Tuesday, March 15, 2022

MKANDARASI APEWA SIKU 7 KABLA MKATABA KUVUNJWA

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. David Kafulila ametoa siku saba kwa Kampuni ya Daska Company Ltd, kuhakikisha inakamilisha ujenzi wa Barabara ya Byuna/Nkindwabiye/ Halawa barabara yenye  urefu wa 14.9km. Thamani ya mradi/mkataba huo ni Tsh.139.993 mln.

“Tofauti na hapo mkataba uvunjwe na taratibu zifuatwe kupata kampuni nyingine.Sina na sijawahi kuwa na subira kwa wakandarasi wababaishaji. Nitoe wito Wakandarasi wote mkae mguu sawa. Nitafuta kazi zote zinazosuasua ili kubaki na wakandarasi wenye uwezo wa kutekeleza kazi kwa mujibu wa mikataba wanayosaini".Amesema Kafulila.

Kafulila ametoa maelekezo hayo kwa Meneja wa Mkoa wa  Mamlaka ya Barabara vijijini( TARURA) wakati wa ziara yake leo Machi14, 2022 wilaya ya Bariadi. Mwisho.









Thursday, March 10, 2022

Katika kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani, TUGHE-Simiyu Yatoa Msaada Kituo cha Afya Ikindilo.


























Sherehe ya siku wa Wanawake duniani, huadhimishwa kila tarehe nane ya mwezi wa tatu. Katika kuadhimisha sherehe hizo, 2022, kama ilivyo ada Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya (TUGHE-Simiyu), waliamua kufanya matendo ya huruma Wilayani Itilima ambapo ndipo sherehe za siku ya mwanamke kimkoa zimefanyika.

Akiwakaribisha wilayani Itilima Mkurugenzi wa Wilaya ya Itilima, Bi. Elizabeth Gumbo amesema ‘’ninafuraha kubwa niwakaribishe sana Wilaya ya Itilima, Pongezi sana  Kwa Mwenyekiti na katibu wa TUGHE Bi. Elizabeth na  Catherine. Niwaombee baraka za mwenyezi Mungu,niwatie moyo wanawake wenzangu,sisi tunaweza, na tumejionea wazi kabisa kutoka kwa Mama yetu, Rais wetu ambaye ni mwanamama Mhe. Samia Suluhu Hassan, kwani, kwa Wilaya ya  Itilima tu ametupatia fedha ambazo zimewezesha ujenzi wa vyumba 82 vya madarasa. Hivyo wakina mama sote tuwe na moyo wa kumuunga mkono Rais wetu mama Samia Suluhu Hassan, tupambane wenyewe, kila mmoja katika nafasi aliyopewa akaonyeshe uwezo wake. Wakina mama tuendelee kuwashauri kina mama wengine, binti zetu, familia, watoto na Taifa letu, kwani wakina mama ni jeshi kubwa’’.

Akielezea sababu za TUGHE-Simiyu, kuchagua eneo hilo na kufanya matendo ya huruma, Mwenyekiti kamati za Wanawake TUGHE Mkoa wa Simiyu,Bi.Elizabeth Nangali Gelege   amesema “ tumeamua kufanya haya matendo ya huruma katika kituo cha afya cha Ikindilo baada ya kufahamishwa na Mganga Mkuu wilaya ya Itilima Dkt. Anorld Musiba, kuwa kituo cha afya Ikindilo kina mahitaji. Tumekuja na mashuka, mama Samia Suluhu Hassan  ameleta  majengo, sisi tumeleta sabuni pamoja na mashuka vyote vikiwa na thamani ya Tsh. Milioni moja. 

Akizungumzia kauli mbiu ya mwaka huu ya siku ya wanawake duniani, ambayo inasema:“Kizazi cha Haki na Usawa Kwa Maendeleo, Tujitokeze Kuhesabiwa’’. Bi. Geleje amesema Kauli mbiu hii inaonyesha wazi kwamba huu ni mwaka wa sensa, hivyo wanawake tujitokeze kuhesabiwa.Kila mwanamke atumie kipaji chake kuhakikisha watu wa familia yake wanahesabiwa na kuendeleza nchi.

Akizungumzia msaada huo Katibu wa TUGHE Mkoa wa Simiyu Bi.Catherine Nyingi amesema katika kuonyesha mshikamano,sisi TUGHE tuna kawaida ya kufanya matendo ya huruma na kurudisha huduma katika jamii.Kama ambavyo tumefanya leo katika kituo hiki cha afya cha Ikindilo.

Akitoa taarifa kuhusu kituo cha afya Ikindilo, Mganga mfawidhi Kituo cha afya Ikindilo Dkt. Elizabeth Malunde amesema Kituo cha afya Ikindilo  ni kimoja kati ya vituo 3 vya afya Wilayani itilima. Kituo hiki kimepanda kutoka daraja namba mbili na sasa kipo namba tatu. 

