Tuesday, March 15, 2022

MKANDARASI APEWA SIKU 7 KABLA MKATABA KUVUNJWA

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. David Kafulila ametoa siku saba kwa Kampuni ya Daska Company Ltd, kuhakikisha inakamilisha ujenzi wa Barabara ya Byuna/Nkindwabiye/ Halawa barabara yenye  urefu wa 14.9km. Thamani ya mradi/mkataba huo ni Tsh.139.993 mln.

“Tofauti na hapo mkataba uvunjwe na taratibu zifuatwe kupata kampuni nyingine.Sina na sijawahi kuwa na subira kwa wakandarasi wababaishaji. Nitoe wito Wakandarasi wote mkae mguu sawa. Nitafuta kazi zote zinazosuasua ili kubaki na wakandarasi wenye uwezo wa kutekeleza kazi kwa mujibu wa mikataba wanayosaini".Amesema Kafulila.

Kafulila ametoa maelekezo hayo kwa Meneja wa Mkoa wa  Mamlaka ya Barabara vijijini( TARURA) wakati wa ziara yake leo Machi14, 2022 wilaya ya Bariadi. Mwisho.









0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!