Saturday, September 17, 2016

WAZIRI MHAGAMA AFANYA ZIARA SIMIYU KUONA HALI YA MAANDALIZI YA KILELE CHA MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2016

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi , Vijana , Ajira na Wenye Ulemavu , Mhe. Jenista Mhagama amefanya kikao cha ndani na Viongozi na Watendaji wa Mkoa wa Simiyu leo katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo Mjini Bariadi, ili kupata taarifa ya maandalizi ya Maadhimisho ya Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru, Wiki ya Vijana na Kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa, yanayotarajiwa kufanyika mkoani humo tarehe 8 na 14 Oktoba  2016 .

Mkoa wa Simiyu umepewa heshima ya kuwa mwenyeji wa maadhimisho hayo kwa mwaka huu. Maadhimisho ya wiki ya vijana yatafunguliwa rasmi tarehe 08 Oktoba 2016 na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi , Vijana , Ajira na Wenye Ulemavu , Mhe. Jenista Mhagama na kuhitimishwa tarehe 14 Oktoba, 2016, ambapo Vikundi vya Vijana na Wajasiriamali kutoka mikoa yote nchini watashiriki na kuonesha kazi zao za uzalishaji ikiwa ni pamoja na shughuli za ugunduzi wa vitu mbalimbali katika Uwanja wa Sabasaba Mjini Bariadi.

Pamoja na maonesho ya kazi za vijana, Maadhimisho ya Kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru na Kumbukumbu ya Baba  kifo cha Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere yatafanyika tarehe 14 Oktoba 2016 katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi ambapo Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli .

Mhe. Mhagama amesema Maadhimisho ya Kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2016 ni ya Kihistoria kwa kuwa ni ya kwanza kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli  na tukio la kihistoria kwa Mkoa wa Simiyu pia.

Akiwa Wilayani Bariadi  Mhe. Mhagama pamoja na kufanya kikao na viongozi na watendaji, alitembelea na kuona Kanisa la Mtakatifu Yohana(John) la Mjini Bariadi, ambapo Ibada ya Kumbukumbu ya Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere itafanyika, Uwanja wa Sabasaba utakaotumika katika maonesho ya kazi za vijana katika wiki ya vijana na Uwanja wa Halmashauri ya Mji Bariadi ambao utatumika katika Maadhimisho ya Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru Oktoba 14, 2016.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi , Vijana , Ajira na Wenye Ulemavu , Mhe. Jenista Mhagama akisalimiana na Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Jumanne Sagini mara baada ya kuwasili mjini Bariadi kwa ajili ya kukutana na Viongozi na Watendaji wa Mkoa huo, kupata taarifa na kujionea maandalizi ya Maadhimisho ya Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru, Wiki ya Vijana na Kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa, yanayotarajiwa kufanyika mkoani humo tarehe 8 na 14 Oktoba  2016 .
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi , Vijana , Ajira na Wenye Ulemavu , Mhe. Jenista Mhagama akisalimiana na Afisa Usalama Mkoa wa Simiyu, mara baada ya kuwasili mjini Bariadi kwa ajili ya kukutana na Viongozi na Watendaji wa Mkoa huo, kupata taarifa na kujionea maandalizi ya Maadhimisho ya Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru, Wiki ya Vijana na Kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa, yanayotarajiwa kufanyika mkoani humo tarehe 8 na 14 Oktoba  2016 .
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga (kulia)akitoa maelezo ya utangulizi (Kwa Niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka) kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi , Vijana , Ajira na Wenye Ulemavu , Mhe. Jenista Mhagama, kabla ya kumkaribisha Katibu Tawala Mkoa, Jumanne Sagini (hayupo pichani) kuwasilisha taarifa ya maandalizi ya Maadhimisho ya Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru, Wiki ya Vijana na Kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa, yanayotarajiwa kufanyika mkoani humo tarehe 8 na 14 Oktoba  2016
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi , Vijana , Ajira na Wenye Ulemavu , Mhe. Jenista Mhagama (kushoto) akipokea taarifa ya maandalizi ya Maadhimisho ya Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru, Wiki ya Vijana na Kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa, yanayotarajiwa kufanyika mkoani humo tarehe 8 na 14 Oktoba  2016 , kutoka kwa Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Jumanne Sagini.

: Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi , Vijana , Ajira na Wenye Ulemavu , Mhe. Jenista Mhagama (kushoto) akizungumza na Viongozi na Watendaji wa Mkoa wa Simiyu(hawapo pichani) , mara baada ya kupata taarifa na kujionea hali ya maandalizi ya Maadhimisho ya Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru, Wiki ya Vijana na Kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa, yanayotarajiwa kufanyika mkoani humo tarehe 8 na 14 Oktoba  2016, (kulia) Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Jumanne Sagini.

