Monday, June 14, 2021

KATIBU TAWALA MKOA WA SIMIYU BI. PRISCA KAYOMBO AFUNGUA MICHEZO YA UMISSETA MKOA


Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu Bi. Prisca Kayombo, tarehe 11/06/2021 alifungua rasmi,michezo ya UMISSETA Mkoa, michezo ambayo ilikuwa ikifanyika katika shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa.

Akizungumza Kaimu Afisa Elimu Mkoa Bwn.Charles Maganga alisema mashindano ngazi ya Mkoa yameanza leo 11/6/21 na yatakamilika 13/6/21 kwa kuunda timu ya Mkoa. Kauli mbiu ya Mashindano haya ya mwaka 2021 ni : “Michezo,Sanaa na  Taaluma Kwa Maendeleo ya Uchumi wa Viwanda”.

Mashindano haya yana jumla ya washiriki 679, kati yao wanafunzi 600,waalimu 61, madaktari 2 na viongozi 16.Washiriki hawa ni kutoka Halmashauri zote za Mkoa.Idadi ya Michezo inayoshindaniwa ni saba na michezo 4 kati ya hiyo inahusisha wavulana na wasichana.
Michezo hiyo ni pamoja na Riadha, Mpira wa Miguu, Mpira wa Wavu, Mpira wa Mikono,Mpira wa kikapu, Mpira wa Netiboli na fani za ngoma na kwaya.

Ili kuendesha mashindano kwa ufanisi tumeunda kamati ya ndhamu, afya, usafi na mazingira. Pia tumeunda kamati za michezo.Kamati hizi zina jukumu la kusimamia uendeshaji wa michezo kwa kuzingatia sheria na kanuni za michezo husika.Na wajumbe wa kamati hizi ni waalimu wa michezo husika.Hali ya kambi ni nzuri, hatujakumbanana changamoto
yeyote, wanamichezo wana ari kubwa ya kishindana katika hali ya utulivu, upendo

Aidha Mkurugenzi wa Halmashauri ya Maswa Dkt. Fredrick Sagamiko, alimkaribisha Mgeni rasmi Bi. Kayombo na kumhakikishia kuwa hali ya Maswa ni shwari hivyo wanamichezo wasiwe na wasiwasi kabisa.

Katibu Tawala, Bi. Kayombo  ambaye  alikuwa mgeni rasmi alikuwa na haya ya kusema;
napenda kuwashukuru  Wazazi/ walezi kwa kuwaruhusu wanafunzi kushiriki michezo.Pia niwashukuru wadau mbalimbali kwa kuwezesha maandalizi mazuri.Niwapongeze wanamichezo  wote kwa kuunda timu za halmashauri, ni matumaini yangu kuwa vipaji mlivyo vionyesha vitaendelea kuonekana katika mashindano haya yatakayofanyika katika ngazi ya Taifa, Mkoani Mtwara kuanzia 20/6/2021 - 03/7/2021.

Kama ilivyo  kauli mbiu ya mwaka. huu Michezo na Sanaa ni sehemu ya Taaluma na maendeleo ya Elimu. Michezo ni muhimu kwa maendeleo ya nchi yetu na imekuwa chimbuko kubwa la kuzalisha na kukuza wanamichezo mbalimbali  wanaounda timu za Taifa. Lengo la michezo hii ni kujenga na kuimarisha umoja, udugu, upendo, mshikamano, hali ya kujiamini, kukuza taaluma na utimamu wa akili kwa wanafunzi.

Tafiti mbalimbali  zimebainisha kuwa michezo huchangia katika kuimarisha ushiriki wa wanafunzi kitaaluma kwa kupunguza utoro na kuimarisha afya za wanafunzi.Michezo imesaidia kujenga mshikamano kimkoa kwa kuwaleta pamoja wadau wa elimu na michezo.

Nitoe  wito kwa wanafunzi wote watakaochaguliwa kuunda timu ya Mkoa, mzingatie kanuni za michezo,  tumieni vipaji vyenu kuhakikisha kuwa  tunapata ushindi. Tumieni fursa hiyo kuutangaza mkoa wa simiyu.Waalimu  chagueni wanafunzi na sio mamluki kwani itakuwa aibu kwa mkoa.Ikiwa mtawela Mamluki.

Changamoto ya viwanja vya michezo, natoa maelekezo maafisa michezo, kuendelea  kupima viwanja vyote vinavyohitajika kwenye maeneo ya shule ili wakuu wa shule waweze kusimamia utengenezaji  wa viwanda hivyo kwa kushirikiana na wanafunzi na vitumike  wakati wote,tusisubiri tu kipindi cha michezo hii ya UMISSETA.

