Balozi wa Indonesia nchini Tanzania, Mhe. Prof. Dkt..Ratlan Pardede na Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe.Dkt.Hamisi
Kigwangalla Agosti 04, 2019 wametembelea Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019
yanayoendelea katika Kanda ya Ziwa Mashariki, viwanja vya Nanenane
Nyakabindi Simiyu.
Akizungumza mara baada ya kuwapokea wageni hao Mkuu wa Mkoa wa
Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema asilimia 80 ya uchumi wa nchi
unategemea kilimo, hivyo kwa kuwa Mhe.Kigwangalla ni Waziri mwenye Dira kwa
kutembelea maonesho haya atatoa mchango,mawazo na hamasa kubwa kuhusiana na
sekta ya kilimo.
Aidha, amesema Prof.Dkt.Ratlan
Pardede amekuja kwa mara ya pili sasa Mkoani Simiyu, ikiwa ni sehemu ya
kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali ya Indonesia na Mkoa wa Simiyu (Tanzania.)
Naye Waziri wa Maliasili na Utalii Mh Dkt.Hamisi Kigwangalla amepongeza
waandaji wa maonesho haya ya Nanenane Kitaifa (Kanda ya Ziwa Mashariki) kwa
maandalizi mazuri ya pia amewapongeza Wakulima na Wafanyabiashara kwani kwa
kushiriki maonesho haya wanapata fursa ya kujifunza na kuuza mazao yao.
Amesema sekta ya kilimo ni sekta muhimu kwani ndiyo sekta
inayoajiri wananchi wengi ikifuatiwa na sekta ya utalii na inategemewa na Uchumi
wa Viwanda kutoa malighafi za viwanda, huku akibainisha kuwa Utalii unachangia
pato la Taifa kwa asilimia 17.6 , pia unachangia kwa zaidi ya 25% ya
upatikanaji wa fedha za kigeni.
.
Mhe. Kigwangalla ameongeza kuwa mwaka 2015 kulikuwa na ongezeko
la Watalii kutoka Milioni 1 hadi milioni 1.1, .Mwaka 2018 Watalii waliongezeka
hadi kufikia Milioni 1.6 na lengo likawa ni kufikia mwaka 2020 idadi
iongezeke zaidi na kufikia watalii milioni mbili.
Naye Balozi wa Indonesia Prof.Dr.Ratlan Pardede amesema amefurahi
kufika Mkoani Simiyu kwa mara ya pili sasa na Indonesia inashiriki Maonesho ya
Nanenane ili kuimarisha uhusiano wake na Tanzania hususani katika kilimo.
“Nimefura sana kufika kwa mara ya pili sasa mkoani Simiyu tunashiriki
Nanenane kwa sababu tunataka kuimarisha
uhusiano wetu na Mkoa wa Simiyu hususani katika kilimo, kusudi likiwa ni kuona
kwa jinsi gani tunaweza kufanya kazi kwa ushirikiano mkubwa katika siku za
usoni kwa manufaa ya nchi zote mbili yaani Tanzania na Indonesia” alisisitiza.
MWISHO
Mkuu
wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akiwatambulisha Balozi wa Indonesia nchini Tanzania, Mhe. Prof.Dkt..Ratlan Pardede na Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe.Dkt.Hamisi
Kigwangalla Agosti 04, 2019 kwa waandishi wa habari walipotembelea Maonesho ya Nanenane
Kitaifa mwaka 2019 yanayoendelea katika Kanda ya Ziwa Mashariki, viwanja
vya Nanenane Nyakabindi Simiyu.
Mkuu
wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akiwatambulisha Balozi wa Indonesia nchini Tanzania, Mhe. Prof.Dkt..Ratlan Pardede na Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe.Dkt.Hamisi
Kigwangalla Agosti 04, 2019 kwa waandishi wa habari walipotembelea Maonesho ya Nanenane
Kitaifa mwaka 2019 yanayoendelea katika Kanda ya Ziwa Mashariki, viwanja
vya Nanenane Nyakabindi Simiyu.
Balozi wa Indonesia
nchini Tanzania, Mhe. Prof.Dkt..Ratlan
Pardede(kushoto) akizungumza na waandishi wa habari(hawapo pichani) mara baada
ya kuwasili Bariadi, Agosti 04, 2019 ambapo amekuja kushiriki Maonesho ya Nanenane
Kitaifa mwaka 2019 yanayoendelea katika Kanda ya Ziwa Mashariki, viwanja
vya Nanenane Nyakabindi Simiyu.
Waziri wa Maliasili na
Utalii Mhe.Dkt.Hamisi Kigwangalla akizungumza na waandishi wa habari(hawapo
pichani) mara baada ya kuwasili Bariadi Agosti 04, 2019 ambapo amekuja kutembelea
Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 yanayoendelea katika Kanda ya Ziwa
Mashariki, viwanja vya Nanenane Nyakabindi Simiyu.
