Friday, July 7, 2017

WANAFUNZI WA SEKONDARI WAHIMIZWA KUSOMA MASOMO YA SAYANSI

Wanafunzi wa shule za sekondari wilayani Bariadi mkoani Simiyu wamehimizwa kusoma masomo ya sayansi ili kuendana na azma ya Serikali ya awamu ya tano ya Uchumi wa Viwanda kama inavyoelezwa pia katika Ujumbe wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu.

Hayo yamesemwa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Amour Hamad Amour wakati wa uzinduzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo wilayani BARIADI.

Amour amesema Serikali imejenga maabara  na kuweka vifaa katika shule mbalimbali za sekondari kwa lengo la kuwezesha wanafunzi kujifunza masomo ya sayansi kwa vitendo ili kuwaandaa kuwa wataalam katika maeneo tofauti.

Amewataka wanafunzi kusoma kwa bidii na kuzitumia vizuri maabara zilizopo ili wapate ujuzi wa nadharia na vitendo utakaowaandaa kuwa wabobezi kwenye maeneo mbalimbali yanayohitaji utalaam wa kisayansi.

“, nahimiza huduma nzuri za maabara vijana hawa waweze kusoma masomo ya kemia, fizikia, bailojia na hisabati ili waende sawa na Kauli mbiu ya Mwenge wa Uhuru mwaka huu ya “Shiriki katika Kukuza Uchumi wa Viwanda kwa Maendeleo ya Nchi yetu” wakashike nafasi mbalimbali wawe wakemia, wahandisi katika viwanda, wawe madaktari na nafasi nyingine nyingi" amesema Amour

Akizungumzia mapambano dhidi ya dawa za kulevya amewataka wananchi kushirikiana na Serikali katika kuziba mianya yote na kutokomeza shughuli za uuzaji na usambazaji wa dawa za kulevya na wasisite kutoa taarifa katika vyombo vya dola wanapobaini watu wanaofanya shughuli hizo ili wachukuliwe hatua..

Aidha, akizungumza na wananchi katika maeneo mbalimbali ambayo Mwenge wa Uhuru umeweka mawe ya msingi, kufungua na kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo, Ndg.Amour amewapongeza na kuwataka wananchi kuendelea kuchangia miradi hiyo na kutokubaliana na viongozi wanaowashawishi kuacha kuchangia maendeleo yao.

“ Kila mradi tuliopita taarifa inaonesha kuna nguvu ya wananchi, nawapongeza sana kwa kushirikiana na Serikali kutekeleza miradi ya elimu, afya, maji na mingine mingi,nawasihi msikubaliane na watu wanaowataka kutochangia miradi ya maendeleo” amesema

Mara baada ya kuweka mawe ya msingi, kuzindua na kufungua miradi mbalimbali katika Halmashauri ya wilaya ya BARIADI Mwenge wa Uhuru tarehe 08/07/2017 utakimbizwa wilayani BUSEGA.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2017, Ndg.Amour Hamad Amour akicheza pamoja na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Nkololo baada ya Mwenge wa Uhuru kufika katika Shule hiyo kwa ajili ya kuzindua klabu ya wapinga rushwa, klabu ya kupambana na dawa za kulevya na kuona mradi wa hifadhi ya mazingira

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, Abdallah Malela akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Mhe.Festo Kiswaga Mwenge wa Uhuru mara baada ya kuupokea kutoka kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji(hayupo pichani)
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2017, Ndg.Amour Hamad Amour akikagua na kuona mraidi wa hifadhi ya mazingira katika Shule ya sekondari Nkololo
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2017, Ndg.Amour Hamad Amour akikagua moja ya vyumba vitatu vya madara vilivyofunguliwa na Mwenge wa Uhuru katika Shule ya Msingi Nkololo “B” wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2017, Ndg.Amour Hamad Amour akisalimiana na baaadhi ya watalaam wa Afya mara baada ya kufungua Kituo cha Ushauri, upimaji na matibabu(CTC)kwa watu wenye VVU katika Kituo cha Afya cha Songambele wilaya ya Bariadi, Mkoani Simiyu.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2017, Ndg.Amour Hamad Amour akimkabidhi cheti mmoja wa wanachama wa Klabu ya kupambana na dawa za kulevya katika Shule ya Sekondari Nkololo mara baada ya kuzindua klabu hiyo.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2017, Ndg.Amour Hamad Amour akimkabidhi cheti cha Utunzaji wa Mazingira Mkuu wa Shule ya Sekondari Nkololo mara baada ya kutembelea na kuona mrai huo.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2017, Ndg.Amour Hamad Amour akiangalia baadhi ya bidhaa za ngozi zinazotengenezwa na kikundi cha vijana kutoka Kata ya Dutwa wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2017, Ndg.Amour Hamad Amour akizungumza na wakazi wa Kijiji cha Nkololo mara baada ya kuweka jiwe la msingi kisima kirefu cha maji kijijini hapo.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2017, Ndg.Amour Hamad Amour akitoa ujumbe wa Mwenge kwa  wanafunzi wa Shule ya Sekondari Nkololo pamoja na wananchi wa Nkololo mara baada kuzindua na kuona miradi mbalimbali shuleni hapo.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2017, Ndg.Amour Hamad Amour akiweka jiwe la msingi katika Mradi wa Maji wa Kisima kirefu katika kijiji cha Nkololo ilaya ya Baraidi, Mkoani Simiyu.


 

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!