Jumla
ya wakazi 346,365 wa Wilaya ya Itilima na maeneo ya jirani wanatarajia
kunufaika na ujenzi wa mradi wa hospitali ya Wilaya ya Itilima inayotarajiwa
kukamilika Juni 30 mwaka 2019.
Mradi
huo wenye lengo la kuimarisha upatikanaji wa huduma za afya na kusogeza karibu
huduma hiyo kwa wananchi ,hadi kukamilika kwake unatarajia kutumia kiasi cha sh
bil 1 .5.
Akisoma
taarifa ya mradi wa Ujenzi wa Hospital ya Wilaya ya Itilima kwa kiongozi wa
mbio za mwenge wa Uhuru mwaka 2019,Mzee Mkongea Ali ,mganga mkuu wa Wilaya hiyo
Dk Anorld Charles amesema kuwa kukamilika kwa mradi huo kutarahisisha huduma
za wananchi wa Wilaya humo.
Dk
Charles ameeleza kuwa wananchi wengi wa Wilaya hiyo wamekuwa wakitembea umbali
mrefu wa wastani wa kilometa 45 hadi 50 kufuata huduma za afya katika hospitali
ya Bariadi.
Amesema
kutokana na hali hiyo ya kutembea umbali mrefu,wengi wao hupoteza maisha kwa
kukosa huduma stahiki za haraka hususani akinamama wajawazito ambao wengi wao
hupoteza damu nyingi njiani.
Ameongeza
kuwa endapo hospitali hiyo itakamilika kwa muda muafaka,itasaidia sana
kupunguza vifo vya akinamama wajawazito wanaopoteza damu nyingi pindi wawapo
njiani kuelekeza katika hospitali ya wilaya ya Bariadi.
Amesema
kwa mwaka 2018 (Jan hadi Dec) pekee jumla ya akinamama 5 walipoteza maisha kwa
kuvuja damu nyingi kwa kucheleweshwa kufika mapema katika zahanati na hospitali
zilizo karibu nao.
Naye
kiongozi wa mbio za mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka 2019 Ndg. Mzee Mkongea Ali
alisema kuwa jitihada za Ukamilishaji wa hospitali hiyo zinatakiwa ziwe za
haraka iwezekanapo kabla ya kuisha mwaka wa fedha, kwani endapo wakishindwa
kukamilisha kwa muda husika hawataweza kupata fedha za ukamilishaji huo.
"
napenda kuwashauri kuwa ukamilishaji wa hospitali hiyo unatakiwa uwe Juni 30
mwaka huu kama ilivyoelekezwa hivyo ni lazima ujenzi uende kwa haraka usiku na
mchana...la sivyo mwaka ya fedha 2018/2019 utakapomalizika itakuwa vigumu
kupata fedha hizo zilizokuwa zimetengwa katika bajeti ya 2018/2019.
Naye
Mkuu wa Wilaya ya Itilima, Mhe. Benson Kilangi amesemaViongozi wilayani humo
watahakikisha Hospitali hiyo inakamilika kabla ya juni 30, 2019 kama
ilivyoelekezwa na Waziri wa nchi, Ofisi ya Rai TAMISEMI.
Marangwa
Maduhu mkazi wa kijiji cha Nguno Wilayani humo,amesema uwepo wa hospitali hiyo
itawasaidia sana kupunguza gharama za usafiri walizokuwa wakizitumia kufuata
matibabu Wilayani Bariadi.
Mpaka
sasa ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Itilima tayari imeshatumia kiasi cha sh
bil 1.2 sawa na asilimia 81 ya utekelezaji wake
Katika
hatua nyingine kiongozi wa mbio za mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka 2019 Ndg. Mzee
Mkongea Ali ametoa wito kwa wananchi kutunza vyanzo vya maji kwa kupanda miti
rafiki katika vyanzo vya maji na kusisitiza wale wote ambao watakiuka sheria
wachukuliwe hatua.
MWISHO
Kiongozi wa Mbio za
Mwenge wa Uhuru mwaka 2019, Ndg. Mzee Mkongea Ali akipata maelezo kuhusu ramani
ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Itilima, wakati wa mbio za mwenge wa uhuru
Mei 24, 2019 wilayani humo.
Kiongozi wa Mbio za
Mwenge wa Uhuru mwaka 2019, Ndg. Mzee Mkongea Ali akimtwisha mama ndoo mara baada
ya kuzindua mradi wa maji wa Mwamapalala wilayani Itilima, wakati wa mbio za
mwenge wa Uhuru wilayani humo, Mei 24,
2019.
Kiongozi wa Mbio za
Mwenge wa Uhuru mwaka 2019, Ndg. Mzee Mkongea Ali akikabidhi cheti wanachama wa
Klabu ya wapinga rushwa katika shule ya Sekondari Mwamapalala, mara baada ya
kuzindua klabu hiyo wakati wa mbio za mwenge wa uhuru Mei 24, 2019 wilayani
humo.
Kiongozi wa Mbio za
Mwenge wa Uhuru mwaka 2019, Ndg. Mzee Mkongea Ali akikagua moja ya vyumba
vitatu vya madarasa katika shule ya Msingi Lagangabilili, wakati wa mbio za
mwenge wa uhuru Mei 24, 2019 wilayani humo.
wanachama
wa Klabu ya wapinga rushwa katika shule ya Sekondari Mwamapalala, wakifurahia
uzinduzi wa klabu hiyo wakati wa mbio za mwenge wa uhuru Mei 24, 2019 wilayani
humo
Kiongozi wa Mbio za
Mwenge wa Uhuru mwaka 2019, Ndg. Mzee Mkongea Ali (mwenye skafu) akipata
maelezo kutoka kwa mtaalamu wa misitu wilayani Itilima, mara baada ya
kutembelea mradi huo wakati wa mbio za mwenge wa uhuru Mei 24, 2019 wilayani humo.
Moja ya majengo ya
Hospitali ya Wilaya ya Itilima
Mkuu wa Wilaya ya
Itilima Mhe. Benson Kilangi akimkaribisha Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru
mwaka 2019, Ndg. Mzee Mkongea Ali kabla ya kukabidhiana Mwenge wa Uhuru na Mkuu
wa Wilaya ya Meatu, Dkt. Joseph Chilongani
Baadhi ya wananchi
wakimsikiliza :- Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2019, Ndg. Mzee
Mkongea Ali (hayupo pichani) wakati wa mbio za mwenge wa uhuru Mei 24, 2019
wilayani humo.
0 comments:
Post a Comment