Waziri wa Maliasili na
Utalii Mhe.Dkt.Hamisi Kigwangalla (mwenye suti) akikagua vipando vya Jeshi la
Kujenga Taifa (JKT) mara baada ya kuwasili Bariadi Agosti 04, 2019 kutembelea Maonesho
ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 yanayoendelea katika Kanda ya Ziwa Mashariki,
viwanja vya Nanenane Nyakabindi Simiyu.
Balozi wa Indonesia
nchini Tanzania, Mhe. Prof.Dkt..Ratlan
Pardede(wa tatu kulia) akiangalia viatu vilivyotengenezwa na Jeshi la Magereza mara
baada ya kutembelea banda la la maonesho, wakati wa ziara yake ya kutembelea Maonesho
ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 yanayoendelea katika Kanda ya Ziwa Mashariki,
viwanja vya Nanenane Nyakabindi Simiyu.
Katibu Tawala Mkoa wa
Simiyu, Bw. Jumanne Sagini(kushoto) akimuongoza Balozi wa Indonesia nchini
Tanzania, Mhe. Prof.Dkt..Ratlan Pardede(wa
pili kulia) kutembelea vipando vya mazao ya Halmashauri za mikoa ya Simiyu,
Mara na Shinyanga wakati wa ziara yake ya kutembelea Maonesho ya Nanenane Kitaifa
mwaka 2019 yanayoendelea katika Kanda ya Ziwa Mashariki, viwanja vya
Nanenane Nyakabindi Simiyu.
Balozi wa Indonesia
nchini Tanzania, Mhe. Prof.Dkt..Ratlan
Pardede(wa pili kulia) akiangalia viatu vilivyotengenezwa na Jeshi la Magereza mara
baada ya kutembelea banda la la maonesho, wakati wa ziara yake ya kutembelea Maonesho
ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 yanayoendelea katika Kanda ya Ziwa Mashariki,
viwanja vya Nanenane Nyakabindi Simiyu.
Baadhi ya wananchi
wakiangalia huduma na bidhaa mbalimbli zinzotolewa na waoneshoaji katika
mabanda ya Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 yanayoendelea katika Kanda
ya Ziwa Mashariki, viwanja vya Nanenane Nyakabindi Simiyu.
Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe.Dkt.Hamisi Kigwangalla (mwenye suti) akipokea maelezo ya mradi wa ufugaji samaki kwa kutumia matanki na kilimo cha mboga mboga wakati akikagua vipando vya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) mara baada ya kuwasili Bariadi Agosti 04, 2019 kutembelea Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 yanayoendelea katika Kanda ya Ziwa Mashariki, viwanja vya Nanenane Nyakabindi Simiyu
Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe.Dkt.Hamisi Kigwangalla (mwenye suti) akikagua
vipando vya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) mara baada ya kuwasili Bariadi Agosti
04, 2019 kutembelea Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 yanayoendelea
katika Kanda ya Ziwa Mashariki, viwanja vya Nanenane Nyakabindi Simiyu
Waziri wa Maliasili na
Utalii Mhe.Dkt.Hamisi Kigwangalla (kulia) akipokea maelezo ya mradi wa kilimo
kupitia kitalu nyumba(green house) wakati akikagua vipando vya Jeshi la Kujenga
Taifa (JKT) Agosti 04, 2019 wakati wa ziara yake ya kutembelea Maonesho ya Nanenane
Kitaifa mwaka 2019 yanayoendelea katika Kanda ya Ziwa Mashariki, viwanja
vya Nanenane Nyakabindi Simiyu.
Waziri wa Maliasili na
Utalii Mhe.Dkt.Hamisi Kigwangalla (mwenye suti) akipokea maelezo ya mradi wa
ufugaji samaki kwa kutumia mabwawa
wakati alipotembelea vipando vya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Agosti 04,
2019 kutembelea Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 yanayoendelea katika
Kanda ya Ziwa Mashariki, viwanja vya Nanenane Nyakabindi Simiyu.
Baadhi ya wananchi
wakipata huduma kutoka kwa waoneshaji
Baadhi ya wananchi
wakipata huduma kutoka kwa waoneshaji ambao ni Halmashauri ya Wilaya ya
Itilima.
Kitalu nyumba kilichopo katika vipando ya Jeshi la Magereza
Baadhi ya wananchi
wakipata huduma kutoka kwa waoneshaji ambao ni Halmashauri ya Wilaya ya
Itilima.
Kitalu nyumba kilichopo
katika vipando ya Jeshi la Magereza
Baadhi ya wananchi
wakipata huduma na kununua bidhaa kutoka kwa waoneshaji ambao ni Halmashauri ya
Wilaya ya Bariadi.
Baadhi ya wananchi wakipata huduma na kununua bidhaa kutoka kwa
waoneshaji ambao ni Halmashauri ya Mji wa Bariadi.
0 comments:
Post a Comment