Wednesday, November 29, 2017

BILIONI 375.4 ZATOLEWA KUTEKELEZA MRADI WA KUKABILIANA NA MABADILIKO YA TABIANCHI NA KUTATUA TATIZO LA MAJI SIMIYU

Serikali ya Tanzania  kwa kushirikiana na Serikali ya  Ujerumani, Mfuko wa Mabadiliko tabia nchi (CGF) na wananchi, imetenga kiasi cha shilingi bilioni 375.4  kutekeleza Mradi wa kukabiliana na changamoto  zinazotokana na mabadiliko ya tabia nchi mkoani SIMIYU kwa awamu ya kwanza, ambao utakuwa suluhisho la kudumu la tatizo la maji mkoani humo

Hayo yamesemwa leo na Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Isack Kamwelwe wakati akifungua kikao cha wadau wa mabadiliko ya tabia nchi kilichofanyika Mjini Bariadi Mkoani Simiyu.

Waziri Kamwelwe amesema moja ya shughuli muhimu na kubwa katika utekelezaji wa Mradi wa kukabiliana na changamoto  zinazotokana na mabadiliko ya tabia nchi,  ni ufikishaji wa huduma ya Maji ya Ziwa Victoria katika Mji wa Bariadi , Busega na Itilima kwa awamu ya kwanza na baadaye katika Wilaya ya Meatu na Maswa.

Ameongeza kuwa upatikanaji wa maji katika Mkoa wa Simiyu uko chini ikilinganishwa na wastani wa Kitaifa na kwa kutambua hali hii,  Serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo ilibuni mradi huu,  ili kupata suluhisho la kudumu  la tatizo la maji kwa wananchi na mifugo ambayo ni moja ya shughuli za kiuchumi za wananchi wa Mkoa wa Simiyu.

Aidha, Waziri Kamwelwe amesema lengo la mradi huu ni kuboresha Afya na kuongeza uzalishaji  ili kuinua hali ya maisha kwa wananchi walioathirika na mabadiliko ya tabia nchi, ambapo amebainisha kuwa katika kufikia lengo shughuli mbalimbali zitatekelezwa katika nyanja za maji safi na usafi wa mazingira, kilimo endelevu na ufugaji.

Waziri pia amebainisha kuwa kutakuwa na ujenzi wa mabwawa ya kilimo cha umwagiliaji endelevu na maji ya mifugo, ujenzi wa mabwawa ya kutibu maji taka pamoja na vyoo vya mfano katika Shule na Vituo vya Afya.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka ameishukuru Serikali kwa kutekeleza mradi huo ambao utawasaidia wananchi wa mkoa huo na utakuwa chachu katika Ujenzi wa Viwanda mkoani humo kwa kuwezesha upatikanaji wa maji ya uhakika.

“Wananchi wa Mkoa wa Simiyu wote wanausubiri sana mradi huu wa maji ya Ziwa Victoria; pia Mkoa wetu unaenda kwenye uwekezaji wa viwanda vikubwa na changamoto tuliyonayo ni suala la upatikanaji wa maji ya uhakika, utekelezaji wa mradi huu utatusaidia sana katika viwanda” amesema Mtaka.

Katibu Mkuu Wizara ya Maji na Umwagiliaji Profesa Kitila Mkumbo amesema kuwa Simiyu ni Miongoni mwa Mikoa yenye kiwango cha chini cha upatikanaji wa huduma ya maji ambayo Serikali imetoa kiupaumbele cha kuipa fedha kutoka katika Fedha za Mfuko wa Maji ili kutekeleza miradi ya maji itakayoibuliwa na kuwasilisha maandiko yake wizarani.

Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Ndg.Jumanne Sagini amewahimiza Wataalam wa Halmashauri kwa kushirikiana na Mkoa kuandaa maandiko ya kuibua miradi ya Maji itakayowasilishwa wizara ya maji,  kwa lengo la kuomba fedha za  kutekeleza miradi hiyo ili kuongeza na kuboresha upatikanaji wa huduma za maji mkoani humo.

Mradi wa kukabiliana na changamoto  zinazotokana na mabadiliko ya tabianchi Mkoani SIMIYU ambao zabuni yake imepangwa kutangazwa Januari 2018; utatekelezwa kwa awamu mbili awamu ya kwanza utaanza na Mji wa Bariadi, Busega na Itilima pamoja na vijiji 278 vilivyopo pembezoni mwa bomba kuu umbali wa Kilomita 12 kila upande,  baadaye maeneo mengine ya Wilaya za Maswa na Meatu.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi .Isack Kamwelwe  akifungua kikao cha Wadau wa Mradi wa  kukabiliana na changamoto zitokanazo na  Mabadiliko ya Tabianchi (hawapo pichani) unaotekelezwa katika Mkoa wa Simiyu kilichofanyika Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili mikakati ya utekelezaji wa mradi huo

