Makamu wa Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan leo Agosti Mosi,
2019 amezindua mkakati wa udhibiti wa upotevu wa mazao wenye lengo la kumsaidia
mkulima namna ya utunzaji Bora wa mazao baada ya mavuno.
Mama Samia amezindua mkakati huo katika
ufunguzi rasmi wa Maonesho ya Nane Name Kitaifa, uliofanyika Kanda ya Ziwa Mashariki
katika Viwanja vya Nyakabindi mkoani
Simiyu.
Amesema upotevu wa mazao ni moja ya changamoto
zinazowakabili wakulima na kupelekea kuwa na tija ndogo huku akizitaja
changamoto nyingine kuwa ni matumizi hafifu ya mbolea, kutopata mbegu na viuatilifu kwa wakati na vilivyo
bora na kutotumia kanuni bora za kilimo.
Aidha, Mhe. Makamu
wa Rais ametoa wito kwa Taasisi za Umma, binafsi, vyama vya ushirika na Taasisi
za kiraia zinzojishughulisha na Maendeleo ya Kilimo kuhakikisha wanarekebisha
kosoro zilizopo na kutoa elimu bora na kutosha inayojibu changamoto hizo.
Katika hatua nyingine Mhe. Makamu wa Rais ametoa rai kwa
watafiti wote nchini kutoa matokeo ya tafiti zao kwa maafisa ugani na wadau
wengine ili wakulima wanufaike na matokeo hayo.
Akizungumzia mkakati wa kudhibiti upotevu wa
mazao miaka 10, Waziri wa Kilimo, Mhe. Japhet Hasunga amesema lengo la serikali
ni kuhakikisha inapunguza upotevu wa mazao kwa asilimia 50 ifikapo mwaka 2025.
Kwa upande
wake Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema dhamira ya mikoa
inayounda Kanda ya Nanenane ya Ziwa Mashariki ni kuvifanya viwanja vya maonesho
ya Nanenane Nyakabindi kuwa ni mahali patakapojibu kwa vitendo sera za wizara
ya kilimo na pawe mfano kwa wananchi kujifunza Kilimo Biashara.
Pia ametoa wito kwa
wanunuzi wa pamba kuendelea kununua pamba kwa bei elekezi ya shilingi 1200 na
taasisi za fedha kutoa fedha kwa wanunuzi pamba ya wakulima inunuliwe, huku
akiiomba Serikali kuridhia sehemu ya fedha ikakatwa fedha hiyo iweze kuwekeza
kwenye ujenzi wa kiwanda cha nguo kwa kushirikiana na wadau wengine ili kuwa na
soko la uhakika la pamba.
Maonesho
ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 yanafanyika kwa mara ya pili mfululizo sasa
katika Kanda ya Ziwa Mashariki inayoundwa na Mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga,
yakiwa na Kauli Mbiu isemayo Kilimo, Mfugo na Uvuvi kwa Ukuaji wa Uchumi wa
Nchi”.
MWISHO
Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akionesha Nakala ya
Mkakati wa Udhibiti wa Upotevu wa mazao uliozinduliwa kwenye ufunguzi wa Maonesho ya Nanenane Kitaifa
mwaka 2019 leo Agosti Mosi, 2019 , yanayofanyika Kanda ya Ziwa Mashariki Viwanja vya Nyakabindi
Bariadi Mkoani Simiyu.
Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Mkuu wa
Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka
Nakala ya Mkakati wa Udhibiti wa Upotevu wa mazao kwa niaba ya wakuu wa mikoa yote nchini, uliozinduliwa kwenye ufunguzi wa Maonesho ya Nanenane Kitaifa
mwaka 2019 leo Agosti Mosi, 2019 yanayofanyika Kanda ya Ziwa Mashariki Viwanja
vya Nyakabindi Bariadi Mkoani Simiyu.
Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Mkuu wa
Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka
Nakala ya Mkakati wa Udhibiti wa Upotevu wa mazao kwa niaba ya wakuu wa mikoa yote nchini, uliozinduliwa kwenye ufunguzi wa Maonesho ya Nanenane Kitaifa
mwaka 2019 leo Agosti Mosi, 2019 yanayofanyika Kanda ya Ziwa Mashariki Viwanja
vya Nyakabindi Bariadi Mkoani Simiyu.
Kutoka kushoto Mkuu wa
Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ,
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu
Hassan na Waziri wa Kilimo, Mhe. Japhet Hasunga wakifurahia jambo katika
ufunguzi wa Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 leo Agosti Mosi, 2019 ,
yanayofanyika katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Mkoani Simiyu.
Baadhi ya Wakuu wa
Mikoa walioshiriki katika ufunguzi wa
Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 leo Agosti Mosi 2019 , yanayofanyika katika Viwanja vya
Nyakabindi Bariadi Mkoani Simiyu.
