Friday, July 14, 2017

VIJIJI 347 KUPATA UMEME WA REA AWAMU YA TATU MKOANI SIMIYU

Jumla ya Vijiji 347 Mkoani Simiyu vinatarajia kupata Umeme kupitia Mradi wa Umeme Vijijini (REA) awamu ya Tatu ambao utatekelezwa katika kipindi cha miezi 24 kuanzia mwezi Julai 2017.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Mhe.Dkt.Medard Kalemani wakati wa Uzinduzi wa Mradi wa Umeme Vijijini (REA) Awamu ya Tatu na utambulisho wa Mkandarasi wa mradi katika Kijiji cha Nangale, Kata ya Ndolelezi Wilaya ya Itilima Mkoani Simiyu.

“Mradi wa REA awamu ya tatu utapeleka Umeme katika vijiji vyote vya Mkoa wa Simiyu hilo la kwanza, pili mradi huu utapeleka Umeme katika vitongoji vyote hata vijiji ambavyo vilipelekewa Umeme lakini baadhi ya vitongoji vyake bado havina, katika awamu hii navyo vinapelekewa” amesema Kalemani. 

Ameongeza kuwa Umeme wa REA awamu ya tatu pamoja na kuwanufaisha wananchi katika makazi yao kwenye vijiji vyote 347 vilivyosalia pia utapelekwa katika Taasisi za Umma zikiwepo shule, vituo vya kutolea huduma za afya, visima na mitambo ya miradi ya maji pamoja na nyumba za ibada( makanisa na misikiti).

Aidha, Dkt.Kalemani amewataka wananchi wa Mkoa wa Simiyu kuutumia umeme huo kibiashara hususani katika shughuli za uzalishaji ambazo zitawaongezea kipato badala ya kuutumia kwa ajili ya kuwasha taa majumbani tu.

Ameupongeza uongozi wa Mkoa wa Simyu  kwa kasi nzuri ya utekelezaji wa Sera ya Viwanda ambapo amebainisha kuwa utekelezaji wa Mradi wa Umeme Vijijini (REA) awamu ya Tatu mkoani humo utasaidia kuwezesha shughuli za viwanda kufanyika vizuri hali itakayowawezesha wananchi kukuza uchumi kwa kuwa mazao yao yataongezewa thamani kupitia viwanda hivyo.

Wakati huo huo Dkt.Kalemani amesema Serikali ina mkakati wa kujenga vituo viwili vya kupozea umeme Mkoani Simiyu, ambapo kimoja kitajengwa Mjini Bariadi na kingine katika Mji wa Lalago wilayani Maswa na kuwahakikishia wananchi kuwa mkoa huo utapata umeme wa kutosha ambao utatumika pia katika viwanda.

Akimkabidhi Mkandarasi wa Mradi wa REA Awamu ya Tatu ambaye ni Kampuni ya JV White City International kwa Wananchi wa Mkoa wa Simiyu, Dkt.Kalemani amemtaka  kuhakisha kuwa anatekeleza mradi  ndani ya muda uliopangwa (miezi 24), akiwatumia wakandarasi wasaidizi wenye sifa kutoka ndani ya mkoa na kuwapa ujira wao kama inavyotakiwa pamoja na  kununua vifaa vyote zikiwemo nguzo na transifoma hapa nchini.

Amemtaka Meneja wa TANESCO Mkoa wa Simiyu, Mhandisi Rehema Mashinji kusimamia na kuhakikisha kuwa wakandarasi watakaowaunganishia wananchi Umeme ni wale walioidhinishwa na shirika hilo ili kuepuka Vishoka ambao watawaongezea wananchi gharama zisizo za lazima.

Amesema Serikali ina mpango wa kujenga Ofisi za TANESCO kila Wilaya na kuweka vituo vya kuhudumia wateja katika kila kata na tarafa ambapo yataanzishwa madawati ya huduma kwa wateja.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka ameomba Shirika la Umeme TANESCO  kuona namna ya kuweka nguvu katika Mkoa huo ili ujitosheleze kwa umeme wa uhakika kuwezesha utekelezaji wa miradi ya viwanda inayoendelea kutekelezwa chini ya Kauli Mbiu ya Mkoa ya “Wilaya Moja Bidhaa Moja Kiwanda Kimoja”

Mtaka ameongeza kuwa Mkoa huo umejipanga kufanya mapinduzi kupitia teknolojia ambapo utatengeneza mpango mkakati wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (ICT Strategy),kujenga  ICT Hub ya mkoa na vituo vya mawasiliano katika baadhi ya shule, ili wanafunzi wa madarasa ya mitihani waweze kupata unafuu wa kufundishwa kupitia teknolojia hususani kwenye masomo ya sayansi, hivyo akasisitiza umeme kupelekwa katika shule na Taasisi nyingine za Umma.

Naye Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Simiyu kupitia CCM, Mhe.Leah Komanya ametoa Rai kwa TANESCO kuhakikisha wanatoa elimu kwa wananchi ili wajue taratibu zote za kuunganishiwa umeme ikiwa ni pamoja kufahamu gharama ambayo ni shilingi elfu 27,000/= ili wasidanganywe na kutumia gharama kubwa kinyume na mpango wa Serikali.

Akizungumza mara baada ya uzinduzi wa mradi huo Mkazi wa Kijiji cha Nangale Bw.Mathias Mabula Mageni ameishukuru Serikali kuwafikishia umeme kupitia REA ambapo amesema utawasaidia katika kukuza uchumi kwa kuwa watautumia katika shughuli mbalimbali zitakazowaingizia kipato kama vile kuchomelea vyuma, kuanzisha mashine za kusaga na kukoboa nafaka, kuanzisha saluni za kike na za kiume pamoja na viwanda vidogo.


