Thursday, September 14, 2017

BAADA YA KIWANDA CHA CHAKI SIMIYU YAJIPANGA TENA UPANUZI KIWANDA CHA MAZIWA, UJENZI WA KIWANDA CHA NYANYA NA PILIPILI

Baada ya mikakati ya upanuzi wa kiwanda cha kutengeneza chaki Wilayani Maswa, Mkoa wa Simiyu umejipanga tena kufanya upanuzi wa Kiwanda cha kusindika Maziwa kilichopo Wilayani Meatu na Ujenzi wa kiwanda cha kusindika Nyanya na Pilipili wilayani Busega.

Hatua hiyo imefikiwa kufuatia zoezi la upembuzi yakinifu kwa viwanda hivyo lililofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF) kwa Ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa(UNDP), kukamilika na taarifa yake kuwasilishwa kwa Viongozi na wadau wa Maendeleo Mkoani Simiyu katika kikao kilichofanyika Mjini Bariadi.

Akiwasilisha taarifa ya Upembuzi Yakinifu wa Upanuzi wa Kiwanda cha Maziwa Wilayani Meatu, Profesa Lusato Kurwijila kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine(SUA) amesema Tanzania inazalisha maziwa lita bilioni 2.1 kwa mwaka, lakini yanayopelekwa viwandani kusindikwa ni asilimia tatu ya maziwa yote, kutokana na ukosefu wa miundombinu ya kukusanyia maziwa.

Amesema upanuzi wa kiwanda cha Maziwa Meatu ni mradi unaotekelezeka hivyo ni vema ukafanyika uwekezaji katika ufugaji wa kisasa ili kupata maziwa ya kutosha, miundombinu ya  kukusanyia na kupozea maziwa,  kuwahamasisha wafugaji kuunda vyama vya ushirika ambavyo vitamiliki na kuendesha vituo vya kukusanyia maziwa na kutoa ajira kwa wananchi hususani vijana na wanawake.

Akizungumzia uanzishwaji wa Kiwanda cha kusindika Nyanya na Pilipili, Mtaalam  wa Bustani  na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine(SUA) Profesa Theodosy  Msogoya amesema, mradi huo unaweza kutekelezwa kwa mafanikio, hivyo ametoa wito kwa Serikali kuajiri watalaam wa Bustani na kuwahamasisha wakulima kujiunga katika vikundi ili waweze kukopesheka.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine(SUA) Profesa Jeremia Makindara amesema, uwepo wa fursa mbalimbali ikiwa ni pamoja na utashi wa kisiasa,upatikanaji wa malighafi, nguvu kazi, maji, kiwanda kujengwa katika njia kuu ya usafirishaji (barabara ya Mwanza-Musoma), upatikanaji wa soko la uhakika kutasaidia kukiletea kiwanda hicho faida.

Kwa upande wao Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega, Anderson Njiginya na Mkurugenzi wa Wilaya ya Meatu, Ndg. Fabian Manoza wamesema, viwanda hivyo vitakuwa vyanzo vipya vya mapato kwa Halmashauri zao na kuwasaidia wananchi kupata ajira na kukukuza uchumi wao.

Katika hatua nyingine Mkurugenzi wa UNDP hapa nchini Ndg, Amoni Manyama ametoa wito kwa Serikali Mkoani Simiyu kuona namna ya kuwashirikisha wanufaika wa TASAF katika maendeleo ya viwanda na kuhakikisha kuwa makundi yote hususani wanawake yanashirikishwa na kunufaika na uanzishwaji wa viwanda hivyo.

 Naye Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka amesema watayafanyia kazi yote yaliyoanishwa katika Tafiti zilizofanywa na Watalaam hao kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam(UDSM) na Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine(SUA)na upembuzi yakinifu huo na kuyaweka katika matendo.

