Wednesday, September 20, 2017

WAKURUGENZI WA MIFUKO, MASHIRIKA WATEMBELEA MAENEO YA UWEKEZAJI WA KIWANDA CHA BIDHAA ZA HOSPITALI, MAJI TIBA SIMIYU

Baadhi ya Wakurugenzi wa Mifuko na Mashirika ya Serikali hapa nchini wametembelea na kukagua maeneo yanayokusudiwa kutumika  katika ujenzi wa kiwanda kikubwa  cha kutengeneza  bidhaa zinazotumika hospitalini zitokanazo na  zao la pamba na kiwanda cha maji tiba(drip) mkoani SIMIYU.

Maeneo yaliyotembelewa ni kijiji cha Nyamikoma  Halmashauri ya Wilaya Busega ,kijiji cha Isenga Halmashauri ya Wilaya Bariadi  na  Mtaa wa  Katenga Halmashauri ya  Mji wa Bariadi.

Akizungumza katika kikao cha majumuisho ya ziara hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania(TIRDO), Profesa Mkumbukwa Mtambo amesema kuanzishwa kwa viwanda hivyo kutasaidia kuokao fedha takribani shilingi bilioni 19 zinazotumika kununua maji tiba na shilingi bilioni 29 kununua bidhaa za hospitali zitokanazo na pamba kwa mwaka, ambavyo vyote kwa sasa vinanunuliwa nje ya nchi.

Profesa Mtambo ameongeza kuwa pamoja na kuokoa fedha viwanda hivyo vitatoa ajira za moja kwa moja kwa Watanzania 1600 na ajira nyingine 5000 hivyo vitachangia katika kupunguza changamoto ya ukosefu wa ajira kwa wananchi wa Mkoa wa Simiyu na Tanzania kwa ujumla.

Aidha, amefafanua kuwa upembuzi yakinifu kwa ajili ya ujenzi wa viwanda hivi vyote viwili utkaofanywa na TIRDO unatarajia kuanza wiki sita kuanzia sasa, hivyo akawaeleza viongozi wa Mkoa wa Simiyu kuwa mara baada ya kukamilika kwa zoezi hilo watawasilisha taarifa itakayosaidia pia kuwaandaa wakulima kuzalisha pamba itakayohitajika kwa ajili kiwanda cha bidhaa za afya zitokanazo na pamba.

Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa(MSD), Laurean Rugambwa amesema jumla ya lita 1,500,000 za maji tiba(drip) hutumika hapa nchini kwa mwaka, ambayo huagizwa nje ya nchi hivyo ameuhakikishia uongozi wa Mkoa kuwa bidhaa zitakazozalishwa katika viwanda hivyo zitapata soko la uhakika kwa kuwa zitanunuliwa na Bohari hiyo kwa ajili ya matumizi ya vituo mbalimbali vya kutolea huduma za Afya hapa nchini.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF) Bernard Kaonga amesema wanaunga mkono ujenzi wa viwanda hivyo na wamekubali kuingia kwenye ubia na TIRDO pamoja na wadau wengine kama wadau wakubwa wa afya, kwa kuwa viwanda hivyo vitasaidia kupunguza gharama ya kuagiza  bidhaa hizo nje ya nchi.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka amesema ni vizuri Mkoa ukapata mapema taarifa ya Upembuzi yakinifu wa kiwanda cha bidhaa za Hospitali zitokanazo na pamba ili kuendana na maandalizi ya msimu wa kilimo cha pamba, ambapo amesisitiza kuwa mkoa huo umejipanga kuongeza uzalishaji kutoka kilo milioni 70 mpaka kilo milioni 130 kwa mwaka 2018.  

Ameongeza kuwa viwanda hivi vitakuwa na manufaa makubwa kwa wanachi wa mkoa huo ikiwepo suala la ajira  kwa watu zaidi ya 6500 wanatarajiwa kuajiriwa katika kiwanda kitakachozalisha bidhaa za hospitali zitokanazo na zao la pamba.

