Wednesday, March 2, 2022

Mkuu wa Majeshi Jenerali Venance Mabeyo Afanya Ziara Mkoa Wa Simiyu

Mkuu wa Majeshi Jenerali Mabeyo ametembelea wilaya za mkoa wa Simiyu ambazo ni Wilaya ya Itilima na Wilaya ya Bariadi. 

Akiwa Wilaya ya Itilima Jenerali Mabeyo alikabidhi madarasa 2, Ofisi Moja na vyoo matundu nane, yaliyojengwa na Meja Jenerali  Paulo Kisesa kwa ushirikiano na Wanajeshi wenzake.Akiwa kwenye hafla hiyo Jenerali Mabeyo aliahidi kutoa kiasi cha Tsh. 30m ambazo zitatumika kukamilisha ujenzi wa baadhi ya Miundo mbinu pamoja na Ofisi ya waalimu.

Aidha Jenerali Mabeyo  akiwa Wilaya ya Bariadi alitembelea Kata ya Matongo, Kijiji cha Matongo, na kuahidi  kuchangia kiasi Tsh. 50m ambazo zitatumika kukamilisha ujenzi wa shule ya wasichana  Matongo-Bariadi ambayo majengo yake yaliachwa tangu mwaka 2010 wakati Simiyu ikiwa sehemu ya Shinyanga.Mwisho.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!