“Tumekuwa ni mkoa ambao tunawashirikisha wataalam kutoka katika vyuo vyetu, dhamira yetu ni kuona matokeo na position(Nafasi) yetu kama Mkoa ni kujipanga  kimkakati na mpango kazi wetu, dira ya mkoa na tunasema  kwenye miaka mitatu tutatekeleza” alisema Mtaka.

Aidha, Mtaka amesema Serikali Mkoani humo iko tayari kushirikiana na sekta binafsi katika uwekezaji, hivyo ametoa wito kwa Watanzania walio tayari kuwekeza Mkoani humo kwa kushirikiana na Halmashauri ambazo zimeanzisha miradi hiyo ya viwanda.

Sambamba na hilo amezishukuru Taasisi za Fedha zilizo tayari kufanya kazi na Mkoa wa Simiyu katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ukiwepo mradi wa kilimo cha Umwagiliaji wilayani Busega hususani Benki ya Maendeleo ya Kilimo(TADB) ambayo imesema iko tayari kufanya kazi na Mkoa huo, katika miradi mbalimbali ya Kilimo.

Upembuzi yakinifu wa ujenzi wa kiwanda cha kusindika nyanya na pilipili wilayani Busega na Upanuzi wa Kiwanda cha Maziwa wilayani Meatu uliofanywa na Wataalam kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam(UDSM) na Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine(SUA) chini ya Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii(ESRF) ulianza kufanyika Mwezi Julai mwaka huu na kukamilika mapema mwezi Septemba.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka(katikati) akizungumza na Viongozi na wadau wa maendeleo mkoani humo katika kikao kilichofanyika Mjini Bariadi kwa ajili ya kuwasilisha taarifa ya Upembuzi Yakinifu wa Ujenzi wa Kiwanda cha kusindika Nyanya na Pilipili Busega na Upanuzi wa Kiwanda cha Maziwa Meatu, uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Kiuchumi na Kijamii(ESRF) Kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP).
Mkurugenzi wa Shirika la Maendeleo ya Umoja wa Mataifa (UNDP) hapa nchini Ndg.Amoni Manyama (kushoto) akizungumza na Viongozi na wadau wa maendeleo mkoani Simiyu katika kikao kilichofanyika Mjini Bariadi kwa ajili ya kuwasilisha taarifa ya Upembuzi Yakinifu wa Ujenzi wa Kiwanda cha kusindika Nyanya na Pilipili Busega na Upanuzi wa Kiwanda cha Maziwa Meatu, uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Kiuchumi na Kijamii(ESRF) uliofadhili na shirika hilo.
Mtaalam wa Maziwa na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine(SUA), Profesa Lusato Kurwijila akiwasilisha taarifa ya Upembuzi Yakinifu wa Upanuzi wa Kiwanda cha Maziwa Meatu, uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Kiuchumi na Kijamii(ESRF) Kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), kwa viongozi na wadau wa maendeleo wa Mkoa wa Simiyu.
Mtaalam wa Uchumi na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dkt.Mutahyoba Baisi akiwasilisha taarifa ya Upembuzi Yakinifu wa Upanuzi wa Kiwanda cha Maziwa Meatu, uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Kiuchumi na Kijamii(ESRF) Kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), kwa viongozi na wadau wa maendeleo wa Mkoa wa Simiyu.
Mtaalam  wa Kilimo na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine(SUA) Profesa Theodosy T. Msogoya akiwasilisha taarifa ya Upembuzi Yakinifu wa Upanuzi wa Kiwanda cha Maziwa Meatu, uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Kiuchumi na Kijamii(ESRF) Kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), kwa viongozi na wadau wa maendeleo wa Mkoa wa Simiyu.
Mhandisi na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine(SUA) Profesa  Benard  Chove akiwasilisha taarifa ya Upembuzi Yakinifu wa Upanuzi wa Ujenzi wa Kiwanda cha kusindika Nyanya na Pilipili, uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Kiuchumi na Kijamii(ESRF) Kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), kwa viongozi na wadau wa maendeleo wa Mkoa wa Simiyu.