“Kwa watu wa Simiyu kupata mradi utakaoajiri watu 1500 moja kwa moja, ajira nyingine 5000 pamoja na ajira za kwenye (ginneries) viwanda vyetu vya kuchambua pamba tutakuwa tumefanya kitu; ni lazima tutengeneze kura mpya za Mhe.Rais mwaka 2020, maana wapiga kura wengi wa mwaka 2020 watakuwa wapya ambao hitaji lao kubwa ni ajira na katika umri wetu huu ni lazima tujibu” amesema Mtaka.

Naye Katibu Tawala Mkoa Simiyu, Ndg.Jumanne Sagini amesema Wakurugenzi wa Halmashauri, Madiwani, Viongozi wa Serikali za Vijiji na Mitaa na wananchi maeneo yote yaliyotembelewa wamekubali kutoa maeneo hayo kwa ajili ya uwekezaji wa viwanda, hivyo ni vema maamuzi ya mahali viwanda hivyo viwili vitakapojengwa yakatolewa mapema na wawekezaji hao ili  yaweze kuandaliwa  hati miliki.


Wabia wakuu katika Ujenzi wa Kiwanda cha kutengeneza bidhaa za hospitali zitokanazo na pamba na kiwanda cha kutengeneza maji tiba(maji ya drip) Mkoani Simiyu ni pamoja na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF),Bohari ya Dawa(MSD),Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA),Shirika la Viwango nchini(TBS), Benki ya Maendeleo(TIB),Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi(WCF), NEMC,TEMDO na Shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania(TIRDO) ambao ndiyo wasimamizi wa Miradi hiyo.
Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka(wa nne kushoto) akiwaongoza baadhi ya Wakurugenzi wa Mifuko na Mashirika pamoja na viongozi wa Mkoa huo katika ziara ya kutembelea na kuona maeneo yanayokusudiwa kujenga kiwanda cha bidhaa za Hospitali zitokanazo na pamba pamoja na maji tiba Mkoani Simiyu.
Afisa Mipango Miji wa Halmasahuri ya Wilaya ya Busega. Yoram Salum (kushoto) akitoa taarifa ya eneo lililotengwa kwa ajili ya viwanda katika kijiji cha Nyashimo  wakati wa ziara ya Wakurugenzi wa Mifuko na Mashirika pamoja na viongozi wa Mkoa wa Simiyu waliyofanya  kwa lengo la kuona maeneo kinapoweza kujengwa kiwanda cha bidhaa za Hospitali zitokanazo na pamba na kiwanda cha maji tiba Mkoani Simiyu
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Bariadi, Ndg.Melkizedeck Humbe akitoa maelezo juu ya eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa viwanda  Mtaa wa Katenga  wakati wa ziara ya Wakurugenzi wa Mifuko na Mashirika waliyofanya kwa lengo la  kuona maeneo kinapoweza kujengwa kiwanda cha bidhaa za Hospitali zitokanazo na pamba na kiwanda cha  maji tiba Mkoani Simiyu.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, Ndg.Abdallah Malela akitoa maelezo juu ya eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa viwanda katika Kijiji cha Isenge wakati wa ziara ya Wakurugenzi wa Mifuko na Mashirika waliyofanyakwa lengo la   kuona maeneo kinapoweza kujengwa kiwanda cha bidhaa za Hospitali zitokanazo na pamba na kiwanda cha  maji tiba Mkoani Simiyu. 
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka akizungumza na Wakurugenzi wa Mifuko na Mashirika(baadhi hawapo pichani) katika majumuisho ya Ziara iliyofanyika katika Halmashauri ya Mji Bariadi, Halmashauri ya Wilaya Bariadi na Busega iliyofanyika kwa lengo la kuona maeneo ya kujenga  kiwanda cha bidhaa za Hospitali zitokanazo na pamba na kiwanda cha  maji tiba Mkoani Humo.
Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Ndg.Jumanne Sagini  akizungumza na Wakurugenzi wa Mifuko na Mashirika na katika majumuisho ya Ziara iliyofanyika katika Halmashauri ya Mji Bariadi, Halmashauri ya Wilaya Bariadi na Busega iliyofanyika kwa lengo la kuona maeneo ya kujenga  kiwanda cha bidhaa za Hospitali zitokanazo na pamba na kiwanda cha  maji tiba Mkoani Simiyu.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda, Prof.Mkumbukwa Mtambo akizungumza na Viongozi wa Mkoa wa Simiyu katika majumuisho ya Ziara iliyofanyika katika Halmashauri ya Mji Bariadi, Halmashauri ya Wilaya Bariadi na Busega iliyofanyika kwa lengo la kuona maeneo ya kujenga  kiwanda cha bidhaa za Hospitali zitokanazo na pamba na kiwanda cha  maji tiba mkoani Simiyu.
 Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF), Bernard Konga akizungumza na Viongozi wa Mkoa wa Simiyu katika majumuisho ya Ziara iliyofanyika katika Halmashauri ya Mji Bariadi, Halmashauri ya Wilaya Bariadi na Busega iliyofanyika kwa lengo la kuona maeneo ya kujenga  kiwanda cha bidhaa za Hospitali zitokanazo na pamba na kiwanda cha  maji tiba Mkoani Simiyu.
Baadhi ya Wakurugenzi wa Mifuko na Mashirika pamoja na viongozi wa Mkoa wa Simiyu walipotembelea kiwanda cha kuchakata pamba cha Alliance Ginneries kilichopo Kasoli wilayani Bariadi wakati wa ziara yao iliyofanyika kwa lengo la kuona maeneo ya kujenga  kiwanda cha bidhaa za Hospitali zitokanazo na pamba na kiwanda cha  maji tiba Mkoani Simiyu.

Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe.Festo Kiswaga akitoa maelezo juu ya eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa viwanda katika Mtaa waKatengawakati wa ziara ya Wakurugenzi wa Mifuko na Mashirika waliyofanya kwa lengo la   kuona maeneo ya kujenga kiwanda cha bidhaa za Hospitali zitokanazo na pamba na kiwanda cha  maji tiba Mkoani Simiyu.
Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa ya Taifa(MSD), Ndg Laurean Rugambwa akizungumza katika kikao cha majumuisho ya ziara ya Wakurugenzi wa Mifuko na Mashirika waliyofanya kwa lengo la   kuona maeneo ya kujenga kiwanda cha bidhaa za Hospitali zitokanazo na pamba na kiwanda cha  maji tiba Mkoani Simiyu.
Mkurugenzi Mkuu wa mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi( WCF) Ndg .Masha Mshomba akizungumza katika kikao cha majumuisho ya ziara ya Wakurugenzi wa Mifuko na Mashirika waliyofanya kwa lengo la   kuona maeneo ya kujenga kiwanda cha bidhaa za Hospitali zitokanazo na pamba na kiwanda cha  maji tiba Mkoani Simiyu.
Wakurugenzi wa Mifuko na Mashirika pamoja na Viongozi wa mkoa wa Simiyu  wakipokea maelezo ya namna wanavyozalisha Mbegu za pamba kitaalam kutoka Mtaalam wa Kampuni ya Alliance Ginneries wakati walipotembelea kiwanda hicho baada ya kuona maeneo ya kujenga kiwanda cha bidhaa za Hospitali zitokanazo na pamba na kiwanda cha  maji tiba Mkoani Simiyu.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka akiwaonesha mbegu za pamba zilizoandaliwa kitaalam  na kiwanda  cha Alliance Ginneries Wakurugenzi wa Mifuko na Mashirika pamoja na Viongozi wa mkoa wa Simiyu (hawapo pichani) walipotembelea kiwanda hicho baada ya kuona maeneo ya kujenga kiwanda cha bidhaa za Hospitali zitokanazo na pamba na kiwanda cha  maji tiba Mkoani Simiyu.
Mwakilishi kutoka Benki ya Maendeleo(TIB), Egata Makanja akizungumza katika kikao cha majumuisho ya ziara ya Wakurugenzi wa Mifuko na Mashirika waliyofanya kwa lengo la   kuona maeneo ya kujenga kiwanda cha bidhaa za Hospitali zitokanazo na pamba na kiwanda cha  maji tiba Mkoani Simiyu.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (kushoto), Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na uzalishaji, Dkt. Gamitwe Mahaza(katikati)na Mkurugenzi Mkuu waTIRDO wakifurahia jambo wakati wa ziara ya Wakurugenzi wa Mifuko na Mashirika waliyofanya kwa lengo la   kuona maeneo ya kujenga kiwanda cha bidhaa za Hospitali zitokanazo na pamba na kiwanda cha  maji Mkoani Simiyu.
