Thursday, January 27, 2022

“Eleweni Changamoto za Wananchi katika Maeneo yenu, na Muwe Watatuzi”- RC KAFULILA











Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. David Kafulila ameyasema hayo wakati wa kikao kazi cha Watendaji wa Kata, Vijiji na Mitaa  wa Halmashauri ya Bariadi Mji na Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi kilichofanyika hivi karibuni.

Mhe.Kafulila ambaye alikuwa mgeni rasmi wakati wa kikao kazi hicho alisisitiza umuhimu wa Watendaji kupewa mafunzo ya mara kwa mara nje ya eneo la kazi pamoja na mafunzo kazini.

 “Kila Mtendaji kata,kijiji na mtaa lazima ajue Sheria ambayo imemfanya awepo kazini. Unapaswa kujua 'ABC' za uendeshaji ofisi. Lazima vikao vyote vya kisheria vifanyike, kuwe na ajenda za vikao na kumbukumbu za vikao hivyo.Lazima muwe na mpango kazi,hizo ndio zana za kazi.Lazima upange kazi zako na uje wiki ijayo utashughulikia nini? Mkiwa viongozi mnapaswa kuelewa changamoto zinazowakabili wananchi wa kwenye maeneo yenu,na kuwa watatuzi wa changamoto hizo.".Ameeleza Kafulila. 

Akielezea agenda nne za Mkoa wa Simiyu na Wilaya zake.Mhe. Kafulila amezitaja ajenda hizo kuwa ni makusanyo, kilimo, ukame/chakula na upandaji miti. 

Akizungumzia agenda namba moja ambayo ni Makusanyo, Mhe. Kafulila amewataka Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi kushindanisha Vijiji kwa asilimia za makusanyo na mashindano hayo yafanyike kila robo mwaka na hatimae kuzitambua halmashauri zilizofanya vizuri aidha kwa kuwapa vyeti au barua ya Pongezi. Hili lifanyike katika Halmashauri zote. Kila Halmashauri iwe na lengo la makusanyo. 

Kuhusu kilimo,Mhe. Kafulila amewataka wakuu hao kujipanga na killimo  cha alizeti. "Matumaini yetu ni kuzalisha alizeti tani 200,000-250,000 ikilinganishwa na tani 81,000 ambazo zilizalishwa Mwaka Jana. Suala la kilimo cha  Pamba na Alizeti linatakiwa kuwa agenda ya eneo lako.Kila kitongoji ni vyema kuwa na majina ya wakulima na kujua  wamelima nini kama ni alizeti au pamba".Amesisitiza Kafulila.

Aidha ili kukabiliana na changamoto ya chakula kutokana na ukame ambao umesababisha bei za chakula kuwa juu,Mhe. Kafulila amewaelekeza Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi kuwahamasisha na kuwaelimisha wananchi wao juu ya umuhimu wa kilimo cha mazao ya chakula ambayo hayahitaji mvua nyingi. "Nimeshaongea Mamlaka ya kilimo Morogoro, baaada ya kutoa Pamba shambani itabiidi wakulima walime dengu.Mamlaka ya kilimo itatoa mbegu, zana na pembejeo za kuwawezesha ili waweze kishiriki kilimo bora.

Akizungumzia ajenda ya tatu, Mhe.Kafulila ameitaja ajenda hiyo kuwa upandaji wa miti. Simiyu ni miongoni mwa  mikoa 5 Tanzania Bara inayoongoza kwa ukataji wa miti, hivyo ili kuepukana na janga la jangwa ni vyema kila kijiji  kiwe na agenda ya upandaji wa miti. Akitaja ajenda namba nne, Mhe.Kafulila ameitaja ajenda hiyo kuwa ni  Elimu," fuatilieni na kusimamia kikamilifu agenda ya Elimu. Wiki ijayo tutakutana kuzungumzia kwa kina kuhusu matokeo.Watendaji wa kata na vijijini wekeni macho yenu kwenye suala la Elimu."Amesisitiza Kafulila.

Mhe. Kafulila amewapongeza watendaji wa kata, vijiji, mitaa, mkuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri hizo mbili kwa uchapakazi. Aidha amewahakikishia wakuu hao imani kubwa aliyonayo kwao ya kwamba wana uwezo mkubwa wa kufanya mambo mengi makubwa zaidi wakiamua."Mnachohitaji ni kuwatambua watu wa chini kwa kazi nzuri wanazofanya.Wapeni hata barua au cheti cha kuwapongeza. Maeneo yote wanayofanikiwa wapeni moyo na wanapokosea wachukulieni hatua kali.Wanaofanya vizuri wapeni hamasa kubwa.Uwezo wa kubadilisha vijiji, Wilaya, upo mkononi mwetu.”