Mkurugenzi wa Vipind na uzalishaji wa Clouds Media, Ruge Mutahaba(kulia) akichangia hoja katika kikao kilichofanyika Mjini Bariadi kwa ajili ya kuwasilisha taarifa ya Upembuzi Yakinifu wa Ujenzi wa Kiwanda cha kusindika Nyanya na Pilipili Busega na Upanuzi wa Kiwanda cha Maziwa Meatu, uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Kiuchumi na Kijamii(ESRF) Kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, mhe.Festo Kiswaga.
Mhadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine(SUA), Dkt. Jeremia Makindara akizungumza na waandishi wa Habari baada ya kuwasilisha taarifa ya Upembuzi Yakinifu wa Upanuzi wa Ujenzi wa Kiwanda cha kusindika Nyanya na Pilipili, uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Kiuchumi na Kijamii(ESRF) Kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), kwa viongozi na wadau wa maendeleo wa Mkoa wa Simiyu.
Mkuu wa Wilaya ya Meatu , Mhe.Dkt.Joseph Chilongani akichangia hoja katika kikao kilichofanyika Mjini Bariadi kwa ajili ya kuwasilisha taarifa ya Upembuzi Yakinifu wa Ujenzi wa Kiwanda cha kusindika Nyanya na Pilipili Busega na Upanuzi wa Kiwanda cha Maziwa Meatu, uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Kiuchumi na Kijamii(ESRF) Kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP).
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, Ndg.Fabian Manoza akichangia hoja katika kikao kilichofanyika Mjini Bariadi kwa ajili ya kuwasilisha taarifa ya Upembuzi Yakinifu wa Ujenzi wa Kiwanda cha kusindika Nyanya na Pilipili Busega na Upanuzi wa Kiwanda cha Maziwa Meatu, uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Kiuchumi na Kijamii(ESRF) Kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP).
Mkuu wa Wilaya ya Busega  Mhe.Tano Mwera akichangia hoja katika kikao kilichofanyika Mjini Bariadi kwa ajili ya kuwasilisha taarifa ya Upembuzi Yakinifu wa Ujenzi wa Kiwanda cha kusindika Nyanya na Pilipili Busega na Upanuzi wa Kiwanda cha Maziwa Meatu, uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Kiuchumi na Kijamii(ESRF) Kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP)
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa, Dkt.Fredrick Sagamiko akichangia hoja katika kikao kilichofanyika Mjini Bariadi kwa ajili ya kuwasilisha taarifa ya Upembuzi Yakinifu wa Ujenzi wa Kiwanda cha kusindika Nyanya na Pilipili Busega na Upanuzi wa Kiwanda cha Maziwa Meatu, uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Kiuchumi na Kijamii(ESRF) Kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP).
Mkurugenzi wa FURSA, Suma Mwaitenda akichangia hoja katika kikao kilichofanyika Mjini Bariadi kwa ajili ya kuwasilisha taarifa ya Upembuzi Yakinifu wa Ujenzi wa Kiwanda cha kusindika Nyanya na Pilipili Busega na Upanuzi wa Kiwanda cha Maziwa Meatu, uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Kiuchumi na Kijamii(ESRF) Kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP).
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Buseg, Ndg.Anderson  Njiginya akichangia hoja katika kikao kilichofanyika Mjini Bariadi kwa ajili ya kuwasilisha taarifa ya Upembuzi Yakinifu wa Ujenzi wa Kiwanda cha kusindika Nyanya na Pilipili Busega na Upanuzi wa Kiwanda cha Maziwa Meatu, uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Kiuchumi na Kijamii(ESRF) Kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP).
