Thursday, January 4, 2018

ANGELINA MABULA: HALMASHAURI ZITUMIE WATAALAM WAKE KUPIMA MAENEO ILI KUWAPUNGUZIA ADHA WANANCHI

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe.Angelina Mabula amezitaka Halmashauri mkoani Simiyu kutumia Wataalam wake kupima maeneo ili wananchi waweze kupata hati miliki ya maeneo yao na kupunguza adha mbalimbali hususani migogoro.

Mhe.Mabula ameyasema hayo wakati wa ziara yake Mkoani Simiyu iliyokuwa na lengo la kukagua jengo litakalotumika kama Ofisi ya Kanda ya Ardhi ya Simiyu na kufuatilia utekelezaji wa maelekezo aliyotoa wakati wa ziara yake mwezi Agosti mwaka jana Mjini Bariadi.

Amesema ikiwa kuna Halmashauri inahitaji kupima viwanja na mashamba na ina watumishi wachache katika Idara ya Ardhi ufanyike utaratibu wa kuomba watumishi kutoka katika halmashauri nyingine ili waweze kuungana na kuweka kambi katika Halmashauri husika wafanye kazi ya kuwahudumia wananchi wengi kwa wakati mmoja.

“ Hatuna wataalam wa kutosha kuweza kupima viwanja vingi kwa wakati mmoja katika Halmashauri, lakini tunao wataalam katika Mkoa husika ambao tulishasema kama kuna uhitaji wa kupima maeneo katika Halmashauri moja wataalam wote ndani ya mkoa wakusanywe waweke kambi hapo mpaka hiyo kazi iishe , wakimaliza wanahamia wilaya nyingine” alisisitiza Mabula.

Ameongeza kuwa Halmashauri yoyote itakapoona ina uhitaji wa watalaam kutoka Ofisi ya Kanda kwa ajili ya kuongeza nguvu katika zoezi la upimaji, Ofisi hiyo ipo tayari kufanya kazi na Halmashauri yoyote itakayoomba.

Aidha, amezitaka Halmashauri mkoani Simiyu kupima maeneo yote ya Mjini pamoja na maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya ujenzi wa viwanda na uwekezaji.

Kwa upande wake Kaimu Kamishna wa Kanda ya Ardhi ya Simiyu, Ndg. Makwasa Biswalo ametoa wito kwa Watalaam mkoani humo kuona namna ya kutenga eneo la mipango miji katika eneo lililopitiwa na barabara ya lami ya  kilomita 70 kutoka Bariadi mpaka Lamadi(kilomita kadhaa kwenye kila upande wa barabara) ambalo ni eneo zuri kwa ajili ya uwekezaji.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka amesema ameshazungumza na Watendaji wa Halmashauri zinazopitiwa na barabara hiyo ya Bariadi-Lamadi(KM 70) kuwa,  waone  namna Halmashauri hizo zinavyoweza kumiliki maeneo hayo walau kilomita moja kushoto na kulia kwa barabara hiyo.
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo na Makazi, Mhe. Angelina Mabula(wa tatu kushoto) akiangalia baadhi ya hati za kimila zilizoandaliwa kwa ajili wananchi wa Wilaya ya Bariadi katika Ofisi ya Idara ya Ardhi ya Halmashauri hiyo, wakati wa ziara yake Mkoani Simiyu.


Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo na Makazi, Mhe. Angelina Mabula akizungumza na viongozi wa Mkoa wa Simiyu wakati wa ziara yake Mkoani humo, (kushoto) Mkuu wa Mkoa huo, Mhe.Anthony Mtaka.
 Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka (kushoto) akizungumza na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo na Makazi, Mhe. Angelina Mabula alipokuwa Mkoani humo kwa ziara ya siku moja.


 Kaimu Kamishna wa Ardhi Kanda ya Simiyu,Ndg.Makwasa Biswalo akifafanua jambo wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo na Makazi, Mhe. Angelina Mabula Mkoani Simiyu,(kulia) Afisa Ardhi Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Bi.Grace Mgombera.
Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu,Ndg.Jumanne Sagini akifafanua jambo wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo na Makazi, Mhe. Angelina Mabula Mkoani Simiyu.
Mkuu wa Idara ya Ardhi  na Maliasili katika Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, Ndg.Mazengo Sabaya akifafanua jambo wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo na Makazi, Mhe. Angelina Mabula Mkoani Simiyu.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, Ndg.Abdallah Malela akifafanua jambo wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya  Makazi, Mhe. Angelina Mabula Mkoani Simiyu.
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe.Angelina Mabula(kulia) akitoa maelekezo kwa baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Simiyu baada ya kukagua Jengo la Ofisi linalotarajiwa kutumika kama Ofisi ya muda ya Kanda ya Ardhi Simiyu, wakati wa ziara yake Mkoani humo.
Baadhi ya viongozi na wataalam wa Mkoa wa Simiyu wakimsikiliza Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe.Angelina Mabula (hayupo pichani) wakati wa ziara yake Mkoani humo.
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe.Angelina Mabula(kulia) pamoja na baadhi ya viongozi na Watalaam wa Mkoa wa Simiyu akitoka katika  Jengo  linalotarajiwa kutumika kama Ofisi ya muda ya Kanda ya Ardhi Simiyu, wakati wa ziara yake Mkoani humo, (kushoto) Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe.Festo Kiswaga.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!