Wakurugenzi wa Mifuko na Mashirika pamoja na Viongozi wa mkoa wa Simiyu  wakipokea maelezo ya namna wanavyozalisha dawa kutoka katika mti wa muorobaini inayotumika katika katika pamba hai (organic cotton) kutoka Mtaalam wa Kampuni ya Alliance Ginneries wakati walipotembelea kiwanda hicho baada ya kuona maeneo ya kujenga kiwanda cha bidhaa za Hospitali zitokanazo na pamba na kiwanda cha  maji tiba Mkoani Simiyu.
Mwakilishi wa Mamlaka ya Chakula na Dawa(TFDA), Moses Mbambe akichangia hoja katika kikao cha majumuisho ya ziara ya Wakurugenzi wa Mifuko na Mashirika waliyofanya kwa lengo la   kuona maeneo ya kujenga kiwanda cha bidhaa za Hospitali zitokanazo na pamba na kiwanda cha  maji tiba Mkoani Simiyu.
Mwakilishi wa Shirika la Viwango nchini(TBS) akichangia hoja katika kikao cha majumuisho ya ziara ya Wakurugenzi wa Mifuko na Mashirika waliyofanya kwa lengo la   kuona maeneo ya kujenga kiwanda cha bidhaa za Hospitali zitokanazo na pamba na kiwanda cha  maji tiba Mkoani Simiyu.
Katibu Tawala Msaidizi wa Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji katika Sekretarieti ya Mkoa wa Simiyu, Dkt.Gamitwe Mahaza(kushto) akichangia hoja katika kikao cha majumuisho ya ziara ya Wakurugenzi wa Mifuko na Mashirika waliyofanya kwa lengo la   kuona maeneo ya kujenga kiwanda cha bidhaa za Hospitali zitokanazo na pamba na kiwanda cha  maji tiba Mkoani Simiyu.
Baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Simiyu  wakifuatilia mjadala katika kikao cha majumuisho ya ziara ya Wakurugenzi wa Mifuko na Mashirika waliyofanya kwa lengo la   kuona maeneo ya kujenga kiwanda cha bidhaa za Hospitali zitokanazo na pamba na kiwanda cha  maji tiba Mkoani Simiyu.
Mdau wa zao la pamba na mfanyabiasha Emmanuel Gungu Silanga akichangia hoja  kikao cha majumuisho ya ziara ya Wakurugenzi wa Mifuko na Mashirika waliyofanya kwa lengo la   kuona maeneo ya kujenga kiwanda cha bidhaa za Hospitali zitokanazo na pamba na kiwanda cha  maji tiba Mkoani Simiyu
Mwenyekiti wa Halmashauriya Mji Bariadi, Mhe.Robert Mgata akichangia hoja katika kikao cha majumuisho ya ziara ya Wakurugenzi wa Mifuko na Mashirika waliyofanya kwa lengo la   kuona maeneo ya kujenga kiwanda cha bidhaa za Hospitali zitokanazo na pamba na kiwanda cha  maji tiba Mkoani Simiyu.
Diwani wa Kata ya Dutwa, Mhe.Mapolu Nunde Mkingwa kikao cha majumuisho ya ziara ya Wakurugenzi wa Mifuko na Mashirika waliyofanya kwa lengo la   kuona maeneo ya kujenga kiwanda cha bidhaa za Hospitali zitokanazo na pamba na kiwanda cha  maji tiba Mkoani Simiyu.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!