MWENGE WA UHURU WAANZA MBIO ZAKE
MKOANI SIMIYU
Na
Stella Kalinga
Mwenge
wa Uhuru umepokelewa na kuanza mbio zake mkoani Simiyu, mkoa ambao kwa mujibu wa ratiba ni mwenyeji wa
kilele chake kitaifa kwa mwaka 2016 ukitokea mkoani Shinyanga.
Akitoa
taarifa ya mkoa kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2016 , George Mbijima
Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka , amesema Mkoa huo unatekeleza kwa
vitendo Ujumbe wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2016 inayosema “Vijana
ni nguvu kazi ya Taifa, Washirikishwe na kuwezeshwa’’ kwa kuwawezesha
vijana wote kutekeleza miradi ya maendeleo kupitia kauli mbiu ya Mkoa wa Simiyu ya “Wilaya
moja Bidhaa moja”.
Mtaka
amesema Mkoa umewahamasisha vijana kujiunga katika vikundi na kuwapatia mitaji katika
kutekeleza agizo la Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania la kuwa nchi
ya Viwanda.
“Utekelezaji
umeanza na Mkoa wa Simiyu tumejichagua kuwa mkoa wa utekelezaji, Utekelezaji huo
upo ambapo Wilaya ya Maswa kwenye hii kauli mbiu yetu ya 'wilaya moja bidhaa moja’ wanatengeneza chaki na
Meatu wanasindika maziwa”, alisema Mtaka.
Aidha,
Mtaka amesema kiwanda cha kuzalisha chaki cha Wilaya ya Maswa kitafunguliwa
rasmi na Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge,Vijana, Ajira,Kazi na
Wenye ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama (Mb), tarehe 10/10/2016 ambapo pia tarehe 11/10/2016 atafungua Kiwanda
cha kusindika maziwa Meatu.
Aidha
kuhusu ujumbe wa kudumu wa Mbio za Mwenge ; Serikali Mkoani Simiyu kwa
kushirikiana na wadau wengine katika kupambana na madawa ya kulevya chini ya
kaulimbiu ya “Tujenge jamii maisha na utu wetu;bila dawa za kulevya” imeendelea kutoa elimu na kuchukua hatua kwa
wasambazaji na watumiaji wa dawa za kulevya.
Katika
Mapambano dhidi ya UKIMWI chini ya kauli mbiu “Tanzania bila maambukizi mapya,
unyanyapaa na vifo vitokanavyo na UKIMWI; Inawezekana” Mtaka amesema mkoa unaendelea kutoa elimu na kuwahamasisha
wananchi kupima kwa hiari virusi vya Ukimwi ili waweze kutambua hali zao na
kujilinda na maambukizi mapya, kuachana na unyanyapaa na kuzuia vifo.
Kuhusu
mapambano dhidi rushwa chini ya kauli mbiu “Timiza wajibu wako; kata mnyororo
wa rushwa” Mtaka amesema TAKUKURU
kwa kushirikiana na Serikali za Mitaa inaendelea kuwachukulia hatua wote
wanaobainika kutoa na kupokea rushwa na
kutoa elimu kwa wananchi juu ya mapambano dhidi ya rushwa ikiwa ni pamoja na
kuelimisha kupitia klabu za wapinga rushwa mashuleni.
Sanjari
na hilo Mtaka pia amesema Mkoa wa Simiyu unaendelea kupambana na Malaria chini
ya Kauli mbiu “Wekeza katika Maisha ya baadaye; Tokomeza Malaria” kwa kuwahamasisha
wananchi kutumia vyandarua, kuua mazalia ya mbu na kwenda katika vituo vya
kutolea huduma za afya pindi wanapoona dalili za ugunjwa wa malaria.
Mhe.
Anthony Mtaka amesema Mwenge wa Uhuru ukiwa
mkoani humo utapita katika Halmashauri sita (6) ukianzia Halmashauri ya Wilaya
ya Maswa, Meatu, Itilima, Busega, Bariadi na Halmashauri ya Mji wa Bariadi kuona
miradi minne (4), kufungua miradi tisa
(9), kuweka jiwe la msingi miradi sita(06) na kuzindua miradi 11 ya maendeleo
katika sekta ya Afya, elimu, maji, kilimo, barabara, sekta binafsi na utawala
bora ambayo kwa ujumla wake ina thamani ya zaidi ya bilioni 12.
Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (kulia) akipokea Mwenge wa Uhuru
kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack (kushoto) katika kijiji cha Wigelekelo
wilayani Maswa ukitokea Kishapu Mkoani Shinyanga.
Kiongozi
wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2016, Ndg. George Mbijima akivikwa skafu na
Vijana wa Skauti wa Wilaya ya Maswa kabla ya kupokelelewa na Viongozi wa Mkoa
Simiyu, akitokea mkoani Shinyanga.
|
Mkuu
wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akimpokea Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru
mwaka 2016, Ndg. George Mbijima
Baadhi
ya Wakimbiza Mwenge Kitaifa wakisalimiana na viongozi wa Mkoa wa Simiyu wakati
wa mapokezi ya mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu yaliyofanyika katika kijiji cha
Wigelekelo wilayani Maswa.
|
Mkimbiza
Mwenge Kitaifa kutoka Mkoa wa Simiyu, James Munguji akisalimiana na baadhi ya
viongozi wa Mkoa wa Simiyu wakati wa mapokezi ya mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu
yaliyofanyika katika kijiji cha Wigelekelo wilayani Maswa.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(kushoto) akimkabidhi Mwenge wa Uhuru Mkuu wa wilaya ya Maswa, Dkt. Seif Shekalaghe mara baada ya kuupokea kutoka Shinyanga. |
Baadhi
ya Viongozi wa Mkoa wa Simiyu wakiwa tayari kushika Mwenge wa Uhuru mara baada
ya mapokezi ya Mwenge wa Uhuru kutoka Shinyanga.
|
0 comments:
Post a Comment