 Ili kufanya vizuri zaidi katika Sekta ya Michezo na Elimu kwa ujumla ni vyema tukazingatia yafuatayo: imarisheni nidhamu yenu katika nyanja zote,nidhamu na maadili ya waalimu na wanafunzi viendelee kudumishwa,Wanafunzi/ wanamichezo sikilizeni na kuzingatia maelekezo, mbinu na mikakati mbalimbali mtakayopewa na waalimu wenu.Watoto waende salama na kurudi salama, nidhamu na maadili vidumishwe, mahusiano kati ya waalimu na watoto, yawe ya mzazi na mtoto.Nami nawatuma mkaniletee ushindi.

Michezo sio uadui hivyo watakaoteuliwa na wasioteuliwa wasilete uadui. Maendeleo yetu hutokana na kuweka  bidii katika michezo.

Akitoa neno la shukrani Bi.Line Chanafi, alisema mgeni rasmi kwa niaba ya wenzangu nikuahidi ushirikiano. Sisi tupo vizuri na tumeanza  vizuri na hatuna mamluki, tuna wanafunzi/ wanamichezo halali, tutafanya yote uliyotuagiza na hasa nidhamu.

MWISHO























WAVUVI, SIRI YA MAFANIKIO NI KUFANYA KAZI KWA VIKUNDI

Hayo yalisemwa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. David Kafulila wakati wa Ziara yake Wilayani Busega, ambapo alipata fursa ya kuzungumza na Wavuvi wa Nyashimo.

Akifungua  Kikao hicho  Mkuu wa Wilaya ya Busega Mhe.Tano Mwera aliwafahamisha wakazi wa Nyashimo kuwa ziara hiyo ya Mkuu wa Mkoa Mpya wa Simiyu, imelenga kusikiliza kero zao na hatimae kupata ufumbuzi wa kero hizo.

Mhe.Tano aliwataka wawakilishi wa wavuvi hao kuwasilisha kero wanazokabiliana nazo katika shughuli za uvuvi, nao walikuwa na haya ya kusema;

Mwenyekiti wa Kijiji cha Nyamikoma- Bw.Kurwa Bula; Changamoto, kubwa ni upumzikaji wa siku 10 hii ni changamoto kwani sisi tukipumzisha ziwa watu kutoka maeneo mengine wanakuja kuvua kwetu kwani wao huwa hawapumzishi Ziwa, ni bora,basi hiyo sheria iwekwe kwa mikoa yote mitatu.Kama kufungwa kufungwe Wilaya zote za mikoa jirani.

Akizungumza Diwani wa Kata ya Kabita- Silas Soshola, alisema changamoto kubwa tunazokabilina nazo ni pamoja na Sheria za uvuvi, nyingi ya sheria hizo ni za zamani na si rafiki, sasa hivi tunalipa Tsh. 400,000/- na bado kuna kodi nyingi Sana,Wavuvi wetu tuna Walipia leseni, tunaomba hiyo leseni ifutwe kwani mbona wakulima hawalipi leseni hizo,tunahitaji Masoko, tunaomba tupate masoko angalau mawili. Tuna Shule moja tu ya Sekondari, ambayo ina Wanafunzi 1250 na waalimu 2 wa somo la Biology, Waalimu 2 somo la Kiswahili ,waalimu 2-basic math, hatuna mwalimu wa fizikia. Wengi wa Waalimu wanaokuja hawakai. Wakazi wa Nyashimo walioamua kujenga Shule ya SekondariVenance Mabesho, ambapo tupo katika hatua za mwisho,tunaomba tupate angalau Mifuko 200 ya sementi kwani itasaidia sana katika ujenzi wa Uzio ili watoto wetu wasiliwe na wanyama. Tunaomba tuwekewe alama ya Pundamilia kwani Barabara yetu inakaosa alama hiyo na kwa kipindi cha kwa miaka watu wengi wamepoteza maisha.

Naye Mwenyekiti wa Kijiji-Paulo Makongoro, alisema moja ya changamoto kubwa inayowakabili wakazi wa Nyashimo ni Changamoto ya viboko ambao wana angamiza watu. Mkazi mwingine wa Nyashimo Bw. Marko Shonokwa alisema ''Tunahitaji kituo cha Polisi, Kwani na kituo cha Polisi kilichojengwa na wananchi kukamilika bado wananchi wanaenda Nyamikoma''. 

Kero nyingine  zilizoelezwa na wakazi hao ni  pamoja na  watu kuchukua mamlaka  mkononi na kumtoa madarakani kiongozi aliyeschaguliwa na wananchi. Leseni  ilitajwa kuwa ni changamoto  kwani wakienda kwingine wanakamwatwa kwanini wao wakija huku hawakamatwi.Vilevile ilielezwa kwamba  shamba la Kijiji  limechukuliwa na kumilikiwa na watu binafsi.

Akijibu hoja hizo Mhe. Mkuu wa Mkoa alisema  Eneo la Nyashimo wilaya ya Busega lina ukanda wenye ukubwa wa kilometa za mraba 200 ambazo zinafaa kutumika kwa shughuli ya uvuvi. Uvuvi wa kutumia vizimba ndio wenye tija zaidi mnavyo Vizimba 12, na nimesikia kuwa mnavuna tani 54.

