Wednesday, March 30, 2016

UONGOZI MKOANI SIMIYU WABAINI WATUMISHI HEWA 33


Kufuatia agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John Pombe Magufuli la kuhakiki watumishi wa Umma nchini, Uongozi wa Mkoa wa Simiyu umebaini watumishi hewa 33 na watoro 29 kati ya watumishi 13,174 wa Mamlaka za Serikali za Mitaa za Serikali kuu.
Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony J.Mtaka (kulia) akizungumza na viongozi wa wilaya za Mkoa wa Simiyuwakati wa tathmini ya hali ya watumishi wa Mkoa wa Simiyu jana, katika ukumbi wa mikutano katika Ofisi yake, kutoka Kushoto wa kwanza ni Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe.Ponsiano Nyami, Mkuu wa Wilaya ya Maswa,Mhe. Rosemary Kirigini na Mkuu wa Wilaya ya Meatu Mhe. Erasto Sima.
Akizungumza na Waandishi wa Habari jana mara baada kikao cha kutathmini hali ya Watumishi katika Mkoa , Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony J. Mtaka alisema uwepo wa watumishi hewa na watoro umeisababishia Serikali hasara ya shilingi 320,993,683.69 .

Mtaka alisema mara baada ya kubaini uwepo wa watumishi  watoro, amewaagiza Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kusimamisha mishahara ya watumishi hao  wakiwemo walimu ambao walikwenda masomoni bila ruhusa ya waajiri wao na wale ambao mashauri yao yapo kwa muda mrefu katika Idara ya Utumishi wa Walimu (TSD) mpaka mashauri hayo yatakapopatiwa ufafanuzi.
 Kutokana na idadi ya watumishi wa kada ya ualimu kuwa kubwa katika watumishi hewa na watoro kuliko kada zingine, Uongozi wa Mkoa wa Simiyu umeshauri Idara ya Utumishi wa Walimu (TSD) kushughulikia kwa haraka mashauri ya walimu yanayopelekwa kutoka ngazi za Wilaya na Mikoa na kutoa ufafanuzi kwa wakati, ili kuondokana hasara ya kulipa mishahara hewa.

Aidha , Uongozi wa Mkoa umeshauri Ofisi ya HAZINA na Utumishi kuona namna ya kugatua madaraka kutoka Ofisi kuu kwenda Ofisi za kanda na mikoa, ili pale mtumishi anapotakiwa kusimamishiwa mshahara wake anapostaafu,kufariki au kufukuzwa kazi iwe rahisi kuwaondoa katika mfumo wa mishahara badala ya kusubiri Ofisi kuu Dar es Salaam kuwatoa kwenye mfumo wa mishahara.


Hali ya watumishi watoro katika Mkoa wa Simiyu inaongozwa na Halmashauri ya Wilaya ya Meatu yenye watumishi watoro 18, hewa mmoja (01), ikifuatiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi yenye watumishi watoro 11, hewa watano (05), huku Halmashauri ya Mji wa Bariadi ikiwa na watumishi hewa watano (05), Itilima sita (06), Busega wanne na Maswa 12 ambapo Halmashauri hizi nne (04) hazina watumishi watoro. 

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!