Kituo cha afya Ikindilo kinatoa huduma mbalimbali kama vile chanjo cha UVIKO,Kliniki ya HIV, tuanafanya tohara kwa watoto wa kiume, tunahudumia wangonjwa wa nje na ndani, poa tunatoa huduma za mama na mtoto. Mwaka jana mwezi wa saba tulifungiwa mfumo wa GhoTomis, hivyo malipo yoye ya huduma za afya yanafanyika kwa kutumia mfumo. Upatikanaji wa Dawa ni  100%, upatikanaji wa damu 100% pia tuna duka la Dawa. 

Pamoja na mafaniko tajwa hapo juu bado tunakabiliwa na  mbalimbali.Changamoto kubwa tuliyo nayo ni kuwa hatuna eneo ila tupo kwenye mchakato wa kutafuta eneo . Pia tuna changamoto ya nyumba za watumishi kwani tuna Nyumba 6 tu na hivyo kufanya watumishi wengine kuishi katika maeneo ya mbali, uchakavu wa majengo, tuna changamoto ya jengo la kulaza wagonjwa- OPD, Changamoto ya watumishi, kituo hakina uzio na hivyo kufanya wanyama kuingia  ndani ya eneo la kituo cha afya,pia hatuna wodi ya kulaza watoto wachanga.Mwisho.

Wednesday, March 9, 2022

Wanawake Endeleeni Kufanya Kazi Kwa Bidii na Kuonyesha Mfano, Mafanikio Yenu Yasiwapelekee Kujisahau Kwamba Baba ndie Kichwa Cha Familia- RC KAFULILA

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. David Kafulila ameyasema hayo wakati wa sherehe ya siku ya wanawake Duniani, ambayo kimkoa imefanyika katika wilaya ya Itilima.

Mhe. Kafulila ambaye ndiye alikuwa mgeni rasmi ametembelea na kukagua mabanda ya wajasiriamali na kuwaagiza wakuu wa wilaya na wakungugenzi kutoa kipaumbele cha mikopo kwa wamama wajasiliamali  ambao bado hawajapata mikopo hiyo.


Akizungumza wakati wa maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani ,Mhe. Kafulilamesema “ sisi sote tumetoka kwa mama, binadamu pekee ambaye hakutoka kwa mama ni Adam pamoja na Hawa ambaye alitoka kwenye ubavu wa Adam, ambaye ni baba.Hivyo hii ni siku pekee ambayo inatupa fursa ya kutafakari safari ya mwanamke katika kutoa mchango wake kwenye taifa lake na dunia hii. 


Kwa uzoefu niliokuwa nao moja ya sifa kubwa ya mwananamke ni kuwa,Wanawake hawapendi kukosea, hivyo atafanya kila kinachowezekana ili asikosee, kwa hiyo leo tunasherehekea siku ya wanawake,mama ambaye ni nguzo ya familia na viumbe wenye uvimilivu kuliko kiumbel kingine chochote duniani.

 

“Wanawake ni waaminifu sana na tafiti zinaonyesha kwamba kati ya wanaume na wanawake, wanaorejesha mikopo kwa wakati ni wanawake. Hivyo Wakurugenzi na wakuu wa Wilaya katika mikopo yote mnayotoa kwa makundi ya wanawake, vijana na wenye ulemavu, mikopo kwa wanawake ipewe kipaumbelekwani hawa wamama/dada zetu endapo wanapewa mikopo ambayo ni mikubwa kidogo wana historia ya  kulipa kwa wakati. Tafiti  za kimataifa zinaonyesha Mwanamke anapofanya kazi na kupata kipato anarudisha nyumbani 90% ya kipato chakelakini mwanaume anapeleka 35% ”.Ameeleza Kafulila.

 

Aidha, akizungumzia mataifa mengine, Mhe. Kafulila ameitaja nchi ya Marekani ambayo iliwachukua  miaka 100 kuruhusu mwanamke kupiga kura,wakati kwa nchi ya Tanzania mifumo yetu ya kisheria haijawahi kumzuia mwanamke kupiga kura. Sanjari na hayo kwa kipindi cha mwaka mmoja wa Rais mwanamama Mhe.Samia Suluhu Hassan amefanikiwa kuituliza nchi na kuikusanya pamoja.Anaendesha nchi kwa viwango vya juu kabisa na nchi imetulia.Mhe. Samia Suluhu Hassan amewezesha upatikanaji wa fedha za miradi kila mahali. Kwa upande wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Samia Suluhu Hassan,ametoa fedha ambazo zimewezesha miradi 26 ya maji,miradi 58 ya barabara-TARURA, Miradi 37 ya TANROADS kufanyika.Amewezesha miradi 60 ya umeme kufanyika ilikuhakikisha kuwa umeme unapatikana katika vijiji 220 kwa kipindi cha miezi 18, ili ifikapo mwanzoni mwa 2023, mkoa mzima wa Simiyu uwe na umeme.

