Monday, May 1, 2017

MEI MOSI SIMIYU: RC MTAKA AWATAKA VIONGOZI WASITOE KAULI ZA KUWAKATISHA TAMAA WATUMISHI

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka amewataka Viongozi Mkoani humo wasitoe kauli za kukatisha tamaa watumishi walio chini yao ili waweze kutekeleza majukumu yao vema ikiwa ni pamoja na kushiriki kikamilifu katika  Agenda ya Mkoa ya Ujenzi wa Uchumi wa Viwanda chini ya Kauli Mbiu"WILAYA MOJA BIDHAA MOJA”.

Mkuu wa Mkoa ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na Watumishi katika Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi (Mei Mosi) duniani yaliyofanyika kimkoa Lamadi Wilayani Busega.

Mtaka amesema Serikali Mkoani humo ina agenda katika Ujenzi wa Uchumi wa Viwanda ambayo ni kujenga Viwanda ambavyo malighafi yake yanapatikana hapa nchini.

Amesema  Serikali Mkoani imedhamiria kujenga  Mkoa utakaoonesha dira katika Ujenzi wa Uchumi wa Viwanda, utaotekeleza Ilani ya CCM, Dira ya Taifa,Mpango wa Taifa wa Miaka mitano, utakaotekeleza maono na matamanio ya Mhe Rais na  ili kutekeleza yote haya Viongozi wanahitaji  kuungwa mkono na watumishi wa Serikali.

“Sisi kama Mkoa tunahitaji kujenga Mkoa wetu kuwa  mkoa wa Viwanda kwa vitendo siyo kwa maneno, ili tuweze kujenga uchumi wa Viwanda ni lazima tuungwe mkono na wafanyakazi, ili tuungwe mkono na wafanyakazi ni lazima kauli zetu ziweze kujenga morali kwa wafanyakazi; hauwezi ukawa unataka kujenga uchumi wa viwanda Simiyu halafu unakuwa ni Mkurugenzi au Mkuu wa Idara mwenye lugha za hovyo kwa wafanyakazi ni vitu visivyowezekana” alisema

Ameongeza kuwa chini ya Kauli Mbiu ya “Wilaya Moja Bidhaa Moja” Serikali imepanga kuwa Wilaya ya Busega iwe na kiwanda cha  kutengeneza Tomato  sauce,Chilli Sauce na bidhaa zote za mbogamboga  ambazo zitauzwa katika mikoa ya Mwanza,Mara,Geita,Shinyanga,Kagera,Singida,Kigoma na Dar es Salaam.

Aidha amesema katika wilaya ya Itilima zitatengenezwa sabuni za maji,unga na za miche, wilaya ya Maswa Halmashauri itapata mkopo wa shilingi Bilioni 1.5 kwa ajili ya upanuzi wa kiwanda cha chaki na wilaya ya Meatu itapata shilingi bilioni 1.3 kwa ajili ya kupanua kiwanda cha maziwa ili maziwa ya unga yazalishwe pia.

Wakati huo huo Mtaka amesema Upembuzi yakinifu kwa ajili ya ujenzi wa Kiwanda cha Vifaa Tiba vitokanavyo na zao la Pamba umeanza kufanyika ambapo Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF), Benki ya TIB, Bohari ya Dawa ya Taifa(MSD),Shirika la Viwanda nchini (TBS) na Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) wamekuwa msaada mkubwa kuhakikisha ujenzi huu unafanyika.

Aidha, ameeleza kuwa mpaka sasa  Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa NSSF, Benki ya Azania na Taasisi ya SELF iliyo chini ya Wizara ya Fedha na Mipango wameonesha utayari wa kuunga mkono Mkoa wa Simiyu katika utekelezaji wa Falsafa ya Wilaya Moja Bidhaa Moja.

Ameongeza kuwa vitajengwa viwanda katika Halmashauri zote ili wananchi wote wanufaike na uwepo wa viwanda hivyo kwa ajira na maendeleo ya uchumi hivyo akawataka watumishi wa Umma wachangamkie fursa hizo wakati Serikali ikitekeleza miradi yote hiyo kujenga Uchumi wa Viwanda.

“ Simiyu tunatekeleza na tunataka mwaka 2020 wakati wa Uchaguzi Mkuu, kila wilaya atakayopita Mhe,Dkt.John Magufuli katika Mkoa wetu akute kura tulizoziandaa , hamasa ya wananchina imani thabiti,vijana na wakina mama ambao mazao yao yatakuwa yameongezewa thamani na viwanda vilivyo ndani ya wilaya zao” alisema.

Mtaka pia amewataka waajiri wote Mkoani humo kuacha tabia ya kuwakopa watumishi  hodari zawadi zao wakati wa Siku ya Wafanyakazi, na badala yake wahakikishe wanawapa kile wanachostahili na akawataka watumishi wote  kutekeleza majukumu yao kwa weledi ambapo amesema ambao watafedhehesha taaluma zao watachukuliwa hatua.

Kwa upande wake Mratibu wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi (Mei Mosi) Ndg. Catherine Nyingi akisoma risala kwa niaba ya watumishi wote amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka kwa kukomesha vitendo vya udharilishaji kwa Waumishi wa Umma vilivyokuwa vikifanywa na baadhi ya wananchi dhidi ya watumishi wa Umma vikiwemo uchapaji wa viboko hadharani, kuhukumiwa na mahakama za kimila (dagashida) na kupewa adhabu mbalimbali ikiwepo ya kutozwa fedha.