 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi , Vijana , Ajira na Wenye Ulemavu , Mhe. Jenista Mhagama Katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi , Vijana , Ajira na Wenye Ulemavu , Mhe. Jenista Mhagama akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kutembelea Kanisa la Mtakatifu Yohana(John) la Mjini Bariadi, mahali ambapo Ibada ya Kumbukumbu ya Baba wa Taifa itafanyika tarehe 14 Oktoba  2016.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi , Vijana , Ajira na Wenye Ulemavu , Mhe. Jenista Mhagama akiagana na Padre Kizito Nyanga  mara baada ya kutembelea Kanisa la Mtakatifu Yohana (John) la mjini Bariadi , mahali ambapo Ibada ya Kumbukumbu ya Baba wa Taifa itafanyika tarehe 14 Oktoba  2016
Waziri wa Nchi  Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi , Vijana , Ajira na Wenye Ulemavu , Mhe. Jenista Mhagama akitoa maelekezo baada ya kukagua sampuli ya mabanda yatakayotumiwa na vijana katika maonesho ya kazi zao wakati wa maonesho ya wiki ya vijana atakayoyafungua rasmi tarehe 08 Oktoba, 2106 katika Uwanja wa Sabasaba Mjini Bariadi, (kulia) Mkurugenzi wa Idara ya Vijana kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi , Vijana , Ajira na Wenye Ulemavu, Bw. Jemasi  Kajugusi
: Waziri wa Nchi  Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi , Vijana , Ajira na Wenye Ulemavu , Mhe. Jenista Mhagama akiangalia baadhi ya miundombinu (haipo pichani) itakayotumiwa na vijana katika maonesho ya kazi zao wakati wa maonesho ya wiki ya vijana atakayoyafungua rasmi tarehe 08 Oktoba, 2106 katika Uwanja wa Sabasaba Mjini Bariadi, ( kutoka kulia), Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Festo Kiswaga, Katibu Tawala mkoa wa Simiyu, Jumanne Sagini,  (kulia) Mkurugenzi wa Idara ya Vijana kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi , Vijana , Ajira na Wenye Ulemavu, Bw. Jemasi Kajugusi.
Waziri wa Nchi  Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi , Vijana , Ajira na Wenye Ulemavu , Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na Baadhi ya Viongozi na Watendaji wa Mkoa wa Simiyu baada ya kukagua sampuli ya mabanda takayotumiwa na vijana katika maonesho ya kazi zao wakati wa maonesho ya wiki ya vijana atakayoyafungua rasmi tarehe 08 Oktoba, 2106 katika Uwanja wa Sabasaba Mjini Bariadi, ( kutoka kulia), Kamanda wa Jeshi la Zimamoto Mkoa, Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Festo Kiswaga, Katibu Tawala mkoa wa Simiyu, Jumanne Sagini,  (kulia) Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa, Mkurugenzi wa Idara ya Vijana kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi , Vijana , Ajira na Wenye Ulemavu, Bw. Jemasi Kajugusi.

Waziri wa Nchi  Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi , Vijana , Ajira na Wenye Ulemavu , Mhe. Jenista Mhagama akimsikiliza Mkurugenzi wa Idara ya Vijana kutoka katika Ofisi yake Bw. Jemasi Kajugusi(wa kwanza kulia),  akiwa na Baadhi ya Viongozi na Watendaji wa Mkoa wa Simiyu baada ya kukagua sampuli ya mabanda  yatakayotumiwa na vijana katika maonesho ya kazi zao wakati wa maonesho ya wiki ya vijana atakayoyafungua rasmi tarehe 08 Oktoba, 2106 katika Uwanja wa Sabasaba Mjini Bariadi.



Vijana wa Halaiki wa Mkoa wa Simiyu wakitoa heshima mbele ya Waziri wa Nchi  Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi , Vijana , Ajira na Wenye Ulemavu , Mhe. Jenista Mhagama (hayupo pichani) alipowatembelea wakati wa ziara yake ya kukagua na kuona Maandalizi ya Maadhimisho ya Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru, Wiki ya Vijana na Kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa, yanayotarajiwa kufanyika mkoani humo tarehe 8 na 14 Oktoba  2016.


:Vijana wa Halaiki wa Mkoa wa Simiyu wakitoa heshima mbele ya Waziri wa Nchi  Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi , Vijana , Ajira na Wenye Ulemavu , Mhe. Jenista Mhagama (hayupo pichani) alipowatembelea wakati wa ziara yake ya kukagua na kuona Maandalizi ya Maadhimisho ya Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru, Wiki ya Vijana na Kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa, yanayotarajiwa kufanyika mkoani humo tarehe 8 na 14 Oktoba  2016 .

Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Jumanne Sagini (wa pili kushoto,  mbele)  akiwa na Viongozi wengine na Watendaji wa Mkoa wa Simiyu wakimsikiliza Waziri wa Nchi  Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi , Vijana , Ajira na Wenye Ulemavu , Mhe. Jenista Mhagama wakati alipotembea na kukagua Uwanja wa Halmashauri ya Mji Bariadi,  ambao utatumika katika maadhimisho ya Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru na Kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa, Oktoba 14, 2016. 

Baadhi ya Viongozi na Watendaji wa Mkoa wa Simiyu wakimsikiliza Waziri wa Nchi  Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi , Vijana , Ajira na Wenye Ulemavu , Mhe. Jenista Mhagama (hayupo pichani) katika kikao kilichofanyika Mjni Bariadi kwa lengo la kupata taarifa ya maandalizi ya Maadhimisho ya Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru, Wiki ya Vijana na Kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa, yanayotarajiwa kufanyika mkoani humo tarehe 8 na 14 Oktoba  2016 .
Baadhi ya Viongozi na Watendaji wa Mkoa wa Simiyu wakimsikiliza Waziri wa Nchi  Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi , Vijana , Ajira na Wenye Ulemavu , Mhe. Jenista Mhagama (hayupo pichani) katika kikao kilichofanyika Mjni Bariadi kwa lengo la kupata taarifa ya maandalizi ya Maadhimisho ya Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru, Wiki ya Vijana na Kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa, yanayotarajiwa kufanyika mkoani humo tarehe 8 na 14 Oktoba  2016 .

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!