Thursday, March 10, 2022

Katika kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani, TUGHE-Simiyu Yatoa Msaada Kituo cha Afya Ikindilo.


























Sherehe ya siku wa Wanawake duniani, huadhimishwa kila tarehe nane ya mwezi wa tatu. Katika kuadhimisha sherehe hizo, 2022, kama ilivyo ada Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya (TUGHE-Simiyu), waliamua kufanya matendo ya huruma Wilayani Itilima ambapo ndipo sherehe za siku ya mwanamke kimkoa zimefanyika.

Akiwakaribisha wilayani Itilima Mkurugenzi wa Wilaya ya Itilima, Bi. Elizabeth Gumbo amesema ‘’ninafuraha kubwa niwakaribishe sana Wilaya ya Itilima, Pongezi sana  Kwa Mwenyekiti na katibu wa TUGHE Bi. Elizabeth na  Catherine. Niwaombee baraka za mwenyezi Mungu,niwatie moyo wanawake wenzangu,sisi tunaweza, na tumejionea wazi kabisa kutoka kwa Mama yetu, Rais wetu ambaye ni mwanamama Mhe. Samia Suluhu Hassan, kwani, kwa Wilaya ya  Itilima tu ametupatia fedha ambazo zimewezesha ujenzi wa vyumba 82 vya madarasa. Hivyo wakina mama sote tuwe na moyo wa kumuunga mkono Rais wetu mama Samia Suluhu Hassan, tupambane wenyewe, kila mmoja katika nafasi aliyopewa akaonyeshe uwezo wake. Wakina mama tuendelee kuwashauri kina mama wengine, binti zetu, familia, watoto na Taifa letu, kwani wakina mama ni jeshi kubwa’’.

Akielezea sababu za TUGHE-Simiyu, kuchagua eneo hilo na kufanya matendo ya huruma, Mwenyekiti kamati za Wanawake TUGHE Mkoa wa Simiyu,Bi.Elizabeth Nangali Gelege   amesema “ tumeamua kufanya haya matendo ya huruma katika kituo cha afya cha Ikindilo baada ya kufahamishwa na Mganga Mkuu wilaya ya Itilima Dkt. Anorld Musiba, kuwa kituo cha afya Ikindilo kina mahitaji. Tumekuja na mashuka, mama Samia Suluhu Hassan  ameleta  majengo, sisi tumeleta sabuni pamoja na mashuka vyote vikiwa na thamani ya Tsh. Milioni moja. 

Akizungumzia kauli mbiu ya mwaka huu ya siku ya wanawake duniani, ambayo inasema:“Kizazi cha Haki na Usawa Kwa Maendeleo, Tujitokeze Kuhesabiwa’’. Bi. Geleje amesema Kauli mbiu hii inaonyesha wazi kwamba huu ni mwaka wa sensa, hivyo wanawake tujitokeze kuhesabiwa.Kila mwanamke atumie kipaji chake kuhakikisha watu wa familia yake wanahesabiwa na kuendeleza nchi.

Akizungumzia msaada huo Katibu wa TUGHE Mkoa wa Simiyu Bi.Catherine Nyingi amesema katika kuonyesha mshikamano,sisi TUGHE tuna kawaida ya kufanya matendo ya huruma na kurudisha huduma katika jamii.Kama ambavyo tumefanya leo katika kituo hiki cha afya cha Ikindilo.

Akitoa taarifa kuhusu kituo cha afya Ikindilo, Mganga mfawidhi Kituo cha afya Ikindilo Dkt. Elizabeth Malunde amesema Kituo cha afya Ikindilo  ni kimoja kati ya vituo 3 vya afya Wilayani itilima. Kituo hiki kimepanda kutoka daraja namba mbili na sasa kipo namba tatu. 

Kituo cha afya Ikindilo kinatoa huduma mbalimbali kama vile chanjo cha UVIKO,Kliniki ya HIV, tuanafanya tohara kwa watoto wa kiume, tunahudumia wangonjwa wa nje na ndani, poa tunatoa huduma za mama na mtoto. Mwaka jana mwezi wa saba tulifungiwa mfumo wa GhoTomis, hivyo malipo yoye ya huduma za afya yanafanyika kwa kutumia mfumo. Upatikanaji wa Dawa ni  100%, upatikanaji wa damu 100% pia tuna duka la Dawa. 

Pamoja na mafaniko tajwa hapo juu bado tunakabiliwa na  mbalimbali.Changamoto kubwa tuliyo nayo ni kuwa hatuna eneo ila tupo kwenye mchakato wa kutafuta eneo . Pia tuna changamoto ya nyumba za watumishi kwani tuna Nyumba 6 tu na hivyo kufanya watumishi wengine kuishi katika maeneo ya mbali, uchakavu wa majengo, tuna changamoto ya jengo la kulaza wagonjwa- OPD, Changamoto ya watumishi, kituo hakina uzio na hivyo kufanya wanyama kuingia  ndani ya eneo la kituo cha afya,pia hatuna wodi ya kulaza watoto wachanga.Mwisho.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!