Tuesday, May 10, 2016

RC SIMIYU APIGA MARUFUKU DAGA SHIDA



Mkuu wa Simiyu Mhe. Anthony J. Mtaka amepiga marufuku tabia ya viongozi wa kimila kuwaadhibu wananchi  wanaobanika kuwa kuwa na makosa kupita mabaraza ya kimila maaarufu  kama DAGA SHIDA na badala yake amewataka  watumie vyombo vya Serikali vinavyotambulika kisheria.

Mtaka alitoa agizo hilo alipozungumza na wananchi wa kijiji cha Ikindilo kata ya Ikindilo tarafa ya Bumela wilayani Itilima, ambapo ameitaka Kamati ya Ulinzi na Usalama wilayani Itilima, kulisimamia suala hilo kwa kuwa limekuwa likiwadharirisha wananchi na wale watakaobainika kukaidi agizo hilo, wafikishwe kwenye vyombo vya sheria na kuchukuliwa hatua.

“Mkuu wa Wilaya na wajumbe wako kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya, simamieni suala hili na mhakikishe linakomeshwa kabisa. Naagiza  hili kwa mkoa mzima sitaki kusikia kitu kinachoitwa daga shida. Hatuwezi kuacha wananchi wanateseka, watumishi wetu tunaowaleta kuwatumikia wananchi nao wanateseka na mifumo kandamizi kama hii wakati vyombo vyetu vya ulinzi na usalama vipo”alisema Mtaka 

Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa aliwataka wananchi watakaoitwa kwa ajili ya kwenda kuadhibiwa na viongozi wa mabaraza ya kimila maarufu kama Sumbantale wasikubali na wawatake viongozi hao wa kimila kuwashtaki  katika ofisi za Serikali au katika Vituo vya polisi ikiwa watajiridhisha kuwa wana makosa.
Mfumo wa daga shida umekuwa ukitumwa katika maeneo mengi mkoani Simiyu, ambapo wananchi  hususani watumishi wa umma wamekuwa wakiadhibiwa na viongozi wa kimila kwa kuwataka kulipa faini ya fedha , mazao, wanyama  na kupigwa pale wanapoonekana kwenda kinyume na matakwa yao ya kimila na wakati mwingine wamekuwa wakizushiwa .

Wakati huo huo Mtaka amewataka  wazazi na walezi kuacha mara moja tabia ya  kuwakatisha masomo watoto wao wa kike na kuwaozesha kwa kuwa wakiendelea kufanya hivyo watachukuliwa hatua kali za kisheria.

“Ole wake mzazi au mlezi atakayemtoa mtoto shule  na akaenda kumuozesha,ajue ameamua kuhamishia maisha yake toka nyumbani kwenda jela, hilo halina mjadala. Mtoto wa shule ni wako kwa kuwa umemzaa lakini akiwa shule toka darasa la kwanza  mpaka kidato cha sita ni mali ya serikali” alisema Mtaka.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!