Waziri
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Mhe. Kassim Majaliwa amezindua mifumo mitatu
ya kielekroniki inayolenga kuboresha na kurahisisha ufanyaji wa biashara
za mazao ya Kilimo ambayo ni mfumo wa
kusajili wakulima nchini, mfumo wa soko
la bidhaa na mfumo wa uingizaji na ununuzi wa mazao nje ya nchi.
Mhe.
Waziri Mkuu amefanya uzinduzi huo Agosti 08, 2019 katika Viwanja vya Nyakabindi
Bariadi Mkoani Simiyu kwenye Kilele cha Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019,
ambapo pia amewahakikishia wakulima wote wa pamba kuwa pamba yote itanunuliwa
na kuondoka mikononi mwao.
Aidha,
amezitaka benki zote zinatoa fedha kwa wanunuzi wa pamba kutoa taarifa kwa
serikali juu ya fedha walizotoa kwa wanunuzi wa pamba, ili Serikali ijue na
kuweka mikakati ya usimamizi katika kuhakikisha fedha zote zinapelekwa kwa
wakulima wa pamba kama ilivyokusudiwa na si vinginevyo.
“Tunataka
pamba yote itoke haraka mikononi mwa wakulima kwa sababu hali ya hewa
inabadilika, tunataka wakulima wapate fedha zao waanze mpango mpya wa kilimo cha
mwaka ujao, wapeleke watoto wote shule wafanye na mambo mengine,”
“Haya
ndiyo matakwa na maagizo yaliyotolewa na Rais wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe
Magufuli kwa hiyo wakulima katika hili muwe na amani kabisa kwamba pamba
inakuja kununuliwa na wanunuzi wako karibu katika wilaya zote” alisisitiza Mhe.
Waziri Mkuu.
Katika
hatua nyingine Mhe. Majaliwa amewaagiza maafisa mifugo kuendelea kutoa elimu
kwa wafugaji kuhusu kuacha tabia ya kupiga chapa na kuweka alama kwenye mifugo
kwa kuchoma ngozi jambo ambalo amesema linaharibu na kupunguza ubora na thamani
ya ngozi hiyo.
Naye
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka amesema katika kutafuta suluhisho la changamoto
ya bei ya pamba Mkoa wa Simiyu unaomba kijengwe kiwanda cha nguo huku
akibainisha kuwa tayari barua imewasilishwa Benki Kuu kuomba idara ya sera na
utafiti kuandaa andiko/ kufanya upembuzi yakinifu kuhusu uwepo wa kiwanda cha
nguo
Ameongeza
kuwa Mkoa wa Simiyu pia ni kwamba unaomba andiko la mradi wa ujenzi wa kiwanda
cha nguo litakapokamilishwa Serikali ione uwezekano wa kutoa fedha za miradi ya
kimkakati kwa Halmashauri za mkoa wa Simiyu ili kiwanda hicho kiweze kujengwa
kupitia fedha hizo.
“Mhe.
Waziri Mkuu tumemuona Mhe. Naibu Waziri wa Fedha akirudisha fedha kutoka kwenye
Halmashauri zilizoshindwa kufanya miradi ya kimkakati, mapendekezo yangu Mhe.
Waziri Mkuu sisi Simiyu tuna Halmashauri sita tunaomba tukipata andiko la mradi
wa kiwanda cha nguo, zile fedha za miradi ya kimkakati ambazo Halmashauri
nyingi zimeshindwa kufanya tuweze kwenda kwenye kiwanda cha nguo” alisema
Mtaka.
Awali
akizungumza kabla ya kumkaribisha Mhe. Waziri Mkuu Waziri wa kilimo, Mhe.
Japhet Hasunga amesema Wizara imejipanga kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi
kwa kuimarisha kilimo cha umwagiliaji, kutumia mbegu bora zinazovumilia ukame
na magonjwa na zinazotoa mavuno mengi
Maonesho
ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 yameongozwa na Kauli Mbiu “Kilimo, Mifugo na
Uvuvi kwa ukuaji wa Uchumi wa Nchi” na yameadhimishwa kwa mara ya pili sasa
katika Kanda ya Ziwa Mshariki ambapo na mwaka 2020 yatafanyika tena Kitaifa
Mkoani Simiyu.
