Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ametoa wito
kwa viongozi na watendaji wa Serikali mkoani hapa kuona umuhimu wa
kuwashirikisha viongozi wa dini, siasa na wa kimila katika utoaji wa elimu kwa
jamii na kuwahamasisha wanawake wajawazito kuhudhuria kliniki na kujifungulia
katika vituo vya kutolea huduma za afya ili kuzuia vifo vitokanavyo na uzazi..
Mtaka ameyasema hayo wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya
Uwajibikaji katika kuzuia vifo vitokanavyo na uzazi ijulikanayo kama
JIONGEZE, Tuwavushe Salama uliofanyika Mei 02, 2019 Mjini Bariadi.
“ Ni vizuri tukaongeza wigo wa kutoa elimu kwa jamii kuhusu umuhimu wa mama
wajawazito kuhudhuria kliniki kipindi cha ujauzito na kuhakiksha
wanajifungulia kwenye vituo vya kutolea huduma za afya; viongozi wa dini,siasa
na wa kimila wana nafasi kubwa kwenye jambo hili muone namna ya kuwashirikisha
“ alisema Mtaka.
Amesema Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa afya ikiwa ni
pamoja na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu
Duniani(UNFPA) imeboresha vituo vya kutolea huduma, hivyo ni vema jamii
ikaelimishwa umuhimu wa kutumia huduma za afya ili kuokoa maisha ya mama na
mtoto.
Katika hatua nyingine Mtaka ameishukuru UNFPA kwa namna ilivyosaidia katika
ujenzi wa miundombinu ya afya,vifaa na vitendea kazi kama magari ya kubeba
wagonjwa huku akisisitiza viongozi na watendaji walioshiriki katika uzinduzi wa
kampeni hii kutoka na dhamira ya kuwavusha salama akina mama wajawazito na
watoto na kupinga vifo vitokanavyo na uzazi..
Mwakilishi wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za
Mitaa, Dinna Atinda ameusisitiza uongozi wa mkoa kusimamia
vituo vinavyotoa huduma za afya za msingi na dharura kuhakikisha vinatoa huduma
bora kwa wananchi.
Naye Mwakilishi wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na
Watoto, Salome Mwijuma ametoa wito kwa jamii kuendelea kuwasaidia
wanawake wajawazito waweze kuhudhuria kliniki muda wote, wapate lishe bora na
kujifungulia katika vituo vya kutolea huduma ili wajifungue salama.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Dkt. Mageda Kihulya amesema mwaka 2015
watoto 680 walifariki na mwaka 2018 watoto 640 walifariki, wakati
kwa upande wa akina mama wanaojifungua vifo vimepungua kutoka 48 mwaka 2015 na
kufikia 40 mwaka 2018, jambo ambalo linaonesha kuwa nguvu ya ziada
kutoka wadau mbalimbali inahitajika kumaliza tatizo hili.
Dkt. Mageda amesema sababu zinazosababisha vifo vingi vya akina mama
wajawazito kama vile kutokwa na damu nyingi wakati wa kujifungua na mkingamo wa
uzazi zinaweza kuzuilika, hivyo akatoa wito kwa wakina mama kujifungulia katika
vituo vya kutolea huduma kuzuia vifo hivyo, huku akisisitiza watoto chini ya
miaka mitano nao wapewe chanjo kuzuia vifo..
Makamu Mwakilishi mkaazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia
idadi ya watu Duniani(UNFPA) hapa nchini, Dkt. Hashina Begum amesema shirika
hilo litaendelea kushirikiana na Serikali katika jitihada mbalimbali za
kupunguza vifo vya akina mama wajawazito na watoto.
MWISHO
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akikata
utepe kuashiria Uzinduzi wa Kampeni ya Uwajibikaji katika kuzuia vifo vitokanavyo na uzazi
ijulikanayo kama JIONGEZE, uliofanyika Tuwavushe
Salama, Mei 02, 2019 Mjini Bariadi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka( wa tano
kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi na wadau wa
afya baada ya Uzinduzi wa Kampeni ya
Uwajibikaji katika kuzuia vifo
vitokanavyo na uzazi ijulikanayo kama JIONGEZE, Tuwavushe Salama, uliofanyika Mei 02, 2019 Mjini Bariadi.
Baadhi ya viongozi na
wadau wa afya Mkoani Simiyu wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony
Mtaka( hayupo pichani) wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Uwajibikaji katika kuzuia vifo vitokanavyo na uzazi
ijulikanayo kama JIONGEZE, Tuwavushe Salama, uliofanyika Mei 02, 2019 Mjini Bariadi.
Baadhi ya viongozi na
wadau wa afya Mkoani Simiyu wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony
Mtaka( hayupo pichani) wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Uwajibikaji katika kuzuia vifo vitokanavyo na uzazi
ijulikanayo kama JIONGEZE, Tuwavushe Salama, uliofanyika Mei 02, 2019 Mjini Bariadi.
Kutoka kulia Mkuu wa
Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Makamu Mwakiilishi mkaazi wa Shirika la
Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu Duniani(UNFPA) hapa nchini,
DKT. Hashina Begum na Mratibu wa UNFPA
Mkoa wa Simiyu, Dt. Amir Batenga wakiteta jambo wakati wa hafla ya Uzinduzi wa Kampeni ya Uwajibikaji katika kuzuia vifo vitokanavyo na uzazi
ijulikanayo kama JIONGEZE, Tuwavushe Salama, uliofanyika Mei 02, 2019 Mjini Bariadi.