Kikundi cha Kwaya ya
ICT Bariadi kikitoa burudani katika ufunguzi
wa Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 leo Agosti Mosi 2019 , yanayofanyika
katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Mkoani Simiyu.
Baadhi
ya mabanda ya Maonesho Nanenane Kitaifa
2019 yanayoendelea katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu, Kanda ya Ziwa
Mashariki.
Baadhi ya mabanda ya Maonesho Nanenane Kitaifa 2019 yanayoendelea katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu, Kanda ya Ziwa Mashariki.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akiagana na Mkuu wa Wilaya ya Itilima, Mhe. Benson Kilangi mara baada ya kufungua Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019
Baadhi ya mabanda ya Maonesho Nanenane Kitaifa 2019 yanayoendelea katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu, Kanda ya Ziwa Mashariki.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akiagana na Mkuu wa Wilaya ya Itilima, Mhe. Benson Kilangi mara baada ya kufungua Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019
Baadhi ya viongozi wa Kitaifa
na mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga wakiimba wimbo wa Taifa, wakati wa
ufunguzi wa Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 leo Agosti Mosi, 2019 ,
yanayofanyika katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Mkoani Simiyu.
Baadhi ya mabanda ya
Maonesho Nanenane Kitaifa 2019
yanayoendelea katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu, Kanda ya Ziwa
Mashariki.
Kikundi cha Ngoma
cha BASEKI mjini Bariadi kikitoa burudani katika ufunguzi wa Maonesho ya
Nanenane Kitaifa mwaka 2019 leo Agosti Mosi 2019 , yanayofanyika katika Viwanja
vya Nyakabindi Bariadi Mkoani Simiyu.
Baadhi ya mabanda ya
Maonesho Nanenane Kitaifa 2019
yanayoendelea katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu, Kanda ya Ziwa
Mashariki.
Baadhi ya viongozi wa
Kitaifa na mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga wakiagana na Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan , mara baada ya ufunguzi wa Maonesho ya Nanenane Kitaifa
mwaka 2019 leo Agosti Mosi, 2019 , yanayofanyika Kanda
ya Ziwa Mashariki Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Mkoani Simiyu.
Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Waziri wa
Kilimo, Mhe. Japhet Hasunga Nakala ya
Mkakati wa Udhibiti wa Upotevu wa mazao kwa
niaba ya Mawaziri wengine,
uliozinduliwa kwenye ufunguzi wa
Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 leo Agosti Mosi, 2019 yanayofanyika katika Viwanja vya Nyakabindi
Bariadi Mkoani Simiyu.
Kutoka kushoto ni Naibu
Waziri wa kilimo, Mhe.Omary Mgumba, Waziri wa Kkilimo Mhe. Japhet Hasunga
wakiteta jambo, mara baada ya
ufunguzi wa Maonesho ya Nanenane Kitaifa
mwaka 2019 leo Agosti Mosi, 2019 , yanayofanyika katika Viwanja vya Nyakabindi
Bariadi Mkoani Simiyu.
Naibu Waziri wa Kilimo,
Mhe. Hussein Bashe akimsikilza Mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Mhe. Zainabu Telack
mara baada ya ufunguzi wa Maonesho ya
Nanenane Kitaifa mwaka 2019 leo Agosti Mosi, 2019 , yanayofanyika katika
Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Mkoani Simiyu.
Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akiagana na Mkuu wa
TAKUKURU Mkoa wa Simiyu, Bw. Adili Elinipenda mara baada ya kufungua Maonesho
ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019.
Mkuu wa Mkoa wa
Shinyanga, Mhe. Zainab Telack akitoa salamu za mkoa wakati wa ufunguzi wa
Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 leo Agosti Mosi, 2019 , yanayofanyika
katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Mkoani Simiyu.
Mkuu wa Mkoa wa Mara,
Mhe. Adam Malima akitoa salamu za mkoa wakati wa ufunguzi wa Maonesho ya
Nanenane Kitaifa mwaka 2019 leo Agosti Mosi, 2019 , yanayofanyika Kanda ya Ziwa
Mashariki katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Mkoani Simiyu.
Mkuu
wa Mkoa wa Mara, Mhe. Adam Malima akitoa salamu za mkoa wakati wa ufunguzi wa
Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 leo Agosti Mosi, 2019 , yanayofanyika
Kanda ya Ziwa Mashariki katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Mkoani Simiyu.
Kikundi cha Eliza band
kutoka Bariadi Simiyu wakitoa burudani
katika ufunguzi wa Maonesho ya Nanenane Kitaifa 2019 yanayofanyika
katika Kanda ya Ziwa Mashariki Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Mkoani Simiyu.
0 comments:
Post a Comment