Mradi wa Umeme Vijijini (REA) Awamu ya Tatu Mkoani Simiyu unatekelezwa na Mkandarasi JV White City International Contractors  ambalo ni Kampuni ya Kitanzania kwa kushirikiana na Guangdong Jianneng Electronic Power Engineering Co. Ltd.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Mhe.Dkt.Medard Kalemani akizindua Mradi wa Umeme Vijijini (REA)Awamu ya Tatu Mkoani Simiyu katika Kijiji cha Nangale wilayani Itilima (kushoto) Mkuu wa mkoa huo, Mhe.Anthony Mtaka.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Mhe.Dkt.Medard Kalemani (mwenye suti nyeusi katikati) akikata utepe kabla ya kuzindua Mradi wa Umeme Vijijini (REA) Awamu ya Tatu Mkoani Simiyu katika Kijiji cha Nangale wilaya ya Itilima
 Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Mhe.Dkt.Medard Kalemani akizungumza na wannachi wa Wilaya ya Itilima wakati wa Uzinduzi waMradi wa Umeme Vijijini (REA) Awamu ya Tatu  Mkoani Simiyu uliofanyika  katika Kijiji cha Nangale wilaya ya Itilima.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Mhe.Medard Kalemani akiwaonesha wananchi Kifaa kiitwacho UMETA(Umeme Tayari) ambacho hutumika kuleta nishati ya umeme katika nyumba ambazo haziwezi husukwa nyaya wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Umeme Vijijini (REA) Awamu ya Tatu  Mkoani Simiyu katika Kijiji cha Nangale wilaya ya Itilima
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu akitoa salamu za Mkoa wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Umeme Vijijini (REA)Awamu ya Tatu katika Kijiji cha Nangale wilaya ya Itilima Mkoani humo.
 Mbunge wa Viti Maalum  Mkoa wa Simiyu kupitia CCM, Mhe.Esther Midimu akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Itilima wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Umeme Vijijini (REA) Awamu ya Tatu katika Kijiji cha Nangale wilaya ya Itilima Mkoani Simiyu.
Mbunge wa Itilima, Mhe.Njalu Silanga akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Itilima wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Umeme Vijijini (REA) Awamu ya Tatu  Mkoani Simiyu uliofanyika katika Kijiji cha Nangale wilayani Itilima.
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Simiyu kupitia CCM, Mhe.Leah Komanya akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Itilima wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Umeme Vijijini (REA)Awamu ya Tatu  Mkoani Simiyu uliofanyika katika Kijiji cha Nangale wilaya ya Itilima.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Mhe.Dkt.Medard Kalemani( wa tatu kulia) akicheza wimbo maalum wa Kisukuma pamoja na viongozi wa mkoa wa Simiyu wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Umeme Vijijini (REA)Awamu ya Tatu Mkoani Simiyu uliofanyika katika Kijiji cha Nangale wilaya ya Itilima.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Mhe.Dkt. Medard Kalemani( wa tatu kushoto) akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu(kushoto) na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Dkt.Titus Kamani wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Umeme Vijijini (REA)Awamu ya Tatu Mkoani Simiyu katika Kijiji cha Nangale wilaya ya Itilima.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Mhe.Dkt.Medard Kalemani( wa pili kulia) pamoja na baadhi ya viongozi wa mkoa wa Simiyu wakicheza kuelekea kuwatuza wasanii waliokuwa wakitoa burudani (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Umeme Vijijini (REA)Awamu ya Tatu Mkoani Simiyu uliofanyika katika Kijiji cha Nangale wilaya ya Itilima.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mh.Anthony Mtaka (kushoto) akiteta jambo na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Mhe.Dkt.Medard Kalemani wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Umeme Vijijini (REA)Awamu ya Tatu Mkoani Simiyu uliofanyika katika Kijiji cha Nangale wilaya ya Itilima.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Dkt.Titus Kamani akizungumza na wananchi wa Itilima wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Umeme Vijijini (REA)Awamu ya Tatu Mkoani Simiyu uliofanyika katika Kijiji cha Nangale wilaya ya Itilima.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka akiteta jambo na Mbunge wa Itilima Mhe.Njalu Silanga wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Umeme Vijijini (REA)Awamu ya Tatu Mkoani Simiyu uliofamyika katika Kijiji cha Nangale wilaya ya Itilima, (kushoto) ni Mbunge wa Maswa Magharibi, Mhe.Mashimba Ndaki.
Mmoja wa Wazee 10 waliopewa kifaa cha Umeme kiitwacho UMETA katika Kata ya Ndolelezi Wilayani Itilima na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Mhe.Dkt.Medard Kalemani akitoa shukrani wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Umeme Vijijini (REA)Awamu ya Tatu Mkoani Simiyu uliofanyika katika Kijiji cha Nangale wilaya ya Itilima.
Baadhi ya wananchi wa Wilaya ya Itilima wakimsikiliza Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Mhe.Dkt.Medard Kalemani(hayupo pichani) wakati wa wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Umeme Vijijini (REA)Awamu ya Tatu Mkoani Simiyu katika Kijiji cha Nangale wilaya ya Itilima.
Kikundi cha Kwaya kutoka wilayani Itilima wakitumbuiza wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Umeme Vijijini (REA)Awamu ya Tatu Mkoani Simiyu katika Kijiji cha Nangale wilaya ya Itilima.
Msanii Elizabeth Maliganya (mwenye kipaza sauti katikati) akicheza wimbo wa Kisukuma na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Mhe.Dkt.Medard Kalemani(kushoto) pamoja na viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Simiyu kufurahia uzinduzi wa Mradi wa Umeme Vijijini (REA)Awamu ya Tatu Mkoani humo katika kijiji cha Nangale wilaya ya Itilima.


0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!