Nyingi pia amesema Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi linaomba Serikali iongeze kima cha chini cha mshahara, ishughulikie upandishaji wa madaraja, kulipa madeni ya watumishi na waajiri wapeleke michango ya watumishi wao katika Mifuko ya Hifadhi ya Jamii kwa wakati.


Kauli Mbiu ya Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi mwaka 2017 ambayo ni yameadhimishwa kwa mara ya tano saa mkoani Simiyu ni “UCHUMI WA VIWANDA UZINGATIE, HAKI, MASLAHI NA HESHIMA YA WAFANYAKAZI” 

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka(wa tano kulia) akiimba wimbo maalum wa mshikamano kwa watumishi wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi duniani yaliyofanyika kimkoa Lamadi Wilayani Busega. 
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka(wa pili kushoto) akipokea maandamano ya watumishi kutoka Vyama mbalimbali vya Wafanyakazi wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi yaliyofanyika kimkoa Lamadi Wilayani Busega.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka(kushoto) akimkabidhi zawadi ya cheti na fedha Katibu Muhtasi katika Ofisi yake bibi .Frolenciana Kagya,  ambaye amekuwa Mtumishi hodari (Ofisi ya Mkuu wa Mkoa) wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi duniani  yaliyofanyika kimkoa Lamadi Wilayani Busega.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka(kushoto) akimkabidhi zawadi ya cheti na fedha Afisa Tawala Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Itilima  ambaye amekuwa Mtumishi hodari (Ofisi hiyo) wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi duniani  yaliyofanyika kimkoa Lamadi Wilayani Busega.
 Baadhi ya walimu wakiwa katika maandamano wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi dunia yaliyofanyika kimkoa Lamadi Wilayani Busega.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka akicheza wimbo wa kabila la Kisukuma pamoja na baadhi ya watumishi na watoto wenye ualbino  kutoka kituo cha Bikira Maria Lamadi wilayani Busega Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi duniani yaliyofanyika kimkoa wilayani humo.


Baadhi ya Watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu wakiwa katika maandamano wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi duniani yaliyofanyika kimkoa Lamadi Wilayani Busega. 
Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe.Dkt.Seif Shekalaghe akiwasalimia Watumishi wa Mkoa wa Simiu na wananchi wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi duniani yaliyofanyika kimkoa Lamadi Wilayani Busega.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka akizungumza na Wafanyakazi na wananchi wa mkoa huo wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi duniani yaliyofanyika kimkoa Lamadi Wilayani Busega

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka(kushoto) akimkabidhi mmoja wa watoto Kituo cha  kulea watoto wenye Ualbino cha Bikira Maria Lamadi fedha zilizochangwa na Wafanyakazi kwa ajili ya watoto hao wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi duniani iliyofanyika kimkoa Lamadi Wilayani Busega, (kulia) ni mlezi wa watoto hao Sister Helena.
Baadhi ya Watumishi wakiwa katika maandamano wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi duniani yaliyofanyika kimkoa Lamadi Wilayani Busega.

Baadhi ya Watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu na Ofisi za Wakuu wa Wilaya wakiwa katika maandamano wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi duniani yaliyofanyika kimkoa Lamadi Wilayani Busega. 
Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Mhe.Joseph Chilongani akionesha maziwa yanayosindikwa wilayani humo kwa Wafanyakazi wa Mkoa wa Simiyu na wananchi wa Busega wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi duniani yaliyofanyika kimkoa wilayani humo

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka (wa tatu kushoto) akizungumza jambo na katibu wa CWT Mkoa Mwl.Said Mselema (kulia) wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi duniani yaliyofanyika kimkoa Lamadi Wilayani Busega.
 Baadhi ya Watumishi wa Wakala wa Barabara (TANROADS) Mkoa wa Simiyu wakiwa katika maandamano wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi duniani yaliyofanyika kimkoa Lamadi Wilayani Busega.

Kwaya ya Walimu wilaya ya Busega ikitoa burudani wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi duniani 
yaliyofanyika kimkoa Lamadi Wilayani humo.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka(kushoto) akimkabidhi zawadi ya cheti na fedha Afisa Tarafa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Bariadi  ambaye amekuwa Mtumishi hodari (wa Ofisi hiyo) wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi duniani yaliyofanyika kimkoa Lamadi Wilayani Busega.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka(mwenye fulana ya bluu kulia) akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi hodari kutoka katika Chama cha Walimu(CWT) pamoja na viongozi wa mbalimbali wa Mkoa huo.
Baadhi ya Watumishi wa Ofisi y Mkuu wa Mkoa wakiwa katika picha ya pamoja na Mfanyakazi Hodari wa Ofisi hiyo Bibi.Florenciana Kagya (wa nne kushoto) wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi duniani yaliyofanyika kimkoa Lamadi Wilayani Busega.


 Baadhi ya Watumishi wa Shirika la Ugavi wa Umeme (TANESCO) wakipita na gari lao wakati wa maandamano katika Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi duniani yaliyofanyika Kimkoa wilayani Busega.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!