Waziri Mkuu Mstaafu
wa Awamu ya nne, Mhe. Mizengo Pinda, amefungua Kongamano la Kilimo Biashara
katika Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 yanayoendelea katika Viwanja vya
Nyakabindi Bariadi Mkoani Simiyu, ambapo amesema kilimo biashara kinaweza kutoa
mwongozo wa changamoto ya tija ndogo katika kilimo; ikiwa ni pamoja na matumizi
ya kilimo cha umwagiliaji, matumizi ya teknolojia sahihi katika uzalishaji na
hifadhi ya mazao.
Mhe. Pinda ameyasema hayo Agosti 06, 2019 mjini Bariadi
katika kongamano la Kilimo Biashara lililofanyika wakati wa Maonesho ya
Nanenane Kitaifa mwaka 2019 yanayofanyika Kitaifa Kanda ya Ziwa Mashariki
Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu.
Mizengo alisema kuwa ni vyema wakatumia teknolojia za kisasa zilizopo
ili waweze kupata tija kwenye kilimo ambacho kina mchango katika pato la Taifa na
kubainisha kuwa mchango wake bado ni mdogo kutokana na sababu nyingi ikiwemo
mabadiliko ya hali ya hewa hatua inayopelekea kilimo kutokuwa na tija ya
kutosha.
Ameongeza kuwa hakuna haja kwa wakulima kulima kwa kutegemea
mvua ilihali maeneo mengi ya Mikoa ya
Kanda ya Ziwa yanazungukwa na ZiwaVictoria lenye maji mengi ambayo yakitumika vizuri
wataweza kuzalisha mavuno mengi kwenye eneo dogo kupitia umwagiliaji na
teknolojia za kisasa zilizopo.
“niishauri tu Mikoa hii ambayo inazungukwa na Ziwa lenye maji
mengi ambayo nchi jirani zinatumia maji hayo kuzalisha mazao kutokana na umwagiliaji
badala ya kutegemea mvua; unapotokea ukame unaathiri mazao hayo ipo haja ya
kuona umuhimu wa kwenda kwenye kilimo cha
umwagiliaji”alisema waziri mkuu mstaafu Pinda
Kwa upande wake Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga amesema sekta ya
kilimo ina uwezo wa kuongeza pato la Taifa kwani inachangia kwa asilimia 28.7 huku
akibainisha kuwa tija ya uzalishaji kwa wakulima bado ipo chini huku
akikisitiza matumizi sahihi ya ardhi na maji hususani kwenye shughuli za
umwagiliaji.
Ameongeza kuwa licha ya asilimia 65.5 ya Watanzania kujiajiri
kwenye sekta ya kilimo moja kwa moja asilimia 66% zinahitajika kwenye viwanda
na kwamba zinatakiwa kuboreshwa ili ziweze kufikia angalau 80%.
Katika hatua nyingine Mhe. Hasunga ametoa wito kwa wawekezaji kuwekeza kwenye viwanda vya mafuta kwani Serikali
inatumia fedha nyingi kuagiza mafuta nje ya nchi licha ya kuwa mazao mengi yana
malighafi ambazo zina uwezo wa kutengeneza mafuta ya kula zipo nchini.
“tuna mazao mengi ambayo malighafi zake zina uwezo wa kutengeza
mafuta lakini serikali inatumia fedha nyingi kuagiza nje ambapo kwa mwaka ni
tani 570,000 huku uwezo wa kuzalisha ukiwa ni tani 250,000 na katika hili tutatumia
maamuzi magumu ili tuwekeze kwenye viwanda vya mafuta” alisema waziri Hasunga
Awali Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka ameyataka makundi ya wanawake, vijana na waoneshaji kwa ujumla wake kutumia fursa ya
uwepo wa Kongamano la Kilimo Biashra kujifunza ili waweze kuongeza ujuzi ambao
utaenda sambamba na kutambua mnyororo wa thamani kwenye mazao na shughuli zao
za kilimo.
Hata hivyo Mkurugezi wa Mtendaji Taasisi ya Utafiti wa
Kiuchumi na Kijamii (ESRF) Tausi Kida amesema kuwa wakati umefika kwa wakulima
kutumia maeneo madogo kuzalisha uzalishaji wenye tija unaoenda sambamba na mazao
bora ambayo yatakuwa na uhakika kwenye masoko ya nje.
MWISHO.
Waziri Mkuu mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Mizengo Pinda akifungua Kongamano la Kilimo Biashara katika Maonesho ya Nanenane yanayofanyika Kitaifa mwaka 2019 Kanda ya Ziwa Mashariki, Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu.
Baadhi ya wakulima, wafugaji, wavuvi,
wafanyabiashara na wajasiriamali wakimsikiliza Waziri Mkuu mstaafu wa awamu ya
nne, Mhe. Mizengo Pinda akifungua Kongamano la Kilimo Biashara katika Maonesho
ya Nanenane yanayofanyika Kitaifa mwaka 2019 Kanda ya Ziwa Mashariki, Viwanja
vya Nyakabindi Bariadi Simiyu.