 

Vilivile fedha za Mama Samia zimewezesha mkataba mkubwa wa maji wenye thamani ya Tsh. 400 bln kufanyika mradi ambao utawezesha vijiji 240 vya mkoa wa Simiyu kupata maji.Mhe.Rais amewezesha upatikanaji wa Tsh. 5.1bln, ambazo zinatumika katika ujenzi wa majengo 25 kwa mpigo ya Chuo cha ufundi VETA.


Mama Samia ndio mfano wa kuigwa kwani amechukua mkopo mfuko wa fedha za kimataifa, mkopo wa UVIKO-19, na kuzitumia kujenga madarasa, kununua vifaa tiba, magari ya kubeba wagonjwa, mapinduzi sekta ya maji, umeme na elimu.

 

“Hivyo wanawake ninyi ni jeshi kubwa na mnaweza kufanya mambo makubwa zaidi.Natamani mfanye kitu kikubwa zaidi, Kamati ya Usalama nusu ya wajumbe ni wanawake. Wabunge wengi ni wanawake, Viongozi wa Taasisi nyingi mkoa wa Simiyu ni wanawake na wanasaidia sana sababu wengi ni wachapa kazi na wanafanya kazi vizuri Sana. Mimi kama kiongozi wenu nitawapa kila aina ya ushirikiano,natamani nione jambo kubwa kuliko mikoa mingine litakaloanzishwa na kufanywa na wanawake wa Simiyu, ili  watu wengine waje kujifunza, endeleni kufanya kazi kwa bidii na kuonyesha mfano, mafanikio yenu yasiwapelekeekujisahau kwamba baba ndie kichwa cha familia.Amesisitiza Kafulila

 

Aidha maadhimisho ya siku ya wanawake duniani Mkoani Simiyu yaliendana sambamba na matendo ya hiruma,ambazo zilitia ndani utoaji wa  madaftari 5000, ambayo yatasambazwa katika shule mbalimbali za mkoa wa Simiyu pamoja na mashuka na sabuni katika kituo cha afya cha ikindilo, wilayani Itilima.

 

Akizungumza Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu Bi. Prisca Kayombo amesema “wakina mama hawa kwa upendo wao wamechanga fedha ambazo zimetumika kununua madaftari 5000 ambayo yatagawiwa katika shule za wilaya zote za mkoa wa Simiyu”.Bi. Prisca Kayombo, amewaeleza washirki wa halfa hiyo kuwa, pamoja na 08/03/2022 kuwa kilele cha siku wa Wanawake Duniani kuanzia 01/03/2022 hadi 08/03/2022, shughuli mbalimbali zimekuwa zikifanywa na kina mama, hii ikiwa ni pamoja na kutoa misaada mbalimbali, kutoa elimu kwa umma, pia baadhi ya kina mama wamepewa fursa ya kupata mikopo.Kawaida “Wakina mama hawakubali kushindwa, hivyo tukiwa kama Malkia tunapaswa kungara na kuwa na umoja’’.Amesisitiza Bi. Kayombo.

 

Nae Mkuu wa Wilaya ya Itilima Mhe. Faidha Salum, amemshukuru Mkuu wa Mkoa pamoja na Katibu Tawala kwa kuiheshimisha Wilaya ya Itilima kwa kitendo cha kuipa fursa Itilima kuwa Wilaya Mwenyeji wa Maadhimisho ya siku ya Wanawake duniani, kimkoa. Aidha Mhe. Faidha amemshukuru sana ,Mam a
























Samia Suluhu Hassan, kwa kuwapatia fedha ambazo zimesaidia katika miradi mbalimbali ikiwa ni pamoja na kumtua mama ndoo kichwani. Mhe. Faidha na Wanaitilima wameahidi kushiriki kikamilifu katika suala la sensa“Tutahakikisha tunatoa watu wote ili wahesabiwe’’. Amesema Faidha.

 

Aidha pamoja na wanawake wa Mkoa wa Simiyu kushiriki kwa wingi katika siku ya wanawake dunia, siku hiyo ilihudhuriwa namwenyekiti wa  Umoja wa Wanawake (UWT-CCMMkoa wa Simiyu, Mama Manyangu,Madiwani na Wabunge wanawake wa mkoa wa Simiyu.

 

Akizungumza Mbunge anayewakilisha Vijana Mkoa wa Simiyu Mhe. Lucy Sabu aliwakumbusha wanawake kuwa “Mwanamke ni nuru iangazayo, mwanamke popote hakikisha kuwa unaangaza, jiheshimu, fanya kazi kwa bidii”amesisitiza Mhe.Lucy.Mwisho.

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!