Wednesday, December 6, 2017

WADAU WA MAENDELEO SIMIYU WAKUBALIANA NA UCHANGIAJI KATIKA UJENZI WA MIUNDOMBINU YA SHULE KUELEKEA MWAKA 2018

Wadau wa Maendeleo Mkoani Simiyu wamekubaliana na Uchangiaji wa Ujenzi wa Miundombinu ya shule Mkoani humo hususani vyumba vya madarasa katika shule za Msingi na Sekondari ili kukabiliana na upungufu uliopo, kutokana na ongezeko la wanafunzi watakaoanza darasa la kwanza na kidato cha kwanza mwaka 2018.

Makubaliano hayo yamefikiwa katika Kikao cha Ushauri wa Mkoa(RCC) kilichofanyika jana Mjini Bariadi.

Akifungua kikao hicho Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka amesema Mkoa huo unahitaji zaidi ya shilingi bilioni 10 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya shule hususani Vyumba vya madarasa , hivyo wananchi pamoja na wadau wengine wanaombwa kuchangia ujenzi huo.

Mtaka amesema hadi sasa wapo wadau kadhaa walioonesha nia ya kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa, matundu ya vyoo na nyumba za walimu kwa kutoa ahadi za vifaa vya ujenzi vikiwemo saruji na mabati.

Mbunge wa Jimbo la Bariadi, Mhe.John Chenge amesema suala la Elimu ni si la Serikali Kuu pekee bali ni pamoja na wananchi, Serikali za Mitaa pamoja na wadau wengine, hivyo wananchi wahamasishwe kuchangia ujenzi wa miundombinu hiyo kwa ajili ya maendeleo ya Elimu mkoani humo.

Akichangia hoja hiyo, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe.Enock Yakobo ameshauri kuwa hamasa ya ujenzi wa  miundombinu ya shule ifanywe na viongozi wote Mkoani humo,  ikiwezekana kwa kubadilishana maeneo ya kwenda kutoa hamasa ambayo ni tofauti na maeneo wanayofahamika zaidi.

“ Wakati  tunaanza ujenzi wa Shule za Kata tulikubaliana kuwa viongozi tubadilishane uzoefu kwa kila mmoja kwenda kuhamasisha maeneo ambayo wananchi hawawafahamu na hawajawazoea;  viongozi wa Wilaya ya Bariadi walienda Meatu, wa Meatu wakaenda Maswa, wa Maswa walienda Bariadi , lile jambo lilifanikiwa sana wananchi walihamasika wakachangia nashauri tutumie pia mfumo huu tutafanikiwa”alisema.

Kaimu Afisa Elimu Mkoa wa Simiyu, Ndg.Charles Maganga amesema Wanafunzi wanaotarajia kuingia darasa la kwanza mwaka 2018 ni 109,899 wakati waliomaliza darasa la saba ni 30,898 hali inayosababisha mahitaji mapya ya vyumba vya madarasa 1757 na madawati 26,334; wanaotarajia kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2018 ni 20,818 waliohitimu kidato cha nne 6195 mahitaji mapya ya vyumba vya madarasa ni 367 na madawati 14,623.

Aidha, Mkuu wa Wilaya ya Maswa,Mhe.Dkt. Shekalaghe ametoa wito kwa viongozi wenzake kuwahamasiha wazazi kuchangia chakula kwa ajili ya watoto wao ili waweze kupatiwa chakula cha mchana kwa shule ambazo bado hazijaanza kufanya hivyo, jambo na  ambalo liliungwa mkono na viongozi wengi

Kuhusu suala la mimba shuleni Mkuu wa Mkoa  wa Simiyu Mhe.Anthony Mtaka amesema Serikali Mkoani humo itaendelea kuwachukulia hatua kali za kisheria wale wote watakaobainika kuwapa mimba wanafunzi wa kike.

