Friday, January 14, 2022

RC- Kafulila Atembelea na Kutoa pole Kwa Familia za Wafiwa Wilayani Busega

 Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe.David Kafulila akiwa ameambatana na Mkuu wa Wilaya ya Busega Mhe.Gabriel Zakaria,Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyu ACP Bracius Chatanda na OCD wa Busega,leo wamewatembelea na kuwapa pole familia ambazo zilipoteza ndugu zao,kwenye ajali iliyotokea 11/1/2022 katika Kijiji cha Kalemela, Wilayani Busega na kusababisha vifo vya watu 15 kufikia leo.

Wakazi wa kijiji cha Kalemela pamoja na maeneo ya jirani wamepoteza watu 9 na kufanya Mkoa wa Simiyu kupoteza watu 9 kupitia ajali hiyo.

 Aidha Mhe.Kafulila ametumia fursa hiyo  kuwapatia wakazi hao Salaam za pole toka kwa Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan na pamoja na ubani kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Mwisho.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Daavid Kafulila akiwa ameambatana ma Mkuu wa Wilaya ya Busega Mhe. Gabriel Zakaria wakitembelea na kutoa pole kwa familia ambazo  zimepoteza ndugu zaokutoka na aksidenti iliyotokea 11/1/2022 Wilayani Busega na kusababisha vifo vya watu 15 kufikia 13/1/2022/

Mhe. Kafulila akitoa neno la faraja kwa Wafiwa 



Ndugu,jamaa na marafiki wa wafiwa 

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. David Kafulila, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyi ACP. Bracius Chatanda pamoja na OCD Busega wakiwafariji ndu za marehemu


Ndugu, jamaa, marafiki na majirani wa Wafiwa

Mkuu wa Wilaya ya Busega Mhe. Gabriel Zakaria akizungumza na kutoa pole kabla ya kumkaribisha mkuu wa Mkoa wa Simiyu


Mhe. Kafulila akitoa mkono wa pole kwa Wafiwa

Mhe Kafulila akitoa neno la faraja kwa wafiwa 



Mhe. Kafulila akitoa mkono wa pole kwa Wafiwa 

Mhe.Kafulila akiagana na wafiwa


0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!