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka akizungumza na Wadau wa Mradi wa  kukabiliana na changamoto zitokanazo  na Mabadiliko ya Tabianchi (hawapo pichani) unaotekelezwa Mkoani humo, katika kikao kilichofanyika Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili mikakati ya utekelezaji wa mradi huo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Profesa Kitila Mkumbo akizungumza na  Wadau wa Mradi wa  kukabiliana na changamoto zitokanazo na Mabadiliko ya Tabianchi (hawapo pichani) unaotekelezwa Mkoani Simiyu  kwenye kikao kilichofanyika Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili mikakati ya utekelezaji wa mradi huo.
Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Jumanne Sagini akichangia hoja katika kikao cha Wadau wa Mradi wa  kukabiliana na changamoto zitokanazo na Mabadiliko ya Tabianchi, unaotekelezwa Mkoani humo kilichofanyika Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili mikakati ya utekelezaji wa mradi huo.
Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Mhe.Dkt.Joseph Chilongani akichangia hoja katika kikao cha Wadau wa Mradi wa  kukabiliana na changamoto zitokanazo na Mabadiliko ya Tabianchi , unaotekelezwa Mkoani Simiyu,  kilichofanyika Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili mikakati ya utekelezaji wa mradi huo.
Mbunge wa Jimbo la Maswa Magharibi Mhe.Mashimba Ndaki akichangia hoja katika kikao cha Wadau wa Mradi wa  kukabiliana na changamoto zitokanazo na Mabadiliko ya Tabianchi , unaotekelezwa Mkoani humo kilichofanyika Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili mikakati ya utekelezaji wa mradi huo.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Bariadi, Mhe.Robert Lweyo akichangia hoja katika kikao cha Wadau wa Mradi wa  kukabiliana na changamoto zitokanazo na Mabadiliko ya Tabianchi ( baadhi hawapo pichani) unaotekelezwa Mkoani Simiyu kilichofanyika Mjini hapo kwa lengo la kujadili mikakati ya utekelezaji wa mradi huo.
PICHA H:-Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Itilima, Ndg.Mariano Mwanyigu akichangia hoja katika kikao cha Wadau wa Mradi wa  kukabiliana na changamoto  zitokanazo na Mabadiliko ya Tabianchi (baadhi hawapo pichani) unaotekelezwa Mkoani Simiyu kilichofanyika Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili mikakati ya utekelezaji wa mradi huo.
Mwakilishi wa Tume ya Mpango wa Matumizi Bora ya Ardhi, Bi.Pili Msati akichangia hoja katika kikao cha Wadau wa Mradi wa  kukabiliana na changamoto zitokanazo na Mabadiliko ya Tabianchi (hawapo pichani) unaotekelezwa Mkoani Simiyu kilichofanyika Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili mikakati ya utekelezaji wa mradi huo.
Katibu Mwenezi wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe.Jeremia Shigala akichangia hoja katika kikao cha Wadau wa Mradi wa  kukabiliana na changamoto zitokanazo na Mabadiliko ya Tabianchi unaotekelezwa Mkoani humo kilichofanyika Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili mikakati ya utekelezaji wa mradi huo.
Baadhi ya wadau wa Mradi wa kukabiliana na changamoto zitokanazo na Mabadiliko ya Tabianchi  unaotekelezwa Mkoani Simiyu akifuatilia masuala mbalimbali yalikuwa yakijadiliwa katika kikao kilichofanyika mjini Bariadi kwa lengo la kujadili mikakati ya utekelezaji wa mradi huo
Baadhi ya wadau wa Mradi wa kukabiliana na changamoto zitokanazo na Mabadiliko ya Tabianchi  unaotekelezwa Mkoani Simiyu akifuatilia masuala mbalimbali yalikuwa yakijadiliwa katika kikao kilichofanyika mjini Bariadi kwa lengo la kujadili mikakati ya utekelezaji wa mradi huo.
Mkuu wa Wilaya ya Busega, Mhe.Tano Mwera akichangia hoja katika kikao cha Wadau wa Mradi wa  kukabiliana na changamoto zitokanazo na Mabadiliko ya Tabianchi unaotekelezwa Mkoani humo kilichofanyika Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili mikakati ya utekelezaji wa mradi huo.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Isack Kamwelwe(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Mkoa wa Simiyu na wadau wa Mradi wa kukabiliana na changamoto zitokanazo na Mabadiliko ya Tabianchi  unaotekelezwa Mkoani humo mara baada ya ufunguzi wa kikao cha wadau hao kilichofanyika Mjini Bariadi.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Isack Kamwelwe(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Mkoa wa Simiyu na wadau wa Mradi wa kukabiliana na changamoto zitokanazo na Mabadiliko ya Tabianchi  unaotekelezwa Mkoani humo mara baada ya ufunguzi wa kikao cha wadau hao kilichofanyika Mjini Bariadi.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Isack Kamwelwe(kulia) na KATIBU Mkuu wa Wizara hiyo, Profesa Kitila Mkumbo wakisaini vitabu vya wageni katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,  baada ya kuwasili mkoani hapo kwa ajili ya kushiriki  kikao cha Wadau wa Mradi wa  kukabiliana na changamoto zitokanazo na  Mabadiliko ya Tabianchi  unaotekelezwa Mkoani humo, kilichofanyika Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili mikakati ya utekelezaji wa mradi huo.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!