Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya dawa (MSD) Laurean
Bwanakunu amesema Bohari ya dawa inatarajia kuanza ujenzi wa kituo cha mauzo
na usambazaji dawa mkoani Simiyu ili kurahisisha utoaji
wa huduma kwa mkoa wa Simiyu na mikoa jirani.
Bwanakunu ameyasema hayo Agosti 19,2019 katika ufunguzi
wa mkutano wa tathmini ya utendaji kazi wa menejimenti na
mameneja wa kanda wa bohari ya dawa nchini.
lengo
likiwa ni kujenga ushirikiano na kufanya kazi kwa timu.
Bwanakunu amesema wameamua
kufanyia mkutano wa tathimini mkoani Simiyu ili kuweza kujionea eneo la ujenzi
wa kituo cha mauzo ya dawa ikiwa ni moja ya kuongeza wigo mpana wa utoaji
huduma.
“Tutakuwa na mkutano
wa siku tatu hapa Simiyu kwa ajili kufanya tathmini ya utendaji kazi ulivyokuwa
kwa mwaka mzima, tutawafanyia tathmini wakurugenzi wote na wenyewe watamfanyia
Mkurugenzi Mkuu; lakini pia tutatumia fursa hii kutembelea mahali tulipoamua
kujenga bohari kwa kuwa tunatarajia kujenga bohari hapa Simiyu”alisema Bwanakunu.
Akifungua mkutano huu,
Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini amesema maboresho
ya usambazaji wa dawa yaliyofanywa na Bohari ya Dawa (MSD) yameongeza
upatikanaji wa dawa mkoani Simiyu ambapo kwa sasa upatikananji wa dawa ni zaidi
ya asilimi 88.
Aidha, Sagini ametoa
wito kwa Taasisi zote za Umma zinazohitaji maeneo kwa ajili ya kujenga Ofisi
zao kufika mkoani Simiyu, ambapo amewahakikishia upatikanaji wa maeneo lengo
likiwa ni kuendelea kusogeza huduma mbalimbali karibu na wananchi.
Mkurugenzi wa Rasilimali
watu wa Bohari ya Dawa(MSD), Bibi. Victoria
Elangwa amesema uwepo wa kituo cha kusambaza dawa Simiyu kutapunguza umbali kwa
Mkoa wa Simiyu na mikoa ya Mara na Shinyanga kupata huduma za Bohari ambazo kwa sasa zinapatikana
Mwanza.
Ameongeza kuwa ujenzi
wa Kituo hicho unatarajia kuanza mara moja kwa kuwa tayari wataalam wameshaanza
kushughulikia masuala ya ukamilifu wa mazingira na baada kukamilisha kazi hiyo
atatafutwa mkandarasi kwa ajili ya kuanza ujenzi.
MWISHO
Mkurugenzi mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD) Laurean Bwanakunu
akitoa neno la utangulizi katika mkutano wa tathimini ya utendaji kazi
wa Bohari ya Dawa(MSD) unaofanyika Mjini Bariadi mkoani Simiyu kwa
siku tatu na lengo likiwa ni kujenga ushirikiano na
kufanya kazi kwa timu, Agosti 19, 2019.
Katibu
Tawala wa mkoa wa Simiyu akifungua mkutano wa tathimini ya utendaji kazi wa Bohari ya Dawa(MSD)
unaofanyika Mjini Bariadi mkoani Simiyu kwa siku tatu na lengo
likiwa ni kujenga ushirikiano na kufanya kazi kwa timu, Agosti 19,
2019.
Katibu
Tawala wa mkoa wa Simiyu akifungua mkutano wa tathimini ya utendaji kazi wa Bohari ya Dawa(MSD)
unaofanyika Mjini Bariadi mkoani Simiyu kwa siku tatu na lengo
likiwa ni kujenga ushirikiano na kufanya kazi kwa timu, Agosti 19,
2019.
Mkurugenzi wa Utawala
na Rasilimali watu wa Bohari ya Dawa(MSD), Victoria Mwanri Elangwa akitoa
taarifa katika mkutano wa tathimini ya utendaji kazi wa Bohari ya Dawa(MSD)
unaofanyika Mjini Bariadi mkoani Simiyu kwa siku tatu na lengo
likiwa ni kujenga ushirikiano na kufanya kazi kwa timu, Agosti 19,
2019.
Katibu Tawala wa Mkoa
wa Simiyu, bw. Jumanne Sagini (wanne kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na
wakurugenzi wa idara mbalimbali na mameneja wa kanda wa Bohari ya Dawa
nchini(MSD) mara baada ya kufungua mkutano wao wa siku tatu, Agosti 19, 2019
ambao unafanyika kwa siku tatu Mjini Bariadi Mkoani Simiyu
Baadhi ya wakurugenzi
wa idara mbalimbali na mameneja wa kanda wa Bohari ya Dawa nchini(MSD) wakiwa
katika mkutano wao wa siku tatu,uliofunguliwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa
Simiyu, bw. Jumanne Sagini Agosti 19,
2019 ambao unafanyika kwa siku tatu Mjini Bariadi Mkoani Simiyu.
Baadhi ya wakurugenzi
wa idara mbalimbali na mameneja wa kanda wa Bohari ya Dawa nchini(MSD) wakiwa
katika mkutano wao wa siku tatu,uliofunguliwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa
Simiyu, bw. Jumanne Sagini Agosti 19,
2019 ambao unafanyika kwa siku tatu Mjini Bariadi Mkoani Simiyu.
Baadhi ya wakurugenzi
wa idara mbalimbali na mameneja wa kanda wa Bohari ya Dawa nchini(MSD) wakiwa
katika mkutano wao wa siku tatu,uliofunguliwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa
Simiyu, bw. Jumanne Sagini Agosti 19,
2019 ambao unafanyika kwa siku tatu Mjini Bariadi Mkoani Simiyu..
Baadhi ya wakurugenzi
wa idara mbalimbali na mameneja wa kanda wa Bohari ya Dawa nchini(MSD) wakiwa
katika mkutano wao wa siku tatu,uliofunguliwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa
Simiyu, bw. Jumanne Sagini Agosti 19,
2019 ambao unafanyika kwa siku tatu Mjini Bariadi Mkoani Simiyu..
0 comments:
Post a Comment