Makamu Mwakiilishi
mkaazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu
Duniani(UNFPA) hapa nchini, DKT. Hashina Begum akizungumza na viongozi na wadau
wa afya Mkoani Simiyu,wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Uwajibikaji katika kuzuia vifo vitokanavyo na uzazi
ijulikanayo kama JIONGEZE, Tuwavushe Salama, uliofanyika Mei 02, 2019 Mjini Bariadi.
Baadhi ya viongozi na
wadau wa afya Mkoani Simiyu wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony
Mtaka( hayupo pichani) wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Uwajibikaji katika kuzuia vifo vitokanavyo na uzazi
ijulikanayo kama JIONGEZE, Tuwavushe Salama, uliofanyika Mei 02, 2019 Mjini Bariadi.
Mwakilishi kutoka Ofisi
ya Rais TAMISEMI, Dinna Atinda akizungumza na viongozi na wadau wa afya Mkoani
Simiyu,wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Uwajibikaji katika kuzuia vifo vitokanavyo na uzazi
ijulikanayo kama JIONGEZE, Tuwavushe Salama, uliofanyika Mei 02, 2019 Mjini Bariadi.
Mganga Mkuu wa Mkoa,
Dkt. Mageda Kihulya akiwasilisha taarifa ya hali ya vifo vya wanawake na watoto, wakati wa hafla ya Uzinduzi wa Kampeni ya Uwajibikaji katika kuzuia vifo vitokanavyo na uzazi ijulikanayo
kama JIONGEZE, Tuwavushe Salama, uliofanyika
Mei 02, 2019 Mjini Bariadi.
Katibu Tawala wa Mkoa
wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini
akizungumza na viongozi na wadau wa afya Mkoani Simiyu,wakati wa
Uzinduzi wa Kampeni ya Uwajibikaji
katika kuzuia vifo vitokanavyo na uzazi ijulikanayo kama JIONGEZE,
Tuwavushe Salama, uliofanyika Mei 02,
2019 Mjini Bariadi.
Katibu Tawala wa Mkoa
wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini (kushoto)
akiteta jambo na Mwakilishi kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI, Dinna Atinda wakati
wa Uzinduzi wa Kampeni ya Uwajibikaji
katika kuzuia vifo vitokanavyo na uzazi ijulikanayo kama JIONGEZE,
Tuwavushe Salama, uliofanyika Mei 02,
2019 Mjini Bariadi.
Mganga Mkuu wa Mji wa
Bariadi akichangia jambo wakati wa
Uzinduzi wa Kampeni ya Uwajibikaji
katika kuzuia vifo vitokanavyo na uzazi ijulikanayo kama JIONGEZE,
Tuwavushe Salama, uliofanyika Mei 02,
2019 Mjini Bariadi.
Mkuu wa Wilaya ya
Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga akichangia
jambo wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Uwajibikaji katika kuzuia vifo vitokanavyo na uzazi
ijulikanayo kama JIONGEZE, Tuwavushe Salama, uliofanyika Mei 02, 2019 Mjini Bariadi.
Baadhi ya viongozi na
wadau wa afya Mkoani Simiyu wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony
Mtaka( hayupo pichani), wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Uwajibikaji katika kuzuia vifo vitokanavyo na uzazi
ijulikanayo kama JIONGEZE, Tuwavushe Salama, uliofanyika Mei 02, 2019 Mjini Bariadi.
Makamu Mwakiilishi
mkaazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu
Duniani(UNFPA) hapa nchini, DKT. Hashina Begum(katikati walioketi) akiwa katika
piccha ya pamoja na baadhi ya viongozi, wataalam na wadau wa afya, baada ya wa Uzinduzi wa Kampeni ya
Uwajibikaji katika kuzuia vifo
vitokanavyo na uzazi ijulikanayo kama JIONGEZE, Tuwavushe Salama,
uliofanyika Mei 02, 2019 Mjini Bariadi.
Makamu Mwakiilishi
mkaazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu
Duniani(UNFPA) hapa nchini, DKT. Hashina Begum(katikati walioketi) akiwa katika
piccha ya pamoja na baadhi ya viongozi, wataalam na wadau wa afya, baada ya wa Uzinduzi wa Kampeni ya
Uwajibikaji katika kuzuia vifo
vitokanavyo na uzazi ijulikanayo kama JIONGEZE, Tuwavushe Salama,
uliofanyika Mei 02, 2019 Mjini Bariadi.
Mkuu wa Wilaya ya
Busega, Mhe Tano Mwera(kushoto) akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Bariadi,
Mhe. Festo Kiswaga wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Uwajibikaji katika kuzuia vifo vitokanavyo na uzazi
ijulikanayo kama JIONGEZE, Tuwavushe Salama, uliofanyika Mei 02, 2019 Mjini Bariadi.
Makamu Mwakiilishi
mkaazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu
Duniani(UNFPA) hapa nchini, DKT. Hashina Begum(katikati walioketi) akiwa katika
piccha ya pamoja na baadhi ya viongozi, wataalam na wadau wa afya, baada ya wa Uzinduzi wa Kampeni ya
Uwajibikaji katika kuzuia vifo
vitokanavyo na uzazi ijulikanayo kama JIONGEZE, Tuwavushe Salama,
uliofanyika Mei 02, 2019 Mjini Bariadi.
0 comments:
Post a Comment