Akizungumzia kusudi la kikao kazi hicho, Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Mhe. Lupakisyo Kapange ameeleza nia ya kikao kazi hicho ni  kujengeana uwezo na kuzindua kauli mbiu ya Halmshauri ya Bariadi Mji na  Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi isemayo: "Serikali mlangoni Mwako". Mwisho.

Tuesday, January 25, 2022

WAKURUGENZI, WAKUU WA WILAYA ELIMISHENI WANANCHI KUHUSU FURSA MBALIMBALI ZA MIKOPO - RC KAFULILA.





Picha ya Pamoja kuanzia kushoto Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bariadi Mji, Meneja wa NMB Bariadi,Mkuu wa wilaya ya Bariadi na Mkurugenzi wa Halmshauri ya Bariadi Mji wakiwa wameshika hundi ya mfano kutoka benki ya NMB

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bariadi Mji Bw. David Masanja ( Kushoto) akimkabidhi hundi ya Mfano Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe David Kafulia (Kulia), ikiwa na kiasi cha fedha kitakachokopeshwa kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Halmashauri ya Bariadi Mji

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. David Kafulila (kulia)  akikabiidhi hundi ya Mfano kwa wawakilishi wa makundi  ya wanawake, Vijana na watu wenye ulemavu. 
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. David Kafulila (Kulia) akiteta jambo pamoja na mkuu wa Wilaya ya Bariadi Mhe.Lupakisyo Kapange wakati wa tafrija hiyo.


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. David Kafulila akizungumza na washiriki wa tafrija hiyo leo katika ukumbi wa Bariadi  Conference -Bariadi Simiyu






Makundi mbalimbali ya washiriki kwenye hafla hiyo.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. David Kafulila,ameyasema hayo leo, wakati wa hafla ya utoaji mikopo kwa vikundi vya wajasiriamali vilivyopo katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi. Akizungumza, Mhe.Kafulila ameeleza lengo la Serikali katika utoaji wa mikopo ya aina hiyo ni kuwawezesha wananchi  wasiokidhi vigezo vya kukopeshwa na benki, kujikwamua kiuchumi kwa kuwapa fursa mbalimbali yakiwemo makundi ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, kwa kuwapatia mikopo ya fedha za asilimia 10 ya mapato ya ndani yaliyokusanywa na halmashauri za miji. 

 Fedha hizo hutokana na tozo na ushuru mbalimbali ambao hukusanywa na kuwekwa pamoja hatimaye 10% yake kutolewa kama mikopo kwa makundi maalum. "Fedha hizo ni mikopo na sio msaada, hivyo mnawajibika kuzirejesha kwa wakati ili ziweze kukopeshwa kwa vikundi vingine, vitakavyokidhi vigezo. Nawaasa mjitahidi kuhakikisha mnatekekeleza miradi mliyoianzisha kwa ufanisi na kurejesha fedha mlizokopeshwa kama sheria, kanuni, taratibu na miongozo inavyowataka". Amesema Kafulila. 

Mhe.Kafulila leo, amepokea hundi ya mfano kutoka benki ya NMB, hundi ambayo amekabidhiwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Bariadi Mji, Bw. Adrian Jungu wakiwa pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Mhe. Lupakisyo Kapange pamoja na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bariadi Mji Bw.David Masanja, hundi  yenye thamani ya Tsh. 256,090,000/-, fedha ambazo zitakopeshwa kwa jumla ya vikundi 53 vyenye wanufaika 364 ikiwa ni  awamu ya kwanza katika mwaka wa fedha 2021/2022. 

Fedha hizo zitagawanywa kwa makundi maalum yenye mchanganuo ufuatao, wanawake vikunndi 37 watakopeshwa kiasi cha Tsh.180,100,000/-, vijana vikundi 11 vitakopeshwa Tsh. 49,420,000/- na watu wenye ulemavu vikundi 5 watakopeshwa Tsh. 26,570,000/-.

Akizungumzia changamoto wanazokabiliana nazo katika utoaji wa mikopo ya 10%,Mkurugenzi wa Halmashauri ya Bariadi Mji. Bw. Adrian Jungu, amezitaja changamoto hizo kuwa, mapato ya ndani kuwa madogo ikilinganishwa na mahitaji ya makundi maalum ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu ambao wanaotakiwa kukopeshwa, baadhi ya vikundi kukosa uaminifu katika kurejesha mikopo, baadhi ya vikundi kubadilisha matumizi ya fedha walizokopeshwa kulingana na miradi waliyoombea mikopo, badala yake kugawana fedha au kuanzisha miradi mipya ambayo hawana uzoefu nayo na hivyo kushindwa kurejesha mikopo hiyo.