Eneo la kilometa za mraba 200 linaweza  kutumika kutengeneza Vizimba zaidi ya 55,000 na hivyo kupata Samaki kiasi cha tani 250,000, hatimae kuwa vinara katika eneo la uvuvi nchini. Njia nyepesi ya kupata msaada ni kukaa katika vikundi na hivyo kuirahisishia Serikali kutoa msaada mkiwa katika vikundi.

Kuhusu suala la kodi na ushuru, Mkurugenzi na watu wako andaeni taarifa kamili ya aina mbalimbali za ushuru/tozo. Pongezi kwa ujenzi wa Shule, mahitaji yenu ni shule nne namnayo moja, hatua madhubuti zitachukuliwa ili kuona ni kwa jinsi gani tutatatua changamoto hiyo.

MWISHO












MKUU WA MKOA WA SIMIYU- MHE. DAVID KAFULILA AKUTANA NA WADAU WA NYUKI

Mhe. Kafulia amekutana na wadau wa ufugaji wa nyuki Mkoa wa Simiyu ambapo pamoja na mambo mengine alitaka kusikia changamoto zao na namna gani Mkoa unaweza kutatua changamoto hizo ili kuongeza tija ya uzalishaji wa asali

 Akizungumza Afisa Nyuki Mkoa, Bw.Maganga Juakali Ongala katika taarifa yake kwa Mhe. Kafulila alieleza  kuwa  Mkoa wa Simiyu una vikundi 91 vya ufugaji wa Nyuki.Katika  mwaka wa fedha 2019/2020 uzalishaji wa asali kwa Mkoa ulikuwa lita 31,788. Asali hiyo iliyovunwa kutoka Halmashauri zote Sita za Mkoa wa Simiyu, huku Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi ikiongoza kwa uzalishaji wa lita 8200.

Pamoja na mafanikio hayo wadau wa ufugaji wa Nyuki mkoani hapa wamekuwa wakikabiliana  na Changamoto mbalimbali kama vile, upatikanaji wa soko la asali hii ni ndani na nje ya  nchi.Ukosekanaji wa  mashine za kuchakata na kupaki asali na hivyo kuomba kukopeshwa vifaa hivyo. Changamoto katika kurina asali na utambuzi wa ukomavu wa Asali hivyo elimu inatakiwa kuwa endelevu kwa wazalishaji.

Aidha Wadau hao waliomba Wafugaji binafsi wa Nyuki wakopeshwe mizinga au vifaa vingine muhimu vya Ufugaji nyuki. Changamoto nyingine ni pamoja na Maeneo ya kufugia nyuki, baadhi ya wafugaji nyuki kuchoma mizinga kwa mfano Meatu eneo la Mwasengela kwa kuhofia kunyang'anywa maeneo yao.


Akijibu hoja hizo Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. David Kafulila alisema kuwa  ni vyema wafugaji kujiunga kwenye vikundi vya uzalishaji wa asali ili waweze kukopesheka.Ufugaji wa nyuki ni muhimu sana katika uchumi wa Taifa Letu.Vikundi 91 vilivyopo ni vichache sana hivyo basi, vikundi viongezwe ili watu wengi zaidi waweze kufikiwa.
Kwa muda nitakaokuwepo Simiyu nitapenda kuona umaskini wa watu unapungua kupitia shughuli muhimu Sana ya Ufugaji nyuki.Nipo tayari kushughulikia changamoto za ufugaji wa nyuki na uzalishaji wa asali.Lengo ni kuona kila mfugaji wa nyuki awe na uwezo  wa kutengeneza kipato cha  angalau Tshs.270,000/= kwa mwezi au mil.3 kwa mwaka.

Hivyo ninaelekeza uandaliwe, mkakati utakaoonesha ni vikundi vingapi vilivyopo na vitakavyoongezeka na hitaji la nyongeza ya mizinga au vifaa vingine muhimu ili kuwawezesha wanachama katika vikundi hivyo kutengeneza kipato cha Tshs.270,000/=  kwa mwezi kwa kila mwanachama.Maafisa Nyuki wa Wilaya kwa kushirikiana na Afisa Nyuki Mkoa waandae mkakati wa angalau watu 10,000 waweze kutengeneza kipato cha Tshs.270,000/= kwa mwezi. Mkakati huo uandaliwe kabla au ifikapo tarehe 18/6/2021.

Changamoto ya upatikanaji wa mizinga itafutiwe namna,Halmashauri kwa kushirikiana na wadau wengine wahusishwe katika upatikanaji wa mizinga hata kwa mkopo, vilevile kwa vifaa vyote vinavyohusiana na ufugaji na uvunaji wa mazao ya nyuki.WMA Makao waandae mkakati kwa ajili ya ufugaji wa nyuki kwa utekelezaji.








MWISHO

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!