Mtaka amesema Serikali Mkoani humo imedhamiria  na kuweka mikakati madhubuti ya kuwalinda watoto wa kike ikiwa ni pamoja na  kujenga mabweni kwa ajili ya wasichana katika shule zote za kata, ili kuwasaidia kuondokana na vishawishi wanavyoweza kuvipata kutokana na kutembea mwendo mrefu.


Mtaka pia alitumia kikao hicho kuwajulisha viongozi na wadau wa Maendeleo Mkoani Simiyu kuwa Mkoa huo umepewa heshima ya kuwa mwenyeji wa Mahafali ya 34 ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania mwaka 2018, hivyo akawataka kujiandaa kwa ajili ya tukio hilo ambalo litaleta watu zaidi ya 1500 kutoka maeneo mbalimbali hapa nchini.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka akifungua kikao cha Kamati yaUshauri ya Mkoa huo(RCC), kilichofanyika jana Mjini Bariadi, (kushoto)Mbunge wa Bariadi Mhe. Andrew Chenge,(wa pili kushoto) Katibu Tawala mkoa Simiyu, Ndg.Jumanne Sagini na ( kulia) Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe.Festo Kiswaga.
Baadhi ya wajumbe wakifuatilia masuala mbalimbali yaliyokuwa yakiwasilishwa katika Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) wa Simiyu kilichofanyia jana Mjini Bariadi.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo akichangia hoja katika Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichofanyia jana Mjini Bariadi.
Mbunge wa Jimbo la Itilima, Mhe.Njalu Silanga akichangia hoja katika Kikao Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC)  Mkoani Simiyu kilichofanyia jana Mjini Bariadi.
Baadhi ya wajumbe wakifuatilia masuala mbalimbali yaliyokuwa yakiwasilishwa katika Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) wa Simiyu kilichofanyia jana Mjini Bariadi.
Kaimu Afisa Elimu Mkoa wa Simiyu, Ndg Charles Maganga akiwasilisha taarifa ya Mkoa ya  Maendeleo ya Elimu katika Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa(RCC), kilchofanyika jana Mjini Bariadi.
Meneja wa AGPAHI Kanda ya Ziwa, Dkt.Nkingwa Mabelele akiwasilisha taarifa ya utendaji kazi wa Shirika hilo ambao wadau wa Afya Mkoani Simiyu, katika Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa(RCC), kilchofanyika jana Mjini Bariadi.
Mbunge wa Jimbo la Bariadi, Mhe.Andrew Chenge akichangia hoja katika Kikao Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC)  Simiyu kilichofanyia jana Mjini Bariadi.
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Maswa, Mhe.Paul Jidayi akichangia hoja katika Kikao Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC)  Simiyu kilichofanyia jana Mjini Bariadi.
Katibu Tawala Msaidizi wa Huduma zaMaji kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhandisi.Hatari Kapufi akiwasilisha Taarifa ya Huduma za Maji Mkoa, katika Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa(RCC), kilchofanyika jana Mjini Bariadi.
Mchungaji wa Kanisa la Waadventista Wasabato (SDA) Bariadi, Mashauri Bahini akichangia hoja katika Kikao Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC)  Simiyu kilichofanyia jana Mjini Bariadi.
Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe.Dkt.Seif Shekalaghe akichangia hoja katika Kikao Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC)  Simiyu kilichofanyia jana Mjini Bariadi.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Itilima, Ndg.Mariano Mwanyigu akichangia hoja katika Kikao Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC)  Simiyu kilichofanyia jana Mjini Bariadi.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Bariadi, Mhe.Robert Lweyo akichangia hoja katika Kikao Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC)  Simiyu kilichofanyia jana Mjini Bariadi.
Kaimu Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Uchumi na Uzalishaji katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Dkt.Gamitwe Mahaza akiwasilisha Taarifa ya Mkoa ya Maendeleo ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, katika Kikao Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichofanyia jana Mjini Bariadi.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt. Mageda Kihulya akiwasilisha Taarifa ya Afya ya Mkoa, katika Kikao Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichofanyia jana Mjini Bariadi.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!