 Aidha Bw. Jungu ameeleza mikakati mbalimbali ambayo Halmashauri ya Bariadi Mji imejipanga kufanya ili kukabiliana na changamoto hizo ikiwa ni pamoja na kuendelea kubuni vyanzo vipya vya mapato ili kuongeza mapato ya ndani, kuboresha mbinu za ukusanyaji mapato kwenye vyanzo vilivyopo,kuendelea kutoa elimu kwa vikundi ili viiweze kuzingatia taratibu na miongozo iliyowekwa na kufuatilia marejesho ikiwa ni pamoja na kuwafikisha mahakamani wadaiwa sugu. Hadi sasa, mashauri 6 ya madai yamefunguliwa mahakamani na tayari vikundi 2 kati ya 6 vilivyoshtakiwa vimelipa na kumaliza deni walikokuwa wanadaiwa.Halmashuri ya Bariadi Mji inadai kiasi cha Tsh. 35,057,450/- kutoka kwenye vikundi 15. 

 Ili kuhakikisha ufanisi katika utoaji wa mikopo hiyo Mhe Kafulila amewaagiza wakurugenzi wote wa halmashauri na wakuu wote wa wilaya za Mkoa wa Simiyu kuwahamasisha na kuwaelimisha wananchi ili waelewe na waitumie fursa hiyo kwani kuna watu wengi ambao hawajui kuhusu fursa hizo. Kuna benki ambazo zinatoa mikopo kwa riba ndogo hivyo ni vyema kwa vikundi ambavyo vimekidhi vigezo vikatumia fursa hiyo na kukopa  kutoka kwenye benki hizo.

Mhe. Kafulila amewataka wakuu hao wote kutumia zoezi la upandaji miti kama kigezo kimojawapo cha kupata mkopo. Wanakikundi wanatakiwa wapande miti ama ya kivuli ama ya Matunda na kuonyesha eneo walilopanda miti hiyo kisha ndio wapewe mkopo, hii itaharakisha na kurahisiha sana Simiyu ya Kijani. 

 Aidha Mhe Kafulila amewataka viongozi hao kujua watu wao wanajishughulisha na nini. "Jengeni dhana pana ya uelewa juu ya shughuli mbalimbali wanazofanya wananchi wa eneo lenu.Maafisa biashara wote ni jukumu lenu kuvijua vikundi vyote vinavyohusika na Mikopo.Maafisa biashara wote ni lazima muwe walezi wa vikundi hivi".Amesisitiza Kafulila. Mwisho.

Friday, January 14, 2022

RC- Kafulila Atembelea na Kutoa pole Kwa Familia za Wafiwa Wilayani Busega

 Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe.David Kafulila akiwa ameambatana na Mkuu wa Wilaya ya Busega Mhe.Gabriel Zakaria,Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyu ACP Bracius Chatanda na OCD wa Busega,leo wamewatembelea na kuwapa pole familia ambazo zilipoteza ndugu zao,kwenye ajali iliyotokea 11/1/2022 katika Kijiji cha Kalemela, Wilayani Busega na kusababisha vifo vya watu 15 kufikia leo.

Wakazi wa kijiji cha Kalemela pamoja na maeneo ya jirani wamepoteza watu 9 na kufanya Mkoa wa Simiyu kupoteza watu 9 kupitia ajali hiyo.

 Aidha Mhe.Kafulila ametumia fursa hiyo  kuwapatia wakazi hao Salaam za pole toka kwa Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan na pamoja na ubani kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Mwisho.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Daavid Kafulila akiwa ameambatana ma Mkuu wa Wilaya ya Busega Mhe. Gabriel Zakaria wakitembelea na kutoa pole kwa familia ambazo  zimepoteza ndugu zaokutoka na aksidenti iliyotokea 11/1/2022 Wilayani Busega na kusababisha vifo vya watu 15 kufikia 13/1/2022/

Mhe. Kafulila akitoa neno la faraja kwa Wafiwa 



Ndugu,jamaa na marafiki wa wafiwa 

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. David Kafulila, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyi ACP. Bracius Chatanda pamoja na OCD Busega wakiwafariji ndu za marehemu


Ndugu, jamaa, marafiki na majirani wa Wafiwa

Mkuu wa Wilaya ya Busega Mhe. Gabriel Zakaria akizungumza na kutoa pole kabla ya kumkaribisha mkuu wa Mkoa wa Simiyu


Mhe. Kafulila akitoa mkono wa pole kwa Wafiwa

Mhe Kafulila akitoa neno la faraja kwa wafiwa 



Mhe. Kafulila akitoa mkono wa pole kwa Wafiwa 

Mhe.Kafulila akiagana na wafiwa


Mkoa wa Simiyu Wafanya Kongamano la Maombi, Kuuombea Mkoa!

