwa kuwa sehemu ya jengo hilo ikamilike haraka na ianze kutumika kama Soko la Madini.
Fundi akiendelea kupaka rangi  katika hatua za ukamilishaji kwenye Jengo la Kituo cha Umahiri Simiyu Simiyu kilichopo Nyaumata Bariadi, ambacho kimeamriwa kuwa sehemu ya jengo hilo ikamilike haraka na ianze kutumika kama Soko la Madini.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!