MWISHO
Waziri
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa
akionesha vitabu vyenye mifumo mitatu inayoboresha na kurahisisha ufanyaji wa
biashara za mazao ya Kilimo ambayo ameizindua katika Kilele cha Maonesho ya
Nanenane Kitaifa mwaka 2019 Agosti 08, 2019, katika Viwanja vya Nyakabindi
Bariadi Simiyu.
Waziri
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa
akionesha vitabu vyenye mifumo mitatu inayoboresha na kurahisisha ufanyaji wa
biashara za mazao ya Kilimo ambayo ameizindua katika Kilele cha Maonesho ya
Nanenane Kitaifa mwaka 2019 Agosti 08, 2019, katika Viwanja vya Nyakabindi
Bariadi Simiyu.
Waziri
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa
akionesha Kifaa maalum kwa ajili ya
mifumo mitatu inayoboresha na kurahisisha ufanyaji wa biashara za mazao
ya Kilimo ambayo ameizindua katika Kilele cha Maonesho ya Nanenane Kitaifa
mwaka 2019 Agosti 08, 2019, katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu.
Waziri
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa
akitembelea mabanda ya Maonesho ya Taasisi mbalimbali mara baada ya kuwasili Bariadi kwa ajili ya
Kilele cha Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 Agosti 08, 2019, katika
Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu.
Waziri
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa
akitembelea mabanda ya Maonesho ya Taasisi mbalimbali mara baada ya kuwasili Bariadi kwa ajili ya
Kilele cha Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 Agosti 08, 2019, katika
Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa na viongozi wetu wa Mkoa wakiimba wimbo wa Taifa ikiwa ni ishara ya kuanza rasmi Halfa ya ya Kilele cha Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 Agosti 08, 2019, katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu.
Waziri
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa akiondoka katika
Viwanja vya Nyakabindi mara baada ya kuhitimisha Maonesho ya Nanenane Kitaifa
mwaka 2019 Agosti 08, 2019, Bariadi Simiyu
Baadhi
ya wakuu wa Wilaya za mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi Waziri
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa katika
Kilele cha Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 Agosti 08, 2019, katika
Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu.
Katibu
Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally akitoa salamu za chama katika Kilele cha
Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 Agosti 08, 2019, katika Viwanja vya
Nyakabindi Bariadi Simiyu.
Mkuu
wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka na viongozi wengine wakicheza wimbo wa
asili ya wauskuma pamoja na Msanii Elizabeth Maliganya katika Kilele cha
Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 Agosti 08, 2019, katika Viwanja vya
Nyakabindi Bariadi Simiyu.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa akizungamza jambo na mwananchi ambaye yupo Viwanja vya Nyakabindi wakati wa Kilele cha Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 Agosti 08, 2019, Bariadi Simiyu.
Waziri
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa akiangalia namna
mazao ya kilimo yanavyopandwa katika ujuzi tofauti mara baada ya kuwasili Viwanja vya Nyakabindi wakati wa Kilele cha
Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 Agosti 08, 2019, Bariadi Simiyu.
Wananchi
wakimsikiliza Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe. Kassim
Majaliwa kwenye Kilele cha Maonesho ya
Nanenane Kitaifa mwaka 2019 Agosti 08, 2019, katika Viwanja vya Nyakabindi
Bariadi Simiyu.
Vikundi
vya Burudani vikitumbuiza kwenye Kilele cha Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka
2019 Agosti 08, 2019, katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu
Vipando
vya Mbogamboga katika Viwanja vya Nanenane Nyakabindi eneo la JKT.
Waziri
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa akimkabidhi
zawadi ya kikombe na cheti Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa, kwa kuwa mshindi wa
kwanza katika kundi la Vyombo vya Ulinzi na Usalama, kwenye Kilele cha Maonesho
ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 Agosti 08, 2019, katika Viwanja vya Nyakabindi
Bariadi Simiyu.
Mkurugenzi
wa AGRICOM akipokea cheti cha mshindi wa
kwanza wa wanaouza bidhaa/zana bora za kilimo kwenye Kilele cha Maonesho ya
Nanenane Kitaifa mwaka 2019 Agosti 08, 2019, katika Viwanja vya Nyakabindi
Bariadi Simiyu.
Mkuu
wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akimpongeza mwakilishi wa CLOUDS
MEDIA Bw. Hassan Ngoma kutokana na
CLOUDS MEDIA kuwa MSHINDI WA KWANZA
Katika kundi la vyombo vya habari vya
utangazaji kwenye Kilele cha Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 Agosti 08,
2019, katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu
0 comments:
Post a Comment