Kongamano la kuuombea Mkoa wa Simiyu limefanyika hivi karibuni kuuombea Mkoa, ili uweze kuepukana na Majanga mbalimbali kama vile Ukame, Magojwa, Misiba na ajali.Kongamano hilo la maombi limefanyika katika Viwanja vya Halmashauri ya Mji Bariadi. 

 Akizungumza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. David Kafulila amesema ili kupata mafanikio yoyote yale duniani ni lazima kumtanguliza Mungu, sababu ya uzito wa jina lake kwenye hatma yetu,kwani yapo mahubiri ambayo mwenyezi mungu anayahubiri katika maisha yetu kwa vitendo.Upo uwezekano wa sisi kupata neema kwa sababu ya wachache walio na Mungu au kupata matatizo kutokana na wenzetu wachache tulionao.katika kusisitiza hilo Mhe Kafulila alitoa mfano wa Abraham wa kwenye masimulizi ya biblia ambaye alimuomba mwenyezi Mungu na kumsihi zaidi ya mara tatu asiliangamize jiji la Sodoma na Gomora naye Mungu alisikiliza sihi na maombi ya Abrahamun zaidi ya mara tatu. 
 Mhe. Kafulila aliendelea kutoa mfano wa  Yona ambaye kwa kukimbia jukumu alilopewa na Mwenyezi Mungu la kwenda kuwahubiria watu wa Ninanwi alisababisha balaa nadani ya  chombo na bahari kuchafuka kiasi cha kwamba chombo kilitaka kuzama, Wakati hali hii inatokea kila mtu alliyekuwa ndani ya chombo alisali kwa Mungu wake na baada ya Yona kutupwa baharini na kumezwa na samaki chombo kilitulia na kisha Yona kutapikwa katika jiji la Tarshishi.Yote haya yaonyesha kwamba hata tuwe katika hali gani wa kumtegemea ni Mwenyezi mungu nmaye  husikia sala za watu wake.

 Mhe. Kafulila ameeleza kuwa tangu ateuliwe kuwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, majanga yamekuwa yakitokea mara kwa mara mkoani humo hususani vifo vya viongozi mbalimbali na hata kifo cha msaidizi wake wa karibu,aidha magonjwa, ukame na aksidenti za barabarani kutia ndani ajali iliyotokea 11/1/2022 ambayo ilisababisha vifo vya watu 15 kufikia leo, ni majanga ambayo yameupata mkoa wetu kwa kipindi kifupi cha wakati

."Hivyo nimeona ni vyema sisi sote kwa umoja wetu bila kujali dini wala itikadi tukutane kwa pamoja na kumsihi Mwenyezi Mungu kupitia haya maombi maalum atuepushe na majanga haya yote pamoja na kushukuru kwa baraka ambazo tayari ametupatia". Amesema Kafulila.

 Kongamamo hilo limeshirikisha viongozi wa Dini zote mkoani Simiyu, wananchi na wanakwaya kutoka katika dini zote.Katika kongamano hilo kwaya mbalimbali zilitumbuiza zikiwa na ujumbe wa kumsihi Mwenyezi Mungu atuepushe na majanga yote na kumshukuru kwa baraka ambazo ameupatia Mkoa wa Simiyu.Pamoja na kuuombea mkoa wa Simiyu,viongozi wa dini walimuombea Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan na kumshukuru kwa vipaumbele ambavyo amevipa Mkoa wa Simiyu.

Viongozi wa Dini walisisitiza Amani, Umoja na Upendo pamoja na tabia ya  kumtegemea Mwenyezi Mungu kwani Mungu asipoijenga Nyumba waijengao wafanya kazi bure. Aidha Viongozi hao walisisitiza pamoja na kuwa na dini mbalimbali cha muhimu ni upendo ambapo tukiwa na upendo ni rahisi kuvumiliana na hivyo kutokeza amani. 

Kila Kiongozi wa Dini alipewa eneo la kuliombea ikiwa pamoja na amani na upendo, magonjwa, ukame, ajali na ustawi wa viongozi.

 "Aidha niwashukuru viongozi wote wa dini kwa jinsi mlivyojipanga na kuongoza maombi haya sina cha kuwalipa zaidi niseme ahsanteni sana.Pamoja na kuwashukuru Viongozi wa dini zote,pia niwashukuru Wanakwaya ambao nanyi ni sehemu ya dini kwani kwa nyimbo zenu mmetoa mahubiri tosha".Amesisitiza Kafulila.

Mwisho.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. David Kafulila akitoa neno la shukrani kwa Viongozi wa dini zote Mkoani Simiyu mara baada ya kongamano la kuuombe Mkoa wa Simiyu.

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!