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya yaItilima, Ndg.Mariano Mwanyigu akichangia hoja katika kikao kilichofanyika Mjini Bariadi kwa ajili ya kuwasilisha taarifa ya Upembuzi Yakinifu wa Ujenzi wa Kiwanda cha kusindika Nyanya na Pilipili Busega na Upanuzi wa Kiwanda cha Maziwa Meatu, uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Kiuchumi na Kijamii(ESRF) Kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP).
Baadhi ya viongozi na wadau wa maendeleo Mkoani Simiyu wakifuatilia taarifa ya Upembuzi Yakinifu wa Ujenzi wa Kiwanda cha kusindika Nyanya na Pilipili Busega na Upanuzi wa Kiwanda cha Maziwa Meatu, uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Kiuchumi na Kijamii(ESRF) Kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), iliyowasilishwa katika kikao maalum Mjini Bariadi.
Baadhi ya viongozi na wadau wa maendeleo Mkoani Simiyu wakifuatilia taarifa ya Upembuzi Yakinifu wa Ujenzi wa Kiwanda cha kusindika Nyanya na Pilipili Busega na Upanuzi wa Kiwanda cha Maziwa Meatu, uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Kiuchumi na Kijamii(ESRF) Kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), iliyowasilishwa katika kikao maalum Mjini Bariadi.
Baadhi ya viongozi na wadau wa maendeleo Mkoani Simiyu wakifuatilia taarifa ya Upembuzi Yakinifu wa Ujenzi wa Kiwanda cha kusindika Nyanya na Pilipili Busega na Upanuzi wa Kiwanda cha Maziwa Meatu, uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Kiuchumi na Kijamii(ESRF) Kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), iliyowasilishwa katika kikao maalum Mjini Bariadi.
 Meneja wa Kitengo cha Kukuza Biashara kutoka Benki ya Maendeleo ya Kilimo(TADB)  akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuwasilishwa kwa  taarifa ya Upembuzi Yakinifu wa Upanuzi wa Ujenzi wa Kiwanda cha kusindika Nyanya na Pilipili, uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Kiuchumi na Kijamii(ESRF) Kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), kwa viongozi na wadau wa maendeleo wa Mkoa wa Simiyu.
Wataalam  kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Chuo Kikuu cha Kilimo (SUA) wakifuatilia mjadala wa viongozi na wadau wa maendeleo Mkoani Simiyu, katika kikao kilichofanyika Mjini Bariadi baada ya kuwasilishwa kwa  taarifa ya Upembuzi Yakinifu wa Upanuzi wa Ujenzi wa Kiwanda cha kusindika Nyanya na Pilipili, uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Kiuchumi na Kijamii(ESRF) Kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), kwa viongozi na wadau wa maendeleo wa Mkoa wa Simiyu.
Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya Nickson Simon kutoka FURSA akichangia hoja katika kikao kilichofanyika Mjini Bariadi kwa ajili ya kuwasilisha taarifa ya Upembuzi Yakinifu wa Ujenzi wa Kiwanda cha kusindika Nyanya na Pilipili Busega na Upanuzi wa Kiwanda cha Maziwa Meatu, uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Kiuchumi na Kijamii(ESRF) Kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP).
Daktari wa Mifugo wa Halmashuri ya Wilaya ya Itilima Faustine Musoke akichangia hoja katika kikao kilichofanyika Mjini Bariadi kwa ajili ya kuwasilisha taarifa ya Upembuzi Yakinifu wa Ujenzi wa Kiwanda cha kusindika Nyanya na Pilipili Busega na Upanuzi wa Kiwanda cha Maziwa Meatu, uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Kiuchumi na Kijamii(ESRF) Kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP).
Ndg.Hassan Ngoma kutoka FURSA akichangia hoja katika kikao kilichofanyika Mjini Bariadi kwa ajili ya kuwasilisha taarifa ya Upembuzi Yakinifu wa Ujenzi wa Kiwanda cha kusindika Nyanya na Pilipili Busega na Upanuzi wa Kiwanda cha Maziwa Meatu, uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Kiuchumi na Kijamii(ESRF) Kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP).

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!