Baadhi ya wakulima, wafugaji, wavuvi,
wafanyabiashara na wajasiriamali wakimsikiliza Waziri Mkuu mstaafu wa awamu ya
nne, Mhe. Mizengo Pinda akifungua Kongamano la Kilimo Biashara katika Maonesho
ya Nanenane yanayofanyika Kitaifa mwaka 2019 Kanda ya Ziwa Mashariki, Viwanja
vya Nyakabindi Bariadi Simiyu.
Mkurugenzi Mkuu wa ESRF Dkt. Tausi Kida akizungumza
katika Kongamano la Kilimo Biashara katika Maonesho ya Nanenane yanayofanyika
Kitaifa mwaka 2019 Kanda ya Ziwa Mashariki, Viwanja vya Nyakabindi Bariadi
Simiyu.
Waziri Mkuu mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Mizengo
Pinda ( wa tatu kulia) akikagua baadhi
ya bidhaa za wajasiriamali waliowezeshwa na Benki ya NBC mara baada ya
kufungua Kongamano la Kilimo Biashara
katika Maonesho ya Nanenane yanayofanyika Kitaifa mwaka 2019 Kanda ya Ziwa
Mashariki, Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu.
Waziri Mkuu mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Mizengo
Pinda ( wa tatu kulia) akikagua baadhi
ya bidhaa za wajasiriamali waliowezeshwa na Benki ya NBC mara baada ya
kufungua Kongamano la Kilimo Biashara
katika Maonesho ya Nanenane yanayofanyika Kitaifa mwaka 2019 Kanda ya Ziwa
Mashariki, Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, mhe. Anthony Mtaka
akisalimiana na Waziri Mkuu mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Mizengo Pinda mara baada ya kuwasili Viwanja vya
Nyakabindi kwa ajili ya kufungua Kongamano la Kilimo Biashara katika Maonesho
ya Nanenane yanayofanyika Kitaifa mwaka 2019 Kanda ya Ziwa Mashariki, Viwanja
vya Nyakabindi Bariadi Simiyu.
Waziri
Mkuu mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Mizengo Pinda na Waziri wa Kilimo, Mhe.
Japhet Hasunga wakifurahia jambo Kongamano la Kilimo Biashara katika Maonesho
ya Nanenane yanayofanyika Kitaifa mwaka 2019 Kanda ya Ziwa Mashariki, Viwanja
vya Nyakabindi Bariadi Simiyu
Waziri Mkuu mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Mizengo
Pinda na Waziri wa Kilimo, Mhe. Japhet Hasunga
akisalimiana na Katibu wa CCM Mkoa wa Simiyu, muda mfupi kabla ya
kufungua Kongamano la Kilimo Biashara katika Maonesho ya Nanenane yanayofanyika
Kitaifa mwaka 2019 Kanda ya Ziwa Mashariki, Viwanja vya Nyakabindi Bariadi
Simiyu.
Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mhe. Adam Malima (mwenye kofia
mbele) akimuongoza Waziri Mkuu mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Mizengo Pinda
kutembelea mabanda ya maonesho katika Maonesho ya Nanenane yanayofanyika
Kitaifa mwaka 2019 Kanda ya Ziwa Mashariki, Viwanja vya Nyakabindi Bariadi
Simiyu.
Waziri Mkuu mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Mizengo
Pinda ( wa pili kushoto) na Maafisa wa Benki ya NMB wakifurahia jambo wakati
alipowatembelea katika Maonesho ya Nanenane yanayofanyika Kitaifa mwaka 2019
Kanda ya Ziwa Mashariki, Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu.
Waziri Mkuu mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Mizengo Pinda ( wa tatu kushoto) akipokea zawadi kutoka kwa mwakilishi wa wakulima ilipowatembelea katika Maonesho ya Nanenane yanayofanyika Kitaifa mwaka 2019 Kanda ya Ziwa Mashariki, Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu.
Waziri Mkuu mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Mizengo
Pinda ( wa nne kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa NMB katika
Maonesho ya Nanenane yanayofanyika
Kitaifa mwaka 2019 Kanda ya lZiwa Mashariki, Viwanja vya Nyakabindi Bariadi
Simiyu.
Waziri Mkuu mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Mizengo
Pinda ( wa nne kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na wawezeshaji wa Kongamano la Kilimo Biashara
kwenye Maonesho ya Nanenane
yanayofanyika Kitaifa mwaka 2019 Kanda ya Ziwa Mashariki, Viwanja vya
Nyakabindi Bariadi Simiyu.
Waziri Mkuu mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Mizengo
Pinda ( wa nne kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wakuu wa
Wilaya na viongozi wengine wa kitaifa, ilipowatembelea
Maonesho ya Nanenane yanayofanyika
Kitaifa mwaka 2019 Kanda ya Ziwa Mashariki, Viwanja vya Nyakabindi Bariadi
Simiyu.
