Naibu
Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhandisi. Stella Manyanya ametoa wito kwa
wananchi kushiriki katika Maonesho ya Nanenane kwa lengo la kujifunza ili
waongeze tija katika uzalishaji, huku akibainisha kuwa maonesho haya
yameboreshwa, kwa wadau na Taasisi zinazotoa huduma kuongezeka na maonesho hayo
kuwa sura ya kuwasaidia wananchi kubadilika.
Mhandisi Manyanya ameyasema hayo Agosti 02, 2019 kwenye Maonesho
ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 yanayofanyika Kanda ya Ziwa Mashariki viwanja
vya Nyakabindi Bariadi mkoani Simiyu.
“ Maonesho ya mwaka huu yamefana sana na kufana kwake hakupo
katika namna mahema yalivyo, bali ushiriki wa waoneshaji, wakulima wenyewe na
nimefurahi kuona baadhi ya mambo yanafanyika kwa vitendo kama uhimilishaji wa
ng’ombe, ufugaji wa samaki, uwepo wa taasisi kama TBS, Wakala wa vipimo na
vyama vya ushirika”
“ Mimi naona tumeboresha zaidi namna ya kufanya haya maonesho
kwenda zaidi katika sura ya kuwagusa wananchi ili waweze kubadilika na kutumia
huduma zinazohitajika, nipende kuwashawishi wananchi wengi zaidi wasikose kuja
kujifunza kupitia maonesho haya, wanapojifunza wanaongeza tija katika maeneo
yao” alisisitiza Mhandisi. Manyanya.
Aidha, amezihamasisha Halmashauri zote nchini kutenga maeneo kwa
ajili ya ujenzi wa viwanda na uwekezaji mwingine ili wawekezaji wanapopatikana
kusiwe na mlolongo mrefu katika kupata
ardhi na kupata vibali mbalimbali, huku akibainisha kuwa Serikali imeshaweka miundombinu
wezeshi kwa uwekezaji kama upatikanaji
wa umeme.
Amesema sekta binafsi ndiyo injini ya ukuaji wa uchumi katika
Taifa hasa kwenye eneo la biashara na viwanda huku akiongeza kuwa ni vyema maonesho
hayo yakawa na kiu ya kufanya mambo yatakayoweza kurahihisha shughuli za
kibiashara.
Awali Naibu Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amesema wananchi
wengi wa Mkoa wa Simiyu wanajishughulisha na shughuli za kilimo hivyo ipo
haja ya kuwepo kituo endelevu cha mafunzo ya kilimo ili wakulima waweze
kupata mahala pa kujifunzia .
“Kutokana na kwamba wananchi wengi wa Mkoa wa Simiyu wanategemea
sana hasa shughuli za kilimo ipo haja ya kuwepo kituo endelevu kwa ajili ya
mafunzo kitachowasaidia wakulima kupata elimu kila siku kutokana na uhitaji
wao”.
Naye Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ametoa wito kwa
wananchi na wajasiriamali wa mkoa wa Simiyu kutembelea Viwanja vya Nanenane kwa
lengo la kujifunza kutoka kwa wenzao kutoka maeneo mbalimbali ya nchi yetu
namna wanavyofanya shughuli zao na namna walivyofanikiwa.
MWISHO
Naibu Waziri wa viwanda na Baishara , Mhandisi. Stella
Manyanya akikagua vipando vya mazao ya kilimo vya Jeshi la Kujenga Taifa(JKT),
Agosti 02, 2019 wakati wa Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019, katika Kanda
ya Ziwa Mashariki Viwanja Vya Nyakabindi bariadi mkoani Simiyu.
Naibu Waziri wa viwanda na Baishara , Mhandisi. Stella
Manyanya akikagua mabanda ya maonesho ya mifugo, Agosti 02, 2019 wakati wa
Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019, katika Kanda ya Ziwa Mashariki Viwanja
Vya Nyakabindi bariadi mkoani Simiyu.
Mmoja wa ng.ombe walio
katika mabanda ya maonesho ya mifugo, kwenye Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka
2019, Kanda ya Ziwa Mashariki Viwanja Vya Nyakabindi Bariadi mkoani Simiyu.
Naibu Waziri wa viwanda na Baishara , Mhandisi. Stella
Manyanya akiangaliabaadhi ya bidhaa zikiwemo viatu zinazotengenezwa na Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la
kujenga Taifa (SUMA JKT) , Agosti 02, 2019 wakati wa Maonesho ya Nanenane
Kitaifa mwaka 2019, katika Kanda ya Ziwa Mashariki Viwanja Vya Nyakabindi Bariadi
mkoani Simiyu.
Naibu Waziri wa viwanda na Baishara , Mhandisi. Stella
Manyanya akimsikiliza mwananchi ambaye aliyekuwa akipatiwa huduma katika
kliniki ya biashara, Agosti 02, 2019
wakati wa Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019, katika Kanda ya Ziwa Mashariki
Viwanja Vya Nyakabindi Bariadi mkoani Simiyu.
Baadhi ya wanafunzi wa
shule ya sekondari Biashara Mjini
Bariadi wakipatiwa elimu katika mabanda ya maonesho ya mifugo kutoka wizara ya
mifugo, Agosti 02, 2019 wakati wa Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019,
katika Kanda ya Ziwa Mashariki Viwanja Vya Nyakabindi Bariadi mkoani Simiyu.
Naibu Waziri wa kilimo,
Mhe. Hussein Bashe akifafanua jambo kwa waandishi wa habari katika mahojiano
maalum Agosti 02, 2019 wakati akiwa kwenye Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019,
katika Kanda ya Ziwa Mashariki Viwanja Vya Nyakabindi Bariadi mkoani Simiyu.
Baadhi ya Viongozi
na Wataalam wakipatiwa elimu katika
mabanda ya Taasisi ya Utafiti wa kilimo, Agosti 02, 2019 wakati wa Maonesho ya
Nanenane Kitaifa mwaka 2019, katika Kanda ya Ziwa Mashariki Viwanja Vya
Nyakabindi Bariadi mkoani Simiyu.
Baadhi ya wananchi
wakielekea kwenye mabanda mbalimbali kwa lengo la kujione huduma na bidhaa
mbalimbali zinazopatikana, kwenye Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019,
katika Kanda ya Ziwa Mashariki Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu.
0 comments:
Post a Comment