Waziri Mkuu mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Mizengo
Pinda ( wa nne kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na kamati ya Ulinzi na
Usalama ya Mkoa wa Simiyu, Maonesho ya
Nanenane yanayofanyika Kitaifa mwaka
2019 Kanda ya Ziwa Mashariki, Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu
Waziri Mkuu mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Mizengo
Pinda (kushoto) akisaini Kitabu cha wageni,
katika Maonesho ya Nanenane yanayofanyika Kitaifa mwaka 2019 Kanda ya
Ziwa Mashariki, Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu.
Waziri Mkuu mstaafu wa awamu nne, Mhe. Mizengo Pinda
akipokelewa na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa, mara baada ya kuwasili kwa
Viwanja vya Nyakabindi kwa lengo la kufungua kongamano la Kilimo
biashara , katika Maonesho ya
Nanenane yanayofanyika Kitaifa mwaka
2019 Kanda ya Ziwa Mashariki, Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu.
Waziri Mkuu mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Mizengo
Pinda ( wa nne kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa
mara baada ya kumalizika kwa Kongamano la Kilimo Biashara kwenye
Maonesho ya Nanenane yanayofanyika
Kitaifa mwaka 2019 Kanda ya Ziwa Mashariki, Viwanja vya Nyakabindi Bariadi
Simiyu.
Waziri Mkuu mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Mizengo
Pinda ( wa pili kushoto)akiangalia ng’ombe wanaofugwa kisasa na JKT wakati wa Maonesho ya Nanenane Kitaifa, Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu, (kulia) Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mhe. Adam Malima.
Waziri
Mkuu mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Mizengo Pinda ( wa tatu kushoto)akiangalia
nguo zinazoshonwa na kuuzwa na JKT.
Waziri Mkuu mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Mizengo
Pinda ( wa pili kushoto)akiangalia namna teknolojia ya ufugaji wa samaki
Viongozi wa Kitaifa na Mkoa wa wakimuongoza Waziri
Mkuu mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Mizengo Pinda ( wa pili kushoto) akiangalia
namna teknolojia ya ufugaji wa samaki
Waziri Mkuu mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Mizengo
Pinda ( wa nne kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa Kongamano la Kilimo Biashara
kwenye Maonesho ya Nanenane
yanayofanyika Kitaifa mwaka 2019 Kanda ya Ziwa Mashariki, Viwanja vya
Nyakabindi Bariadi Simiyu.
Waziri
Mkuu mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Mizengo Pinda ( wa pili kulia)akisaini
Kitabu cha wageni katika Banda la Benki ya CRDB , kwenye Maonesho ya
Nanenane yanayofanyika Kitaifa mwaka
2019 Kanda ya Ziwa Mashariki, Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu.
Waziri Mkuu Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Mizengo Pinda
(kulia) akiteta jambo na Meneja wa NMB Kanda ya Magharibi, Bw. Sospeter Magesse
wakati alipotembelea banda la Benki ya NMB kwenye
Maonesho ya Nanenane yanayofanyika
Kitaifa mwaka 2019 Kanda ya Ziwa Mashariki, Viwanja vya Nyakabindi Bariadi
Simiyu.
Waziri Mkuu Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Mizengo Pinda
(kulia) akiangalia mafuta ya nazi yanayotengenezwa na Shirika la Uzalishaji
Mali la Jeshi la Kujenga Taifa(JKT), wakati alipotembelea banda la JKT kwenye
Maonesho ya Nanenane yanayofanyika
Kitaifa mwaka 2019 Kanda ya Ziwa Mashariki, Viwanja vya Nyakabindi Bariadi
Simiyu.
Waziri Mkuu Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Mizengo Pinda
(wa nne kulia) akiangalia teknolojia ya ufugaji samaki kwa kutumia matanki wakati alipotembelea eneo la JKT kwenye
Maonesho ya Nanenane yanayofanyika
Kitaifa mwaka 2019 Kanda ya Ziwa Mashariki, Viwanja vya Nyakabindi Bariadi
Simiyu.
Waziri Mkuu Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Mizengo Pinda
(wa pili kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Mkoa wa
Simiyu na maafisa wa JKT mara baada ya kufungua Kongamano la Kilimo Biashara
kwenye Maonesho ya Nanenane yanayofanyika Kitaifa mwaka 2019 Kanda ya
Ziwa Mashariki, Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu.
Waziri wa Kilimo, Mhe. Japhet Hasunga akizungumza na
washiriki wa Kongamano la Kilimo Biashara(hawapo pichani) ambalo lilifunguliwa na Waziri Mkuu Mstaafu wa
awamu ya nne, Mhe. Mizengo Pinda, Agosti 06, 2019 kwenye Maonesho ya Nanenane yanayofanyika Kitaifa mwaka 2019 Kanda ya
Ziwa Mashariki, Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu.
Waziri Mkuu mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Mizengo
Pinda ( wa nne kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wakurugenzi
wa idara mbalimbali katika Wizara ya kilimo na Wizara ya Mifugo na Uvuvi baada
ya kufungua Kongamano la Kilimo Biashara Agosti 06, 2019 kwenye Maonesho ya
Nanenane yanayofanyika Kitaifa mwaka
2019 Kanda ya Ziwa Mashariki, Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu.
0 comments:
Post a Comment